Rais Mstaafu Jakaya Kikwete agomea eneo la ekari 50, ataka ekari 500

Mkuu kaongea vizuri kama Mbeya hawana ardhi ya kutosha ekari 500 basi hilo tawi la UDSM litaenda kuanzishwa mikoa mingine kama Rukwa, Katavi na kwingineko kwenye mapori meengii tuu yasiyo na mwenyewe.
Waje Rukwa tuu hapa maeneo yapo ya kutosha.
 
Hiyo Ardhi Mbeya hawezi kuipata maana wilaya ambazo zina Ardhi kidogo ya akiba ni Chunya na Mbarali lakini 500-1000 too much hata UDSM main campus hawana eneo la hivyo
Ipo ya kutosha,Chuo cha kilimo na Tanganyika packers na TBC Wana maeneo makubwa Sana.Unalima.maharage mjini Ili iwe nini?

Chuo cha kilimo uyole kihame pale mjini liende mkoa kama Rukwa ndiko wapewe maeneo ya kufanyia utafiti sio mjini .
 
Waende wakajenge Dodoma huko ndo Kuna miekari ,mbeya ni jiji la viwanda na ni mkoa wa kilimo,unalisha takribani 75% ya mikoa yote tz,tuwape miekari 1000,halafu tulime wapi ,kwanza hiyo UDSM kwetu si kipaumbele labda wangekuwa SUA at least tungeweza kufikilia ,UDSM ni chuo Cha mashalobaro na sistaduuz ,ekari 50 hamtaki Basi,nendeni kwingine,
Acha ufala na ujinga wa kujitungia vitu vya kufikirika ambavyo Mbeya haifanyi..
 
Mawazo mengine ktk nchi za kiafrika ni ya kuchekesha sana,suala la kutaka eneo si muhimu sana kama ilivyo muhimu kutathmin elimu inayotolewa pale USDM.Tutajidai kwa kuwa na vyuo vzr lkn tujue vyuo hv vinavyotengeneza viongozi ombaomba na watembeza bakuli kila kukicha kiongozi anapanga akaombe fedha nchi huko ulaya,hv vyuo vyetu lzm tukubali kwamba vimefeli maana elimu inayotolewa haijakidhi mahitaji ya taifa ndio maana tuna wasomi ambao si creative hata kidogo,hivyo tusiangaike kusumbua watanzania huko Mbeya eti ili kutafuta eneo la kujenga tawi la UDSM ni UPUUZI tu.
 
Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amekataa kupokea ekari 50 ambazo Serikali ya Mkoa wa Mbeya imezitoa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Chuo Kikuu cha Dar es Saalam kampasi ya Mbeya na kutaka wapewe eneo lenye ukubwa wa ekari 500 au 1,000.

Kikwete amesema kama mkoa huo hautawapa eneo wanalolihitaji watahamishia chuo hicho katika mkoa mwingine ambao utakuwa tayari kuwapa ardhi yenye ukubwa wanaouhitaji.

Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi, Novemba 27,2021 wakati wa mahafali ya 51 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi kampasi ya Mbeya yaliyofanyika jijini hapa.

Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa chuo hicho kina hadhi kubwa hivyo wanahitaji ekari 500 hadi 1000 kwa ajili ya kujenga hosteli, makazi ya wahadhiri, wafanyakazi na hospitali.

Kauli hiyo ameitoa baada ya hotuba ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Mwanaidi Mtanda kusema kuwa ukosefu wa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili licha ya kuwasilisha maombi yao kwa Serikali ya mkoa tangu mwaka jana.

"Ingawa simuoni hapa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (Juma Homera) lakini naamini viongozi wa Mkoa watamfikishia ujumbe, tunaomba kiwanja tujenge chuo cha kisasa na hili lipewe kipaumbele" amesema Mwanaidi.

Mara baada ya hotuba hiyo, Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa hazikidhi mahitaji yao

"Hii siyo sekondari kupewa ekari 50, tunataka eneo kubwa la ekari 500 hadi 1000 tenga hata kule Forest, mkishindwa tunahamia mkoa mwingine utakaoweza kutoa eneo kubwa, huu ni ujumbe kwa nyie viongozi" amesema Kikwete.
Kichwa habari utafikiri ameomba binafsi kumbe kwa ajili yachuo muemnaandika ilimueleweke
 
Hizo heka 500 wanazo hapa dar, au ni kutafuta kiki tu.....yaani mnyanga'nye wananchi maeneo yao ili mjenge chuo kikuu uchwara, aka. jalalani........basi nendeni katafute huko kwengine mlipoziweka. Kuna mapori tabora huko hayakaliwi na watu zaidi ya mbung'o kajengeni huko, ebooo!
 
