Mpaka sasa wenye uelewa wa kawaida tu wanafahamu ni nini mama Samia anakiandaa kwa siku zijazo hususani 2025. Mama na CCM wanajua fika kuwa bila rafu mambo yatakuwa magumu sana 2025.
Kila wakati historia imeonesha kuwa pamoja na CCM kuwa madarakani na kujinasibu kama chama makini na kujiuza kwa miradi kemkem, CCM haijaweza kukubali kuruhusu uchaguzi huru na wa haki.
Shinikizo la katiba mpya limeonesha wazi kwa watawala kutokuwa tayari kwa mabadiliko, na hata mchakato wa katiba mpya kukamilika itakuwa ni kati ya 2025 kuelekea 2030 baada ya uchaguzi.
Watawala wetu wapo tayari kufanya chochote ile wabaki madarakani, na wanaelewa njia "nzuri" ni kucheza rafu, kwani bila hivyo hawatoboi. Kwanini CCM wamefumba macho hata baada ya rekodi mbaya ya Makonda kuhusu haki za binadamu?
Magufuli alimtumia Sabaya pale nyumbani kwa Mbowe jimbo la Hai, na kanda ya Kaskazini. Sabaya alikuwa hazuiliki na mtu yeyote kwani alikuwa na maagizo kutoka juu. Hata mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakati ule mama Anna Magwira alijibiwa kwa kiburi na jeuri na kijana Sabaya kwani Sabaya alikuwa na uhakika kwamba hakuna madhara yoyote.
Kibri na jeuri tunazoona sasa kutoka kwa Paul Makonda hadi kufikia hatua ya kuwaamrisha Waziri Mkuu, mawaziri na watendaji wakubwa wa serikali sio hivihivi, ana ruhusa kutoka juu.
Kwa namna hii navyomjua Makonda, atatenda mengi sana na kuvuka mipaka kama alivyofanya Sabaya. Inajulikana pia kwamba wakati wa Magufuli Makonda aliwekewa red tape na jumuiya ya kimataifa hasa Marekani kama mtu anayekiuka haki za binadamu.
Je, ni kwanini Mama amemchagua hata baada ya rekodi hii mbaya kimataifa? Hakuna watu safi nchi hii? Hakuna namna nyingine ya CCM kufanikiwa bila rafu za akina Sabaya na Makonda?
Kila wakati historia imeonesha kuwa pamoja na CCM kuwa madarakani na kujinasibu kama chama makini na kujiuza kwa miradi kemkem, CCM haijaweza kukubali kuruhusu uchaguzi huru na wa haki.
Shinikizo la katiba mpya limeonesha wazi kwa watawala kutokuwa tayari kwa mabadiliko, na hata mchakato wa katiba mpya kukamilika itakuwa ni kati ya 2025 kuelekea 2030 baada ya uchaguzi.
Watawala wetu wapo tayari kufanya chochote ile wabaki madarakani, na wanaelewa njia "nzuri" ni kucheza rafu, kwani bila hivyo hawatoboi. Kwanini CCM wamefumba macho hata baada ya rekodi mbaya ya Makonda kuhusu haki za binadamu?
Magufuli alimtumia Sabaya pale nyumbani kwa Mbowe jimbo la Hai, na kanda ya Kaskazini. Sabaya alikuwa hazuiliki na mtu yeyote kwani alikuwa na maagizo kutoka juu. Hata mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakati ule mama Anna Magwira alijibiwa kwa kiburi na jeuri na kijana Sabaya kwani Sabaya alikuwa na uhakika kwamba hakuna madhara yoyote.
Kibri na jeuri tunazoona sasa kutoka kwa Paul Makonda hadi kufikia hatua ya kuwaamrisha Waziri Mkuu, mawaziri na watendaji wakubwa wa serikali sio hivihivi, ana ruhusa kutoka juu.
Kwa namna hii navyomjua Makonda, atatenda mengi sana na kuvuka mipaka kama alivyofanya Sabaya. Inajulikana pia kwamba wakati wa Magufuli Makonda aliwekewa red tape na jumuiya ya kimataifa hasa Marekani kama mtu anayekiuka haki za binadamu.
Je, ni kwanini Mama amemchagua hata baada ya rekodi hii mbaya kimataifa? Hakuna watu safi nchi hii? Hakuna namna nyingine ya CCM kufanikiwa bila rafu za akina Sabaya na Makonda?