Rais Samia alikuwa anamtisha nani hapa?

Rais Samia alikuwa anamtisha nani hapa?

Juzi hapa katika mjadala kuhusu kinachoendelea kati ya Israel na Palestina, kuna mtu alisema ni wazi Hitler alikuwa na sababu nzuri za kuwamaliza Wa-Israel. NIlimwambia hata Israel wafanye ukatili na unyama wa namna gani kwa Wapelestina, wewe unakuwa muovu zaidi ya Hitler kwa kuhalalisha maovu aliyofanya kwa Waisrael.

Sasa leo namsikiliza Raisi wangu mwenyewe akitamka kwa kinywa chake kuonyesha kwamba kile kilichofanywa kwa wanasiasa wa upinzani huko nyuma ilikuwa ni halali. Sikujua kuna siku ndani ya Tanzania nitakuja kusikia kauli kama hii ikihalalisha maumivu yaliyosababishwa na utawala uliopita! Tatizo ni nini hasa, kuutaka uraisi? Kuna nini huko Ikulu kinachofanya watu wajitoe ubinadamu kwa kiwango hiki?
 
Back
Top Bottom