Opportunity Cost
JF-Expert Member
- Dec 10, 2020
- 9,035
- 6,907
Waje Rukwa tuu hapa maeneo yapo ya kutosha.Mkuu kaongea vizuri kama Mbeya hawana ardhi ya kutosha ekari 500 basi hilo tawi la UDSM litaenda kuanzishwa mikoa mingine kama Rukwa, Katavi na kwingineko kwenye mapori meengii tuu yasiyo na mwenyewe.
Ipo ya kutosha,Chuo cha kilimo na Tanganyika packers na TBC Wana maeneo makubwa Sana.Unalima.maharage mjini Ili iwe nini?Hiyo Ardhi Mbeya hawezi kuipata maana wilaya ambazo zina Ardhi kidogo ya akiba ni Chunya na Mbarali lakini 500-1000 too much hata UDSM main campus hawana eneo la hivyo
Acha ufala na ujinga wa kujitungia vitu vya kufikirika ambavyo Mbeya haifanyi..Waende wakajenge Dodoma huko ndo Kuna miekari ,mbeya ni jiji la viwanda na ni mkoa wa kilimo,unalisha takribani 75% ya mikoa yote tz,tuwape miekari 1000,halafu tulime wapi ,kwanza hiyo UDSM kwetu si kipaumbele labda wangekuwa SUA at least tungeweza kufikilia ,UDSM ni chuo Cha mashalobaro na sistaduuz ,ekari 50 hamtaki Basi,nendeni kwingine,
Chochote unacho wewe kichwani mwakoHamnazo hao, sasa JK unaona ana chochote kichwani
Linazidi hizo ekari,hayo maeneo ni makubwa Sana.Linafika heka 500-1000?
Ni zaidi ya ekari 3000Linafika heka 500-1000?
Si kwajili yake Bali ulimwengu na watotozenu wakiwemo ndani ya ulimwengu huuNa yeye ameanza kuvimba
Kichwa habari utafikiri ameomba binafsi kumbe kwa ajili yachuo muemnaandika ilimuelewekeRais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amekataa kupokea ekari 50 ambazo Serikali ya Mkoa wa Mbeya imezitoa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Chuo Kikuu cha Dar es Saalam kampasi ya Mbeya na kutaka wapewe eneo lenye ukubwa wa ekari 500 au 1,000.
Kikwete amesema kama mkoa huo hautawapa eneo wanalolihitaji watahamishia chuo hicho katika mkoa mwingine ambao utakuwa tayari kuwapa ardhi yenye ukubwa wanaouhitaji.
Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi, Novemba 27,2021 wakati wa mahafali ya 51 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi kampasi ya Mbeya yaliyofanyika jijini hapa.
Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa chuo hicho kina hadhi kubwa hivyo wanahitaji ekari 500 hadi 1000 kwa ajili ya kujenga hosteli, makazi ya wahadhiri, wafanyakazi na hospitali.
Kauli hiyo ameitoa baada ya hotuba ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Mwanaidi Mtanda kusema kuwa ukosefu wa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili licha ya kuwasilisha maombi yao kwa Serikali ya mkoa tangu mwaka jana.
"Ingawa simuoni hapa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (Juma Homera) lakini naamini viongozi wa Mkoa watamfikishia ujumbe, tunaomba kiwanja tujenge chuo cha kisasa na hili lipewe kipaumbele" amesema Mwanaidi.
Mara baada ya hotuba hiyo, Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa hazikidhi mahitaji yao
"Hii siyo sekondari kupewa ekari 50, tunataka eneo kubwa la ekari 500 hadi 1000 tenga hata kule Forest, mkishindwa tunahamia mkoa mwingine utakaoweza kutoa eneo kubwa, huu ni ujumbe kwa nyie viongozi" amesema Kikwete.
Kosa ni nini hapa????Badala ya kujenga UDSM kampasi ya Mbeya kwa nini kisijengwe chuo kikuu cha Mbeya?
Kwa nini Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika mkoa wa Mbeya?
SUA ni kata iliyochangamka siyo mchezo
Aisee, bado najiuliza ilikuajekuaje hadi wakamiliki eneo lote lile!!SUA ni kata iliyochangamka siyo mchezo
mbeya kuna dhahabu labda wanataka kuimarisha ulinzi.Lakini niulize swali? hicho chuo kinataka kulima au kufundisha wanafunzi? hivi kweli unahitaji hekali 500 za chuo kwa ajiri ya nini? Pale Dar sidhani hata kama zinafika hizo hekali 1000 na zimewashinda wameanza wamezijengea mlimani city & more are coming.
Mawazo mengine ktk nchi za kiafrika ni ya kuchekesha sana,suala la kutaka eneo si muhimu sana kama ilivyo muhimu kutathmin elimu inayotolewa pale USDM.Tutajidai kwa kuwa na vyuo vzr lkn tujue vyuo hv vinavyotengeneza viongozi ombaomba na watembeza bakuli kila kukicha kiongozi anapanga akaombe fedha nchi huko ulaya,hv vyuo vyetu lzm tukubali kwamba vimefeli maana elimu inayotolewa haijakidhi mahitaji ya taifa ndio maana tuna wasomi ambao si creative hata kidogo,hivyo tusiangaike kusumbua watanzania huko Mbeya eti ili kutafuta eneo la kujenga tawi la UDSM ni UPUUZI tu.
Hiyo UDSM yenyewe haina ekari 1000 lakini hata hizo 100 tu wameshindwa kuzitumia.Safi sana Kikwete. UDSM inapewaje ekari 50 imekuwa sekondari hiyo?
Havimbi bali atakuwa ameshauriwa na chuo chenyewe. Kuna kitu watakuwa chuo hawajaridhika wamekiona hakiendi sawa, ikabidi wapeleke hoja zao kwa mkuu wa chuo.Na yeye ameanza kuvimba