Rais Samia amefanya Uteuzi na Uhamisho wa viongozi mbalimbali leo tarehe 14.12.2023

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,313
UTEUZI:
Rais wa Tanzania, Dtk. Samia Suluhu Hassan amemteua Michael Kachoma kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega akichukua nafasi nafasi ya Veronica Vicent Sayore ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Rais Samia pia amemteua Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Wanging’ombe Maryam Ahmed Muhaji kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara akichukua nafasi ya Karoline Albert Mthapula ambaye atapangiwa kazi nyingine na amemteua Afisa Mwandamizi katika Mfuko wa Taifa wa Maji, Zuhura Abdulrahman Rashid kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Ruangwa akichukua nafasi ya Shamim Sadiq ambaye atapangiwa kazi nyingine.

UHAMISHO:

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uhamisho wa Wakuu wa Wilaya sita ambapo amemuhamisha Maveka Simon Maveka kutoka Wilaya ya Chunya kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa na Remidius Mwema Emmanuel amehamishwa kutoka Wilaya ya Kongwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto.

Amemuhamisha pia Mbaraka Alhaji Batenga kutoka Wilaya ya Kiteto kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chunya na Kanali Hamis Mayamba Maiga amehamishwa kutoka Wilaya ya Rombo kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Misenyi huku Kanali Wilson Christian Sakullo akihamishwa kutoka Wilaya ya Misenyi kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro na Raymond Stephen Mwangwala amehamishwa kutoka Wilaya ya Ngorongoro kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rombo.

Katika hatua nyingine Rais Samia amefanya uhamisho wa Wakurugenzi wa Halmashauri 15 ambapo amemuhamisha Rose Robert Manumba kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi, Rehema Said Bwasi amehamishwa kutoka Malinyi kwenda kuwa Mkurugenzi Mendaji wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu.

Yefred Edson Myenzi amehamishwa kutoka Mbulu kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Geita akichukua nafasi ya Zahara Muhiddin Michuzi ambaye amehamishiwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara.

Lena Martin Nkya amehamishwa kutoka Ifakara kwenda kuwa DED
Tunduma na Chiriku Hams Chilumba amehamishwa kutoka Namtumbo kwenda kuwa Mkurugenzi DED Kigoma, Kisena Magena Mabuba amehamishwa kutoka Kilosa kwenda kuwa DED Shinyanga akichukua nafasi ya Simon Sales Berege ambaye anakwenda kuwa DED Rufiji akichukua nafasi ya Michael John Gwimile ambaye anakwenda kuwa DED Kilosa.

Wengine ni Regina Lazaro Bieda ambaye amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Momba kwenda kuwa DED Kibaha, Mwajuma Abasy Nasombe amehamishwa kutoka Mwanga kwenda kuwa DED Moshi na Rashid Karim Gembe amehamishwa kutoka Moshi kwenda kuwa DED Mkinga.

Zahara Abdul Msangi amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga na Philemon Mwita Magesa amehamishwa kutoka Tunduma kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo na Butamo Nuru Ndalahwa amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Momba.

20231214_013507.jpg


20231214_013512.jpg


20231214_013515.jpg
 
Usiku wa manane ndiyo mambo mengi hufanyika.

Ma-DED wanaenda kujifunza mapya katika wilaya walizohamishiwa wakati ndiyo kwanza walikuwa wageni katika vituo vyao vya awali.

Kwa mtindo huu maDED watakuwa wanaendelea kuwa wageni katika vituo vyao kadhaa vya kazi hadi watenguliwe au kustaafu.

Madhara yanakuwa hakuna muuendelezo thabiti wa kile wanachobuni maDED pia madhara makubwa ni wilaya hizo kukosa maendelea endelevu kutokana na mambo kuamuliwa kutoka ikulu Dodoma au ikulu ya DSM .

Serikali Kuu Dodoma / DSM imehodhi mamlaka yote hata kwa kile cha wilayani huku serikali hiyo kuu haifahamu kwa ndani matamanio ya raia wa hizo wilaya 123 zenye mazingira na vipaumbele tofauti tofauti.

Serikali za mfumo wa ugatuzi kuzipa majimbo mamlaka zaidi ya maamuzi inahitajika.

Na hili ili kufanikiwa, lazima maamuzi ya maendeleo ya wananchi wilayani linahitaji katiba mpya ya majimbo.

Katiba mpya itakayo washirikisha Wananchi kuwa na sauti pia mamlaka katika maeneo yao (wilayani) kupewa uwezo wa kusimamia viongozi na kuwatimua ikibidi, ili miradi ya mazingira, afya, miundombinu ya kuunganisha barabara za vijiji, elimu, kilimo, visima vya maji iweze kufanikiwa wilayani na majimboni..
 
UTEUZI:
Rais wa Tanzania, Dtk. Samia Suluhu Hassan amemteua Michael Kachoma kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega akichukua nafasi nafasi ya Veronica Vicent Sayore ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Rais Samia pia amemteua Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Wanging’ombe Maryam Ahmed Muhaji kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara akichukua nafasi ya Karoline Albert Mthapula ambaye atapangiwa kazi nyingine na amemteua Afisa Mwandamizi katika Mfuko wa Taifa wa Maji, Zuhura Abdulrahman Rashid kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Ruangwa akichukua nafasi ya Shamim Sadiq ambaye atapangiwa kazi nyingine.

