JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Rais Putin amezungumza kwa njia ya simu na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron ambaye alikuwa akishawishi kumaliza vita hiyo baada ya Urusi kuivamia kijeshi Ukraine.
Nchi za Magharibi zimekuwa zikiisaidia Ukraine kwa vifaa vya kujilinda na kupigana na Urusi, jana Mei 2, 2022 Uingereza kutoa msaada wa vifaa vya dola 376m ikiwemo vifaa vya kielektroniki vya vita, mfumo wa rada, vifaa vya GPS na vifaa vya kuona usiku.
Maelfu ya watu wakiwemo raia wa kawaida wameuawa au kujeruhiwa katika vita hiyo tangu ilipoanza Februari 24, 2022.
Rais Macron ndiye aliyempigia simu Rais Putin na kusema yupo tayari kusaidia kumaliza mgogoro huo.
Source: BBC