Rais Nkurunzinza yupo Dar es salaam

Rais Nkurunzinza yupo Dar es salaam

jamaa yupo mbagala mitaa ya masakou
 
Nkurunzinza amepinduliwa jana wewe unataka Habari gani zaidi? Au unataka ngonjera kama za Al sahaf wa Sadam Hussein?

Kwani hujasikia kwamba kuna wanajeshi ambao bado ni watiifu kwa Pierre? Nchi ndio inaingia kwenye civil war kwa ajili ya makamanda wa Jeshi wasio na maamuzi ya busara kama Godefroid, kulikuwa na ugumu gani kusubiri kikao cha usuluhishi kikamilike kwanza, then maamuzi ya kuendelea ama kufanya coup d'etat ndio yangefuatia kutokana na maamuzi ya kikao hicho. Pia profile ya Godefroid inaonyesha wazi kwamba ana chuki dhidi ya Pierre hivyo ilikuwa rahisi kumpindua akiwa nje ya nchi. Bahati nzuri bado Nkurunzinza ana wanajeshi walio upande wake. Godefroid anaweza akaingiza Burundi kwenye civil war.
 
Kwann lakin viongozi wengi wa Africa wana uchu wa madaraka sasa yaliyomkuta Hugo bwa rais wa Burundi nikama aliyata mwenyewe sasa umekuwa mgogo Mkubwa mpaka kusababisha haya yanayotokea:
 
Nkurunzinza aliombwa na wananchi walio wengi wa Burundi aendelee kuwaongoza ili kulinda amani ya burundi ,hao wanaompinga ni genge tu la wahuni

Madaraka ni matamu sana! Abebe msalaba huo kwa kuachia madaraka, katiba inasema awamu mbili, sasa wananchi wanamtaka kivipi? Kama wanamtaka wameshindwa nini kumshauri Nkurunziza wabadili katiba yao na mambo yaendelee?

Amani ya Burundi inawezekana bila Nkurunziza ndugu! Ufisadi ndo unawafanya mnawapigia debe wahuni hasa huyu mpuuzi unayemshabikia ovyo kabisa!
 
Kwani we unajua kipikibaya alicho kifanya? wacha kurahisisha vitu jamaa hakuwa mbaya kwa wanaojua historia ya Burundi

Ebu tuondolee upoyoyo wako hapa jamvini,angalia watu wanavyo sherehekea mjini bujumbura,angalia wanajeshi wanavyo shangilia na vifaru mitaani bujumbura,wewe unataka kutwambia kuwa unaijua burundi kuliko wanajeshi waliokuwa wanalipwa mishahara na uongozi wa nkurunzinza?
 
Ndugu Emma lazima utambue kama umewai shuhudia mamako,babako na nduguzako wakiuliwa vibaya sidhani inaweza kuwa rahisi kusahau, na dalili kama hizo zikianza kujileta kamwe huwezi endelea kuwapo hapo

Ondoa utumbo wako hapa kabisa
 
Last edited by a moderator:
Ukimuua haitakuwa powa kamanda, anatakiwa abaki aone wenzake watakavyotawala kidemocrasia nafsi imsute......wakati huo akiwa kwenye ile mahakama yetu

Kule kwa kina van persie
 
Kwani we unajua kipikibaya alicho kifanya? wacha kurahisisha vitu jamaa hakuwa mbaya kwa wanaojua historia ya Burundi

Inawezekana katenda mazuri yote lakini huwezi pendwa na wote.Cha msingi ni kuheshimu demokrasia na katiba.Na kikubwa zaidi kuwa na hekima ya kutambua majira na nyakati
 
Huyu anatakiwa saa hizi awe mgeni wa Taylor wa Liberia pale The Hague Uholanzi akipigwa na baridi.Kumhifadhi dikteta ni kuinajisi demokrasia ya Watanzania,Bensouda mgeni wenu mtarajiwa yupo Dar njoo mumuchukue.
 
Hzo western media zinawadaganya,demokrasia ipi ndugu,burudi will never be at peace again mayb,ni bora wangeacha jamaa,agombee wamnyime,kura,ama akiiba ndo wapigane lakini huu ujinga walioufanya wa kupindua nchi.?trust me,mzigo ni wetu,niko ngara hapa jana tumetoka kusafisha sehemu watakayo fikia uko lukole,na tumekata miti kadhaa watengeneze mbao zitakazo saidia kujengea makazi yao.the burden is ours,hapo bado akina hussain rajab awajaamsha maskio.kwa haya mapinduzi kwa wanao ijua burudi tht country will never be at piece,hyo nkuruzinz ni mzaliwa wa hapa mpakani na tanzania yan mkoa wa kwanza ukiingia burudi ndo kwao panaitwa ngozi ,magari yake,masemi kibao alishavushia tz mda mrefu ana nyumba zaidi ya kumi hapa ngara ata wale majudge waliompitisha,walivyompitisha tu wakaamia ngozi,wakisubilia mda wowote kuvuka,maana walijua lazima kitanuka tu.
Ikumbukwe kwamba nkurunziza alitokea polin so sio hatari saana kwake kurudi polini,hata kma hatakuwa raisi yeye ila mtu anae mtaka yeye.

Wewe na warundi wenye nchi yao nani anajua hali ya amani iliyopo? Wananchi hawakutaki wewe unalazimisha tena kwa mitutu ya bunduki?
 
Hao wakimbizi wamekuja yeye bado ni rais, sasa hapa sijui kipi kinafanya useme kupinduliwa kwake ni mzigo kwetu.

Iwe iwavyo, burundi itaendelea kuwapo lakini pierre na cndd-fdd ni vitu vya kupita....kama ambavyo wewe na mimi ni wa kupita tu. Huyu rais alishalikoroga na kwa kuwafukuza watu waliomshauri kwa hekima alijitengenezea mazingira hatarishi hata kama angeshinda huu uchaguzi anaolazimisha kugombea.

Duniani hakuna mtu ambaye ni indispensable! Busara ya kawaida ilikuwa ni kufuata nyayo za akina Mwl nyerere ambaye katiba, chama pamoja na wananchi walikuwa wanataka aendelee kuwa rais lkn busara ikamtuma kuachia na wengine, ndivyo na Mandela alivyofanya.

cb

Ubarikiwe mkuu kwa point zako zenye busara na kueleweka
 
Sehemu kubwa ya wale wakimbizi ni wale waliowahi kuishi TZ,enzi zile za ukimbizi,sasa hivi wanatumia hayo machafuko km loop hole ya kurudi tena Tanzania.

Ukweli ni kuwa wananchi wa burundi hawakutaka aendelee kuwaongoza
 
Kichwa cha habari kimekosewa. Nkurunzinza sio rais tena. labda agombee urais wa TFF akishachukua uraia Tz maana sisi kwa kimbelembele cha kuhifadhi wauaji gama huyu hatujambo. Nkurunzinza au kurumbiza ni jobless kama jobless wengine Dar

Teeee,teeee,mkuu ni machinga kama wengine
 
Back
Top Bottom