Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi kama ifuatavyo:
Amemteua Dkt. Hashil Twaib Abdallah kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Abdallah alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara (Uwekezaji).
Amemteua Bw. Kaspar Kaspar Mmuya kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Mmuya alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu).
Uteuzi huu ni kuanzia tarehe 09 Desemba, 2022.
Amemteua Dkt. Hashil Twaib Abdallah kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Abdallah alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara (Uwekezaji).
Amemteua Bw. Kaspar Kaspar Mmuya kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi. Kabla ya uteuzi huo Bw. Mmuya alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu).
Uteuzi huu ni kuanzia tarehe 09 Desemba, 2022.