Lakini niulize swali? hicho chuo kinataka kulima au kufundisha wanafunzi? hivi kweli unahitaji hekali 500 za chuo kwa ajiri ya nini? Pale Dar sidhani hata kama zinafika hizo hekali 1000 na zimewashinda wameanza wamezijengea mlimani city & more are coming.
mbeya kuna dhahabu labda wanataka kuimarisha ulinzi.
[/QUOTE]
Dhahabu si ni chunya kule, kikwete anazungumzia mpaka maeneo ya Forest, au nishaisahau Mbeya mara hii. Hayo maeneo ya Forest kuna chuo cha mzumbe kimebanana kwelikweli na makazi ya watu, hiyo forest anayozungumzia Kikwete ni ipi? 1000 hectas?
 
Mawazo mengine ktk nchi za kiafrika ni ya kuchekesha sana,suala la kutaka eneo si muhimu sana kama ilivyo muhimu kutathmin elimu inayotolewa pale USDM.Tutajidai kwa kuwa na vyuo vzr lkn tujue vyuo hv vinavyotengeneza viongozi ombaomba na watembeza bakuli kila kukicha kiongozi anapanga akaombe fedha nchi huko ulaya,hv vyuo vyetu lzm tukubali kwamba vimefeli maana elimu inayotolewa haijakidhi mahitaji ya taifa ndio maana tuna wasomi ambao si creative hata kidogo,hivyo tusiangaike kusumbua watanzania huko Mbeya eti ili kutafuta eneo la kujenga tawi la UDSM ni UPUUZI tu.
Mkuu Hiki ulichoandika Indio UPUUZI sasa. Hivi una taarifa kwamba tuna upungufu sana wa wahudumu wa Afya nchi hii?

FYI Kitivo cha Tiba UDSM sio kwamba ndio kinaanza , program ilianzi tangu mwaka 2015/2016 pale pale UDSM main campus. Yule bwana aliwahi kuishi magogoni kwa sasa amelala huko chato alipinga uwepo wa kozi ya Medicine UDSM kwa kuna tayari kuna hiyo program Muhimbili. Ikabidi kitivo kihamishiwe Mbeya, Kwanini? Kwa kuwa ili uweze kutoa mafunzo bora kwa madaktari unahitaji MADAKTARI BINGWA kwenye fani mbalimbali kuweza kuwafundisha hawa wanafunzi. Hawa unaweza kuwapata Hospitali ya Rufaa Kanda Mbeya. Its as SIMPLE as that hakuna siasa hapa. Mwaka Jana 2020 wamehitimu zaidi ya madaktari 100 watakua wamekamilisha Internship now tayari kukuhudumia huko kwenu.

Sasa Kwa maono ya UDMS sio kuwa na Lecture halls tu, wanahitaji kuwa na Hospitali Kubwa ya Kisasa kuweza kutoa huduma na kutoa mafunzo ndio maana wanahitaji eneo kubwa la kuweka hizo miundombinu. Nenda Katembee Mloganzila Hospital ndio utaelewa kwanini JK anahitaji eka Hizo kule Mbeya. Hiyo Hospitali ya Mloganzila ni mpango/mradi wa chuo cha Muhimbili Kiliamua kuwa na Hospitali Yake kutoa huduma na kufundishia. Again, yule mwanasiasa wa Chato akawaambia Hiyo Hospitali iwe chini ya Management ya Muhimbili National Hospital. Ikabadilishwa jina toka MUHAS Medical Academic Centre to Muhimbili National Hospital-Mloganzila. Unaweza kuona MUHAS wako Upanga lakini ilibidi watafute eneo nje ya Mji karibu kilomita 30 kujenga Hospitali ya kutoa mafunzo. Ukiniuliza sababu nitakwambia "Poor planning from the very beginning".​
 
Na yeye ameanza kuvimba
Havimbi bali atakuwa ameshauriwa na chuo chenyewe. Kuna kitu watakuwa chuo hawajaridhika wamekiona hakiendi sawa, ikabidi wapeleke hoja zao kwa mkuu wa chuo.
Tuache siasa kwenye elimu, hasa hizi muhimu zinazohusu uhai wa binadamu moja kwa moja. Mimi nilitarajia wangekua wamepewa eneo lenye ukubwa ambao wao wenyewe chuo wangeamua kulikataa na kurudisha sehemu yake
 
50 Reactions
Reply
Back
Top Bottom