benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akizungumza katika kipindi cha Clouds360 kinachorushwa kupitia Clouds TV ameeleza kuwa Rais wa Tanzania; Dkt Samia Suluhu ameridhia kufanyika kwa mapitio ya baadhi ya tozo ili kupunguza gharama za Bando kama ambavyo watanzania wengi wamekuwa wakihimiza huku pia akieleza kuwa kuna mikakati zaidi ya kupunguza gharama za bando nchini ambayo itawekwa wazi siku za usoni.
“Mheshimiwa Rais amekubali tupitie baadhi ya tozo, ili kupunguza gharama za matumizi ya bando, na pia zipo hatua mbalimbali tunazichukua ambazo siku zijazo tutaweka wazi hatua hizo ambazo zitaleta unafuu katika gharama za matumizi ya intaneti.”
“Mheshimiwa Rais amekubali tupitie baadhi ya tozo, ili kupunguza gharama za matumizi ya bando, na pia zipo hatua mbalimbali tunazichukua ambazo siku zijazo tutaweka wazi hatua hizo ambazo zitaleta unafuu katika gharama za matumizi ya intaneti.”