Rais Mteule Barack H. Obama!

Carter na Clinton walisaidiaje dunia, Afrika, na Tanzania?

Watanzania hatumuungi mkono mgombea Urais wa Marekani kwa kutegemea kwamba ataisadia dunia, Afrika na Tanzania. Kuwa na Rais wa US ambaye hatatumia majeshi ya Marekani kuanzisha vita visivyokuwa na kichwa wala miguu ni sababu tosha kabisa ya kumuunga mkono Rais kama huyo maana vita hivyo vinaathiri dunia nzima kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta na athari nyingine mbali mbali.

Bush hizo pesa zake zote alizoahidi kuisadia Afrika ikiwemo Tanzania hazitatoka kwanza kutokana na hali ya uchumi wa US na pili Rais anayeingia kipaumbele chake kitakuwa siyo kuisaidia dunia, Afrika au Tanzania bali kuwasaidia Wamarekani kwanza ili kuujenga tena uchumi wa Marekani ambao umegubikwa na unemployment inayokuwa kwa kasi kubwa sana, budget deficit ya $500 billion and counting na deni la nje la $10.4 trillioni. Mpaka hapo uchumi wa Marekani utakapotengamaa nchi yeyote duniani isitegemee msaada toka US hata baadhi ya wananchi wameanza kuhoji umuhimu wa kuwapa Israel $3 billioni kwa mwaka wakati nchi yao iko katika hali mbaya ya kiuchumi.
 
Correction...
He is not pro abortion but pro-choice.

he is not pro choice for there is no higher choice than that of life; he is pro-abortion which is the purposeful termination of unborn child for convenience sake or any reason, or for no reason at all. That is not pro-choice that is pro-abortion. Pro-choice is just a mere euphemism for pro-abortion.
 
Sikubaliani na wewe pale unapomlinganisha Obama na Kikwete.

Wanalingana sana:

Wote ni populists
Wote wanatumia ahadi ya pepo na mambo mazuri bila kuwaambia watu ukweli wa hali halisi.
Wote wawili wamekampeni kwa kutumia ahadi tupu bila rekodi yoyote.
Wote wawili wamebebwa na vyombo vya habari to the expense of any other
Wote wawili wanatumia mvuto wa sura kama inspiration
Wote wawili wanaahidi kuwafanyia watu mengi zaidi kuliko yanayowezekana kibinadamu ikiwemo "lets go and change US, lets go and change the world - Obama" na "Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana" - Kikwete.
Wote wawili wanadaiwa kuwa na mahusiano na watu wenye mashaka; Obama na kina Ayers, Kikwete na kina Patel


Of course wanatofautiana pia; mmoja ni Mmarekani mwingine ni Mtanzania.
 
Uchambuzi wako Mwanakijiji sidhani kama ni sahihi.
Kwanza kama wewe unadhani sera za Bush ni nzuri...Then ni wazi sitoshangazwa unapomfagilia Mc Cain.

Jambo moja uelewe...Sera za Bush na Obama ni tofauti so as vs Mc Cain.

MKJJ huo utajiri unaodai utasambazwa ni upi huo? Mbona ndani ya miaka nane ya Bush walishushiwa kodi lakini bado makampuni yaka outsource biashara zao? Republican hawataweza kushusha kodi kiwango cha kupambana na lets say Mexico, China na hata India.

Uchaguzi huu Mc Cain naye anaweza kushinda, hilo la washabiki kufanya hayo si jambo la ajabu....Hata hivyo umenishangaza sana kwasababu hujatilia maanani historia ya Taifa hili...Kwao uchaguzi huu ni wa tofauti sana na wanautilia maanani sana na matokeo yataonyesha ni kwa jinsi gani wananchi wa marekani wamejihusisha na siasa kwa kiwango kisicho cha kawaida.

Watu wameshapiga kura na bado wanapiga kura kwa viwango vya kuvunja rekodi....Yani kila mtu ni simulizi. Ukizungumza na wamarekani hata ambao si weusi kama unavyodai na wao pia ni jambo la kihistoria kutokana na historia ya Taifa hili.

