Kama ulifanya kazi kwa jasho na ukachangia mifuko,lazima ulipwe,hatutaki dhulumati dhulumati
Mfumo uliyogundua kuwa huyu ana cheti feki ndio mfumo uliyomwajiri ndio mfumo uliotoa wanafunzi waliofeli na waliofaulu kupitia walimu hawa feki ambao walikatwa Kodi na mfumo huo na Makati ya NSSF yananyojenga mabarabara. Nani anauoeleka huo mfumo jela ambako unastahili kwa kuliingiza taifa hili kuwaajiribu walimu fekiKwa hili nadhani mama Samia ameliwazia kisiasa zaidi badala ya kiweledi.
Mtu aliyeghushi vyeti vya kitaaluma ni mhalifu na angetakiwa awe jela, wanasiasa wetu wana akili ndogo sana, daima wanawaza kutoa kauli na matamko yatayowafurahisha wapiga kura ili waendelee kubakia utawalani.
Mtu anayekalia nafasi ambayo ametumia njia za udanganyifu kuipata anazuia nafasi kwa wengine waliovuja jasho kwa ajili ya nafasi hiyo.
Naona hawa vyeti feki waliotumbuliwa wanataka kujiongeza ili walipwe Mama amesema darasa la saba tu wasiofoji vyetiHv alisema na wa vyeti feki si Wale wa darasa la Saba tu!!??
Tuliuliza wataje majina ya waliolipwa hata wawili tu , wakakimbia na hwajarudi hadi leoNa kuna taarifa kutoka PSSSF walisema walishaanza kuwalipa.
Hakika mkuu, mtu alidanganya halafu umlipe? Kuwaondoa kazini na kuwaacha huru inatosha sana kwani walistahili kufunguliwa mashtaka ya kughushi nyaraka na uhujumu uchumi.Yani mtu alifeli sa saba au form four, akaamua kuchukua cheti cha ndugu au rafiki yake ambaye either hakutaka kuendelea na shule au alishasoma mda, akaingia chuo na kumaliza shule huku anaitwa Najenjwa badala ya Naomi, leo tumuite MUHANGA? Mtu mwizi, kaghushi vyeti anaitwaje MUHANGA?
Sisi tuendelee tu kuwa taifa la hovyo.
Ajabu hii, halafu anakuja mtu anawaita wezi wahanga, hivi mkuu tunajielewa kweli?Hakika mkuu, mtu alidanganya halafu umlipe? Kuwaondoa kazini na kuwaacha huru inatosha sana kwani walistahili kufunguliwa mashtaka ya kughushi nyaraka na uhujumu uchumi.
hadaa za nape kwa mamaSasa ni dhahiri kwamba Wale walioondolewa kwenye ajira ya serikali kwa kile kilichoitwa vyeti vyao vya masomo ya sekondari ni feki , hawatolipwa chochote , hata ile michango yao tuliyoambiwa majuzi kwamba watalipwa ni hakika imeota mbawa .
Sitaki kurudia kulisema jambo hili kwa undani wake wote , maana linaeleweka na kila mtu .
Bali swali langu ni hili , Aliyewadanganya Wahanga hawa kwamba watalipwa michango yao , huku akijua kwamba SERIKALI HAINA PESA WALA HAINA NIA YA KUWALIPA ni nani ? Ni Mh Rais Dkt Samia ambaye alisikika akitamka hadharani kwamba walipwe kuanzia Novembba mosi , Ni Waziri wa Utumishi au ni CCM chama ambacho nguzo yake kuu ni Uongo ?
Lengo la kuwadanganya wahanga hawa walioridhika na dhuluma waliyofanyiwa na serikali ya awamu ya 5 na kuamua kumuachia Mungu lilikuwa nini hasa ?