UHAMISHO:
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uhamisho wa Wakuu wa Wilaya sita ambapo amemuhamisha Maveka Simon Maveka kutoka Wilaya ya Chunya kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa na Remidius Mwema Emmanuel amehamishwa kutoka Wilaya ya Kongwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto.

Amemuhamisha pia Mbaraka Alhaji Batenga kutoka Wilaya ya Kiteto kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chunya na Kanali Hamis Mayamba Maiga amehamishwa kutoka Wilaya ya Rombo kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Misenyi huku Kanali Wilson Christian Sakullo akihamishwa kutoka Wilaya ya Misenyi kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro na Raymond Stephen Mwangwala amehamishwa kutoka Wilaya ya Ngorongoro kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rombo.

Katika hatua nyingine Rais Samia amefanya uhamisho wa Wakurugenzi wa Halmashauri 15 ambapo amemuhamisha Rose Robert Manumba kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi, Rehema Said Bwasi amehamishwa kutoka Malinyi kwenda kuwa Mkurugenzi Mendaji wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu.

Yefred Edson Myenzi amehamishwa kutoka Mbulu kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Geita akichukua nafasi ya Zahara Muhiddin Michuzi ambaye amehamishiwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara.

Lena Martin Nkya amehamishwa kutoka Ifakara kwenda kuwa DED
Tunduma na Chiriku Hams Chilumba amehamishwa kutoka Namtumbo kwenda kuwa Mkurugenzi DED Kigoma, Kisena Magena Mabuba amehamishwa kutoka Kilosa kwenda kuwa DED Shinyanga akichukua nafasi ya Simon Sales Berege ambaye anakwenda kuwa DED Rufiji akichukua nafasi ya Michael John Gwimile ambaye anakwenda kuwa DED Kilosa.

Wengine ni Regina Lazaro Bieda ambaye amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Momba kwenda kuwa DED Kibaha, Mwajuma Abasy Nasombe amehamishwa kutoka Mwanga kwenda kuwa DED Moshi na Rashid Karim Gembe amehamishwa kutoka Moshi kwenda kuwa DED Mkinga.

Zahara Abdul Msangi amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga na Philemon Mwita Magesa amehamishwa kutoka Tunduma kwenda kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo na Butamo Nuru Ndalahwa amehamishwa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba.

1702513727053.jpg

1702513734310.jpg

Screenshot_20231214-040522_1.jpg
 
UTEUZI:
Rais wa Tanzania, Dtk. Samia Suluhu Hassan amemteua Michael Kachoma kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya
*Maveka Simon Maveka kutoka Wilaya ya Chunya *

CCM MUNGU AWABARIKI, huyu akikuwa mchimbaji wa madini amewasumbua sana wachimbaji wadogo huko chunya!

Kongwa sasa akachungwe ng’ombe !
Anazo leseni nyingi sana za uchimbaji wa dhahabu huko chunya pia serikali imfuatilie sana huyu bwana!
 
Usiku wa manane ndiyo mambo mengi hufanyika.

Ma-DED wanaenda kujifunza mapya katika wilaya walizohamishiwa wakati ndiyo kwanza walikuwa wageni katika vituo vyao vya awali.

Kwa mtindo huu maDED watakuwa wanaendelea kuwa wageni katika vituo vyao kadhaa vya kazi hadi watenguliwe au kustaafu.

Madhara yanakuwa hakuna muuendelezo thabiti wa kile wanachobuni maDED pia madhara makubwa ni wilaya hizo kukosa maendelea endelevu kutokana na mambo kuamuliwa kutoka ikulu Dodoma au ikulu ya DSM .

Serikali Kuu Dodoma / DSM imehodhi mamlaka yote hata kwa kile cha wilayani huku serikali hiyo kuu haifahamu kwa ndani matamanio ya raia wa hizo wilaya 123 zenye mazingira na vipaumbele tofauti tofauti.

Serikali za mfumo wa ugatuzi kuzipa majimbo mamlaka zaidi ya maamuzi inahitajika.

Na hili ili kufanikiwa maamuzi ya maendeleo ya wananchi wilayani linahitaji katiba mpya ya majimbo kupewa uwezo wa kusimamia miradi ya mazingira, afya, miundombinu ya kuunganisha barabara za vijiji, elimu, kilimo, visima vya maji .
Ukisikia DED kaama jua mnoko ni mkuu wa wilaya na ukisikia mkuu wa wilaya kaama jua mnoko Ni mkuu wa mkoa.
Kwa mabadiliko hayo tutarajie hama hama ya wafanyakazi wengi kwani hao ma DED na DC wengi wanakuaga miungu watu
 
Hivi ndio vyeo nitavifuta within 4 hrs ya Urais wangu,Tanzania inahitaji service delivered sio utitiri wa cadre deployment, Tanzania mikoa 15 tu,wilaya 50 tu,wizara 15 tu(hakuna kabisa hawa deputy ministers),why singida bado kuna umasikini mkubwa?
 
Back
Top Bottom