Kwamba imetokea kuwa ni mweusi hilo ni jambo la kihistoria hilo halina ubishi....Kwamba ana sera nzuri inategemea na kama wewe ni tajiri mkubwa mwenye uchu na asiyewajali masikini ambao uwezo wao wa kuspend ndio unausukuma uchumi.
Hao matajiri wanaotaka kuwekeza hapa marekani na kupata faida ya kuwatosha huku taifa likineemeka ndio matajiri wazuri ambao wako nyuma ya Obama...Matajiri ambao wanasema kama marekani iliweza kuutokomeza ugonjwa wa malaria hapa marekani ni kwanini isiwezekane Afrika?
Uchaguzi wa kesho ni wa kihistoria na yeyote kati ya Mc Cain na Obama anaweza kushinda...Lakini yeyote kati yao atakayechaguliwa atafanya tofauti kabisa na atakalofanya mpinzani wake kama angechaguliwa.

usiamini hayo yote; akiingia Obama kesho na akiapishwa tu miezi michache inatokea shambalizi la kighaidi, unafikiri Obama atasita kutuma majeshi ya Marekani kwenye taifa lolote lile kuzipiga? don't believe the hype hawa ni wamoja. Kumbuka Carter alipojifanya yeye tofauti na kucheza cheza na Wairani guess what happened to him...

Ndio maana Clinton alikuwa anaishia kupiga vijibomu hapa na pale..
 
Histolia inaonyesha wazee ndio wanaongoza kwa kuiba kula....wengi wao hawapendi kabisa kukosa madalaka...sijui ni africa tu au hata uko inawezekana huyu Mc Cain akaiba kula...very very doubt na huyu mzee...
 
Wanalingana sana:

Wote ni populists
Wote wanatumia ahadi ya pepo na mambo mazuri bila kuwaambia watu ukweli wa hali halisi.
Wote wawili wamekampeni kwa kutumia ahadi tupu bila rekodi yoyote.
Wote wawili wamebebwa na vyombo vya habari to the expense of any other
Wote wawili wanatumia mvuto wa sura kama inspiration
Wote wawili wanaahidi kuwafanyia watu mengi zaidi kuliko yanayowezekana kibinadamu ikiwemo "lets go and change US, lets go and change the world - Obama" na "Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana" - Kikwete.
Wote wawili wanadaiwa kuwa na mahusiano na watu wenye mashaka; Obama na kina Ayers, Kikwete na kina Patel


Of course wanatofautiana pia; mmoja ni Mmarekani mwingine ni Mtanzania.
Naomba usubiri 3 years ndio useme hivyoo. Kuna mambo kayafanya kwenye short career yake, tofauti na Kikwete.
 
Wanalingana sana:

Wote ni populists
Wote wanatumia ahadi ya pepo na mambo mazuri bila kuwaambia watu ukweli wa hali halisi.
Wote wawili wamekampeni kwa kutumia ahadi tupu bila rekodi yoyote.
Wote wawili wamebebwa na vyombo vya habari to the expense of any other
Wote wawili wanatumia mvuto wa sura kama inspiration
Wote wawili wanaahidi kuwafanyia watu mengi zaidi kuliko yanayowezekana kibinadamu ikiwemo "lets go and change US, lets go and change the world - Obama" na "Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana" - Kikwete.
Wote wawili wanadaiwa kuwa na mahusiano na watu wenye mashaka; Obama na kina Ayers, Kikwete na kina Patel


Of course wanatofautiana pia; mmoja ni Mmarekani mwingine ni Mtanzania.


Mkuu mkjj nadahani hapa umepotosha kidogo

Well

1. Populist charge - JK anajulikana na amestruggle sana kuwa popular -kwa hili hamna ubishi na hata aides wake na washauri wa karibu ni wale waanaomsifia whilst BHO popularity is from him being one of the very few american ever hold the senator position, The way he ran one of the most successful primary campaiign in US history. The way he has been running this gen. election campaign has bn outstanding. Aides wake ni wataalamu na wenye record ya perfomance. Just think of Ax.

