Rais Samia, ikitupendeza futa Jeshi la Polisi, Tuletee Huduma ya Polisi

50thebe

JF-Expert Member
Mar 10, 2011
3,875
3,730
Mheshimiwa Rais

Nianze kwa kukusalimu kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lengo ni lile lile la kazi iendee.

Tumekuwa na mijadala nchini mwetu kwa nyakati tofauti kuhusu namna Jeshi letu la Polisi linavyofanya kazi. Mara nyingi Jeshi limekuwa likishutumiwa kwa masuala kadhaa ikiwamo kujihusisha na vitendo vya Rushwa, kubambikia watu kesi, kushirikiana na wahalifu na masuala mengine kama hayo. Pengine sio rahisi sana kuthibitisha tuhuma hizi.

Hivyo basi, napenda nitumie fursa hii kupendekeza kwako ulifumue na kuliunda upya Jeshi la Polisi. Kwamba Polisi iwe ni huduma kama huduma za uhamiaji. Kwa mfano, badala ya kuwa na Jeshi la Polisi tuwe na Huduma ya Polisi. Vivyo hivyo tuwe na Huduma ya Magereza etc.

Mambo ya Kijeshi yabaki kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Imani yangu ni kwamba tukiwa na Huduma ya Polisi chombo hiki kitajikita kuelimisha Raia huku kikitekeleza majukumu ya ulinzi wa Raia na Mali zao. Kwenye jumuiya yetu ya SADC wenzetu wa Botswana hawana Jeshi la Polisi badala yake Wana huduma ya Polisi. Natumai tunaweza kujifunza kwao.

Hivyo basi ikikupendeza Mheshimiwa Rais waweza kuelekeza vyombo vyako vifanye uchunguzi na utafiti zaidi kuhusu hili kwa kuzingatia mazingira ya nchi yetu na maendeleo yetu. Kisha utujalie tupate chombo hiki cha Huduma ya Polisi.

Nawasilisha.
 
Wazo limetoka,kama ungeandika pia mfumo huo unafanyaje kazi,tofauti ya kuwa jeshi na huduma ni ipi japo umedokeza kidogo lakini ungeeleza zaidi hizo faida kulinganisha na changamoto zilizopo.Ukifanya hivyo hoja yako itapata mashiko hata na wale ambao wanatarajia kukupinga pasi na kujua unacho jengea hoja watakao kupinga ni wale majuao unacho simamia.Ngoja wakuu waje nami ntarudi....
 
Mluu ni mambo gani ambayo yakiondolewa itafanya polisi isiwe jeshi badala yake iwe huduma ?
 
Mluu ni mambo gani ambayo yakiondolewa itafanya polisi isiwe jeshi badala yake iwe huduma ?

Mwelekeo uwe kuelimisha Raia zaidi badala ya ilivyo sasa kwamba ukiwa mikononi mwa Polisi uhai wako unakuwa mashakani. Badala yake uwe salama ukiwa mikononi mwa Polisi.

Sio kwamba ukiwa mikononi mwa Polisi kesho yake tukute umekufa.
 
Mheshimiwa Rais

Nianze kwa kukusalimu kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lengo ni lile lile la kazi iendee.

Tumekuwa na mijadala nchini mwetu kwa nyakati tofauti kuhusu namna Jeshi letu la Polisi linavyofanya kazi. Mara nyingi Jeshi limekuwa likishutumiwa kwa masuala kadhaa ikiwamo kujihusisha na vitendo vya Rushwa, kubambikia watu kesi, kushirikiana na wahalifu na masuala mengine kama hayo. Pengine sio rahisi sana kuthibitisha tuhuma hizi.

Hivyo basi, napenda nitumie fursa hii kupendekeza kwako ulifumue na kuliunda upya Jeshi la Polisi. Kwamba Polisi iwe ni huduma kama huduma za uhamiaji. Kwa mfano, badala ya kuwa na Jeshi la Polisi tuwe na Huduma ya Polisi. Vivyo hivyo tuwe na Huduma ya Magereza etc.

Mambo ya Kijeshi yabaki kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Imani yangu ni kwamba tukiwa na Huduma ya Polisi chombo hiki kitajikita kuelimisha Raia huku kikitekeleza majukumu ya ulinzi wa Raia na Mali zao. Kwenye jumuiya yetu ya SADC wenzetu wa Botswana hawana Jeshi la Polisi badala yake Wana huduma ya Polisi. Natumai tunaweza kujifunza kwao.

Hivyo basi ikikupendeza Mheshimiwa Rais waweza kuelekeza vyombo vyako vifanye uchunguzi na utafiti zaidi kuhusu hili kwa kuzingatia mazingira ya nchi yetu na maendeleo yetu. Kisha utujalie tupate chombo hiki cha Huduma ya Polisi.

Nawasilisha.
Yaani hilo jeshi usiliguse ndugu. Tunalitegemea mno chama chetu wakati wa uchaguzi
Ila katiba yetu ni kichekesho cha mwaka
 
Mwelekeo uwe kuelimisha Raia zaidi badala ya ilivyo sasa kwamba ukiwa mikononi mwa Polisi uhai wako unakuwa mashakani. Badala yake uwe salama ukiwa mikononi mwa Polisi.

Sio kwamba ukiwa mikononi mwa Polisi kesho yake tukute umekufa.
Unataka kuniambia kuwa kurekebisha huu mwelekeo lazima jeshi livunje ili iwe huduma hapo ndo wataweza kurekebisha mwelekeo ?

Au inawezekana kurekebisha mwelekeo huu wakati polisi likiwa bado jeshi na huduma bado zikapatikana ?
 
Unataka kuniambia kuwa kurekebisha huu mwelekeo lazima jeshi livunje ili iwe huduma hapo ndo wataweza kurekebisha mwelekeo ?

Au inawezekana kurekebisha mwelekeo huu wakati polisi likiwa bado jeshi na huduma bado zikapatikana ?
Mandate ya Jeshi ni mwendo wa Kijeshi.

Mandate ya Huduma ni mwendo wa Huduma.
 
Mandate ya Jeshi ni mwendo wa Kijeshi.

Mandate ya Huduma ni mwendo wa Huduma.
Haya maneno yako tafsiri yake ni kuwa lazima jeshi livunje ili iwe huduma hapo ndo wataweza kurekebisha mwelekeo na kuwa huduma.

Sasa mimi nakuuliza mkuu ni mambo gani unahisi yaondolewe ili lisiwe jeshi badala yake iwe ni taasisi ya huduma tu
 
hata mimi ningependa polisi iwe huduma polisi kuwe na vitengo
kwa mfano polisi wa homicide mambo ya mauaji, maswala ya homeland and national security , DSM iwe na kitengo chake cha police Dpd apd yaani kama mbele huko
 
Back
Top Bottom