Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,815
- 11,992
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) tarehe 26 Julai, 2023 jijini Dar es Salaam.
===
Rais Samia anazungumza
Ninayo furaha kubwa kuwakaribisha Tanzania. Tunakutana leo kujadili ajenda mabyo ndio moyo wa mataifa yetu. Mkutano wetu wa leo utaamua ni aina gani ya uwekezaji tunafanya, hakuna muda mwingine wa kujadili haya isipokuwa sasa.
Ni jambo la kusikitisha kuwa baadhi ya nchi za Afrika ukuaji wa uchumi haujakua hasa kuchochea ajira mpya kwa vijana, pia bara la Afrika bado linakabiliwa na matatizo ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana, njaa n.k
Bara letu lina watoto na vijana wengi, tunapaswa kuwekeza kwenye rasilimali watu. Kwetu sisi tuliopo hata tujiulize, bara tulilotithi ndilo bara tunalotaka kuwaachia vijana wetu warithi?
Mwalimu JK Nyerere aliwahi kunukuliwa akisema maendeleo ni watu, watu ndio walengwa na wanufaika wa chochote kinachoitwa maendeleo. Hatuwezi kuliomboa bara letu pasipo kuwekeza kwa rasilimali watu, tangu mtoto anapozaliwa kwa maana ya upatikanani wa lishe bora na chanjo ili kupunguza udumavu.
Pia elimu ili kuwaandaa watoto vizuri, mitaala ikidhi mahitaji ya sasa.
Nelson Mandela alisema Elimu ndio silaha yenye nguvu zaidi inayoweza kutumika kuubadilisha ulimwengu. Kama Tanzania, tumetenga fedha nyingi kwa ajili ya afua mbalimbali za lishe na afya ya mama, kuanzisha vituo vya elimu ya awali, mapitio ya sera ya elimu, programu na mitaala ya elimu, uanzishaji wa mfuko wa kusaidia familia maskini, uanzishaji wa programu ya elimu bila malipo kuanzia shule za msinhgi hadi form 6.
Kuwezesha vijana kiuchumi kwa kutoa 4%, kwa wanawake 4% na watu wenye ulemavu 2%. Pia, kuruhusu waliopata ujauzito kurejea shuleni, pamoja na kuwekeza kwenye kilimo.
Idadi kubwa ya vijana tulionao Afrika ni fursa pekee ni fursa kubwa, vijana hawa wanapaswa kuendelezwa.
Vijana wafundishwe kuhusu uzazi wa mpango, tuhakikishe elimu tunayotoa inakuwa na tija kwa vijana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Madagascar Mhe. Andry Nirina Rajoelina mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa São Tomé na Principe, Carlos Vila Nova mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Kenya, William Ruto mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Sierra Leone Mhe. Julius Maada Bio mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa kando ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika Bi. Victoria Kwakwa pamoja na ujumbe wake mara baada ya mazungumzo kando ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
===
Rais Samia anazungumza
Ninayo furaha kubwa kuwakaribisha Tanzania. Tunakutana leo kujadili ajenda mabyo ndio moyo wa mataifa yetu. Mkutano wetu wa leo utaamua ni aina gani ya uwekezaji tunafanya, hakuna muda mwingine wa kujadili haya isipokuwa sasa.
Ni jambo la kusikitisha kuwa baadhi ya nchi za Afrika ukuaji wa uchumi haujakua hasa kuchochea ajira mpya kwa vijana, pia bara la Afrika bado linakabiliwa na matatizo ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana, njaa n.k
Bara letu lina watoto na vijana wengi, tunapaswa kuwekeza kwenye rasilimali watu. Kwetu sisi tuliopo hata tujiulize, bara tulilotithi ndilo bara tunalotaka kuwaachia vijana wetu warithi?
Mwalimu JK Nyerere aliwahi kunukuliwa akisema maendeleo ni watu, watu ndio walengwa na wanufaika wa chochote kinachoitwa maendeleo. Hatuwezi kuliomboa bara letu pasipo kuwekeza kwa rasilimali watu, tangu mtoto anapozaliwa kwa maana ya upatikanani wa lishe bora na chanjo ili kupunguza udumavu.
Pia elimu ili kuwaandaa watoto vizuri, mitaala ikidhi mahitaji ya sasa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) uliofanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Nelson Mandela alisema Elimu ndio silaha yenye nguvu zaidi inayoweza kutumika kuubadilisha ulimwengu. Kama Tanzania, tumetenga fedha nyingi kwa ajili ya afua mbalimbali za lishe na afya ya mama, kuanzisha vituo vya elimu ya awali, mapitio ya sera ya elimu, programu na mitaala ya elimu, uanzishaji wa mfuko wa kusaidia familia maskini, uanzishaji wa programu ya elimu bila malipo kuanzia shule za msinhgi hadi form 6.
Kuwezesha vijana kiuchumi kwa kutoa 4%, kwa wanawake 4% na watu wenye ulemavu 2%. Pia, kuruhusu waliopata ujauzito kurejea shuleni, pamoja na kuwekeza kwenye kilimo.
Idadi kubwa ya vijana tulionao Afrika ni fursa pekee ni fursa kubwa, vijana hawa wanapaswa kuendelezwa.
Vijana wafundishwe kuhusu uzazi wa mpango, tuhakikishe elimu tunayotoa inakuwa na tija kwa vijana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Madagascar Mhe. Andry Nirina Rajoelina mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa São Tomé na Principe, Carlos Vila Nova mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Kenya, William Ruto mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Sierra Leone Mhe. Julius Maada Bio mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa kando ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika Bi. Victoria Kwakwa pamoja na ujumbe wake mara baada ya mazungumzo kando ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2023.