2. Ahadi za pepo charge - JK was and still purely Vague, whilst BHO the plans and promises are well explained in his website (In this case manifesto). JK hata ile ilani ya CCM haileweki ni namna gani watatizmiza ahadi zao. Na kuhusu rekodi mkuu tafadhali BHO alikuwa community organiser for some years... Remember those piles of asbestos waste in Alt. South side? Alikuwa part time law proffessor Chicago uni. with accomplishments well expalined in his website. senetarial record is also well explained in his website and also the US senate website.

3. Media charge - Whilst JK na maswahiba wae walikuwa wanawahonga waandishi ili JKasifiwe na kupambwa BHO amewainspire liberal media to an extent wanajikuta wakimuandika vzuri muda mwingi. Of late ofcourse election ya Marekani feza inaplay part kubwa sana therefore mwenye hela mingi atakuwa anapost ads nyingi pia hii ni regardless you are republican, democrat, Mcain, BHO, Romney or Hillary.

4. Mvuto wa sura charge: Mkuu kwa JK hii ni kweli kabisa lakini kwa BHO ni combination ya mvuto na mambo mengi especially speeches, message and deliverance. Historia pia ya BHO ni too inspiring. Na eneo hili ndio viongozi wetu wengi watZ ratings are so low. Mkjj don't tell me kwamba the masses wanaoattend rally za BHO possibly wameuwa inspired na mvuto wa sura?????

5. Change charge - Mkuu maisha bora kwa kila mtanzania hii ilikuwa ni ndoto amabayo inawezekana kama you have a right leardeship to bring about. Change as for BHO is imminent. Imagine Closing the Guantanamo. Normalizing relationship wth Cuba, Venezuela and possibly Iran. Ending the war in Iraq and so many more that even the Bush administration as slowly leaning to admittance.

6. Controversial relationships charge - Whilst BHO and controversial Ayers were together in the Chicago board of education, and contr. Wright was his pastor I fail to understand how JK is in the tank of Jeetu, RA, Vhlatini etc.

nawakilisha..........
 
Watanzania hatumuungi mkono mgombea Urais wa Marekani kwa kutegemea kwamba ataisadia dunia, Afrika na Tanzania. Kuwa na Rais wa US ambaye hatatumia majeshi ya Marekani kuanzisha vita visivyokuwa na kichwa wala miguu ni sababu tosha kabisa ya kumuunga mkono Rais kama huyo maana vita hivyo vinaathiri dunia nzima kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta na athari nyingine mbali mbali.

Bush hizo pesa zake zote alizoahidi kuisadia Afrika ikiwemo Tanzania hazitatoka kwanza kutokana na hali ya uchumi wa US na pili Rais anayeingia kipaumbele chake kitakuwa siyo kuisaidia dunia, Afrika au Tanzania bali kuwasaidia Wamarekani kwanza ili kuujenga tena uchumi wa Marekani ambao umegubikwa na unemployment inayokuwa kwa kasi kubwa sana, budget deficit ya $500 billion and counting na deni la nje la $10.4 trillioni. Mpaka hapo uchumi wa Marekani utakapotengamaa nchi yeyote duniani isitegemee msaada toka US hata baadhi ya wananchi wameanza kuhoji umuhimu wa kuwapa Israel $3 billioni kwa mwaka wakati nchi yao iko katika hali mbaya ya kiuchumi.

BUBU ATAKA KUSEMA uko sahihi kwa asilimia 100 kwa watu ambao hawaongozwi na ushabiki tu.

Sera ya Obama kuongeza kodi haitafanikiwa sana Marekani sababu kampuni nyingi zina-outsource na kuhamishia uzalishaji wao kwa njia za Contract Manufacturing n.k kuhamishia mataifa mengine ambako gharama za uzalishaji ziko chini na viwango vya kodi viko chini kuliko Marekani.Hivyo tatizo la ukosefu wa kazi litazidi kuwa kubwa zaidi Marekani kwa makampuni kukimbia ongezeko la kodi kwenda nchi zingine na hilo litasababisha vibiashara vingi vidogo na vikampuni vidogo na vya kati na chini kufa kwa wingi na sekta ya nyumba kuzidi kuporomoka na watu wengi wa chini anaotaka kuwasaidia kuwa katika shida zaidi.

