BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Rais Samia ametoa kauli hiyo kwenye ufunguzi wa Kikao cha Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi, ambapo amesema amekuwa akipata jumbe zinazoonesha bado kuna Kesi za Kubambikizwa kwenye Vituo vya Polisi Nchini.
Rais amelitaka Jeshi la Polisi kulifanyia kazi tatizo hilo ili wanaofikishwa kwenye Mikono ya Sheria wawe na Makosa ya Kweli na sio ya kukomoana. Amesema kwasababu Wananchi wanalalamika na yeye anasikia hivyo ameona ni vema kulifikisha hilo kwao.
Hivi karibuni, Tume ya kuangalia namna ya kuboresha Taasisi za Haki Jinai iliwasilisha Ripoti kwa Rais iliyoonesha malalamiko ya Wananchi kubambikiwa Mashtaka na baadhi ya Askari yameongezeka katika Vituo vya Polisi Nchini.