11 Septemba 2021: Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alikutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Amina J. Mohammed, Ikulu Chamwino, Dodoma. Mazungumzo yalihusu ushirikiano wa UN na Tanzania, maendeleo endelevu, afya ya mama na mtoto, maji safi na salama, pamoja na kukabiliana na COVID-19.