Hata masoko yao ya Bidhaa makampuni makubwa concentration yao haiko Marekani tena wanalenga mataifa ya nje ya Marekani kwa soko la bidhaa zao hivyo kutegemea kuwa ndoto hewa zake za kupata Kodi kubwa zitafanikiwa ili awasaidie walalahoi wa Marekani hazitatimia sana.

Kwa upande wa sera ya nje naona sera yake ya kuondoa majeshi ya Marekani ni mbaya itazalisha vita kubwa za ndani (Internal wars) ambazo zitasambaratisha kabisa nchi za Iraq,Afghanstan na Pakistan na Georgia na Kuwaiti ambako kutasababisha bei za mafuta kupanda juu mno na kuleta mtafaruku mkubwa wa kiuchumi duniani ambao historia ya dunia haijapata kuuona ambao utazalisha maskini wengi mno duniani.

Sera za Utawala wa Obama kama akishinda hazitakuwa na maslahi kwa Marekani weusi waliojaa matumaini hewa kutokana na hasira za kuwa third class citizens wa daraja la chini Marekani. Hali za Marekani weusi ni mbaya sasa hivi lakini zitakuwa mbaya zaidi Obama akishika serikali sababu sera zake hazitazaa matunda.
 
Hatuwezi kuwalaamu wala kuwashangaa waafrika hasa tukiangalia historia ya watu weusi huko marekani. Obama anabeba tawira nzito sana na kuwafungulia milango wengi wataokuja badae, amefutilia mbali mstari uliokuwa umechorwa kwa misingi ya rangi katika historia ya marekani pengine ndio ameweza kuuishi dhana ya fursa sawa kwa wote; kwa namna yoyote ile hii ni haki ya asili ya waafrika kuunga mkono mweusi mwenzao baada ya mlolongo wa historia chungu ya weusi marekani, huu ni mgeuko wa aina yake katika historia ya dunia. Ziada ya hayo Obama amekwenda hatua moja mbele, ubinifu katika kampeni hasa mfumo wake wa kuchangisha hela za kampeni na wakati wote ameonyesha uelewa wa hali ya juu wa kila anachokisema na kutetea.

Ni makosa makubwa yenye msukomo wa nia mbaya kumfaninisha JK na Obama! Jk amejipambanua kama mtu aliejijengea historia ya kipekee, ni kiongozi asijiweza na alijionyesha hivyo tangu wakati wa kampeni hakuweza kufafanua kauli mbiu yake ya ari, nguvu na kasi mpya ina maana gani na aliogopa kuvilinganisha na vitu vinavyoshikika! Jk kwa kiasi kikubwa alichukua nchi kwa kwa majungu na kupewa sifa ambazo hana sambambamba na kuwachafua wagombea wenzake!Leo tunamshuhudia kiongozi aliegeuka kuwa mziko mgubwa mno kwa nchi yake na pengine kikwazo kikuu cha ustawi wa taifa!

Halikadhalika kuwafananisha Nyerere na Obama ni vigumu kwani wamepita katika historia, mazingira na changamoto tofauti! Na katika medani ya kuongoza nchi uwezo wa Obama bado haujajaribiwa wala kuthibitishwa kwa hiyo huu unaweza kuwa mjadala mbichi mabapo wakati wake bado haujawadia!

Mwanakijiji sijui kwa msikumo upi umeamua kumuotea vibaya Obama katika utawala wake iwapo atashinda na umeamua kuutabiria vema utabiri wa Mccain kama atashinda(japo ana fusra ndogo). Kwa kufanya hivyo unatuaminisha kuwa msukumo wako ni wa kisiasa, jambo ambalo linakubalika na kuvumilika katika demokrasia pana,ambacho ulistahili kufanya ni kujenga hoja kwanini ni Mccain ni zaidi ya obama kwa mtazamo wa mambo wanayosimamia na rekodi zako, umekosea kusukuma hoja yako kwa kutumia rangi na kumfafananisha na JK! Umesambaratusha lengo lako na kuupasua mjadala wenyewe hivyo umekuwa umetanuka mno toka marekani mpaka Tanganyika ya mwaka 196! Karabati hoja zako vizuri ili mjadala uwe afya!​
 
Tunachoshangilia ni ushindi kwa ubinadamu. Miongo minne nyuma wakati Obama akiwa mtoto mdogo, si tu kuwa Obama asingegombea huo urais, kuna majimbo ambayo asingeweza hata kupiga kura. Kuna kijakazi mmoja nilimuona kwenye TV akisema kuwa hatamchagua Obama kwa kuwa si mkristu. Kazi ya kuibadili dunia haiwezi kufanywa na Obama au mtu yeyote peke yake. Kazi hiyo ni ya wakazi wote wa dunia na kazi hiyo itakamilika pale wenye mawazo sawa na huyu kikongwe watakapotambua kuwa mtu hapimwi kwa ukristo wake wala kwa uislamu wake, weupe wake au weusi wake. Tunashangilia kwa kuwa kwa mbali ile nchi ya ahadi kama ilivyobainishwa na Luthe King jr tunaweza kuiona. Tutaifikia lini, hilo ni swala jingine.
 
Kuna mamilioni ya watu katika bara letu ambalo wanasubiri kwa hamu ushindi unaotarajiwa wa Obama kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi huko Marekani. Kuna tafrija na sherehe zilizoandaliiwa sehemu mbalimbali ambapo watu weusi watasimama kufurahia ushindi wa Obama.

Sitoshangaa wengi wanaosubiri huo ushindi wa Obama wanafanya hivyo si kwa sababu wanakubaliana na sera zake zote (kuongeza kodi, kugawanya utajiri n.k) au misimamo yake ya kijamii (kuunga mkono utoaji mimba au haki za mashoga n.k) bali wanafanya hivyo kwa sababu Obama ni "mweusi mwenzetu".
Hili hata hivyo linanikumbusha jinsi watu walivyomshabikia Kikwete mwaka 2005 licha ya kuwa hakuwa na rekodi yeyote, hakuwa tayari kufanya midahalo na wagombea wenzake na alikuwa na maneno matamu ya "change" yaliyotumiwa kwa mbiu ya "ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya".

Wapo watu wale wale ambao leo wanamgeuka Kikwete ndio leo wanakumbatia kwa haraka maneno ya "change" na ya kuwa "Yes we can". Lakini nyuma ya ushabiki huu Watanzania na watu wa mataifa mengi ya dunia wanachoshabikia kule Marekani kwa kweli ni Rangi; kwamba hatimaye Taifa lenye watu wengi weupe likaongozwa na mtu mweusi!

hapa najikumbusha maneno ya Mwalimu "Sisi bwana hatutukuzi rangi, tunatukuza mtu bwana"!

Yawezekana ulimwengu ukakosea katika ushabiki wake wa Obama kama Watanzania asilimia 80 ya wapiga kura walivyokosea walipomshabikia Kikwete. Kweli Obama ataweza kutimiza ahadi yake ya "kuibadili Marekani, na kuibadili dunia"?

Yawezekana kiongozi ambaye watanzania na nchi za ulimwengu wa tatu zilipaswa kumshabikia ni McCain na siyo Obama kama wangeamua tu kuweka rangi pembeni? Well, masaa 24 yajayo will give us a clue.

Hapa naona umepotoka kidogo mkuu, katika kura za maoni yaliyofanyika katika nchi mbali mbali duniani, zikiwepo Holand, Norway, Germany, Sweden, China n.k. Obama ameibuka kidedea kwa asilimia nyingi sana. je na hawa vile vile wanampenda kwa sababu ni 'mweusi mwenzetu'? na kwanini iwe tofauti kwa mwafrika kumpenda Obama? Swali gumu zaidi ni kwamba, kwanini Wamerekani weupe wawe tayari kumchagua Obama hasa ukizingatia historia ya wamarekani na maswala ya ubaguzi wa rangi? hata majimbo kama Montana, North Dakota, Virginia, North Carolina Obama anaongoza!! hata hawa ni kweli kwamba wamevutiwa tu na sura ya Obama? I don't think so! tufikirie maswala ya uchumi, vita na sera mbovu za Bush ndio tutapata jibu kwa nini Obama ni maarufu, na kamwe usimlinganishe na kilaza wetu JK! JK anaweza kutoa hoja kwenye midahalo kama Obama alivyofanya? unalo jibu mwenyewe.
 
...ilikuwa haina hata haja ya kumjibu!! Obama ni baaaaaab'kubwa kuliko Nyerere mara million!!!

Kuna watu wengi wanaumwa lakini kwa kufananisha huku nadhani wewe jamaa unahitaji msaada mkubwa. Sidhani kama ni haki nasawa kumfananisha Nyerere na Obama...

Obama yupo juu sana na ana mvuto kisiasa na kijamii lakini huwezi mfananisha na J.K. Nyerere...Nyerere ni level nyengine kabidsa ndugu Jina Langu.
 
After months of campaigning, hours of election speeches and debates, and hundreds of opinion polls tracking the ebb and flow of the 2008 US presidential election, the time of reckoning is here-WHAT IS KIKWETE'S OPINION ON US ELECTION, WHO DOES HE SUPPORT AND WHY?.

Kuna yeyote anayejua, kama ndivyo tueleze.
 
Pia utujalie na ule uwanja wetu pale Kisumu upanuliwe haraka ili Air force one iweze kutua kwa urahisi. Amen
 
kama watu wangetaka kumlinganisha Obama na Nyerere wangefanya hivyo mwaka 1961!

Kaka MNJJ nashukuru kwa hili, ujumbe umefika na umeeleweka kiasi cha kutosha... LOL!!!

Hivi 1961 kwa Marekani jaribio la kugombea Urais kwa mtu mwenye background kama ya BO kungesababisha nini? Historia yangu kama ina ukungu vile. Lol!!!
 
Nadhani hii thread imeanzishwa ili tukune vichwa kufikiri wakati tunasubiri matokeo ya uchaguzi wa kihistoria huko Marekani. Vinginevyo hoja zilizomo ni nyepesi mno, na sitajaribu kuzijibu.

Hata hivyo nisemu kuwa SIASA inategema msingi mmoja mkuu, nao ni kuwambia watu kile kitu wanachotaka kusikia kwa wakati huo; na siyo kile unachotaka kusema wewe (tell the people what they want to hear and not what you want to say!). Mwanasiasa akimudu hilo anapiga bao. Na hili linategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa kusoma nyakati. Sasa wachangiaji mnaweza kuamua wenyewe nani ameweza kuzisoma nyakati vizuri kati ya Obama na McCain.

Lakini kubwa ni kuwa kila binadamu ameumbwa na hisia. Hizo hisia ukizigusa vizuri basi unampeleka kwenye dunia ya ajabu, dunia ya matumaini, dunia ya kila kitu. Na tulio wengi tunatamani kusikia neno moja tu, MABADILIKO (CHANGES). Iwe ni mabadiloko hasi au chanya, hilo tutalishughulikia baadaye. Kwa hali ya dunia ilivyo tunataka mabadiliko. Yeyote anayeonesha kuwa kwa kiasi kikubwa anaweza kuteletea mabadiliko basi tutamshabikia; awe mweupe, mweusi au kijani!!
 
........bali wanafanya hivyo kwa sababu Obama ni "mweusi mwenzetu".

Obama akiwa mweusi wewe utakuwa nani?

Obama is as white as any kid in america.

From a white a mom and a mzungu upbringing, calling him mweusi is like his mom and his up bringing dont exist.

Trust me there is a big reason behind this....thing BIG.

Miafrika 100% ndivyo tulivyo hata weupe 50% tunavutia kwetu.
 
Back
Top Bottom