Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

Ni kweli kabisa kuna mengi ambayo yalikuwa red flags kuhusu huyu kutokuwa na sifa za kuongoza nchi ikiwemo kushiriki ukwapuzi wa nyumba za Serikali, ununuzi wa boti lililooza kwa shilingi bilioni 8 na lililopigilia msumari huyu kutokuwa na sifa za kuongoza nchi ni pale mkewe alipogoma kumfanyia kampeni. Yote haya wakaamua kuyadharau na matokeo yake ndiyo hayo ya nchi kuongozwa katika style ya one man show ambapo madhara makubwa sana yanaweza kuikumba nchi yetu ikiwemo la uchumi kutetereka kwa kasi kubwa.

Tabia haina dawa alishasema kauli za ajabu ajabu toka enzi
 
Na kwanza tuliosema huyu ni One term president inawezekana hata asikamilishe One Term

Ofcourse sio lazima akae madarakani miaka 5.
Mkuu Benjamin huogopi kuitwa na policcm kuhojiwa?lol
Hawakawii kukuita mchochezi watch out bro!
 
I agree with you. Hata wafanyakazi wengi wa umma hawana furaha na staili hii ya Magu. Na hili la kuhamia Idodomya fasta ndio usiseme.
Mzee hafikirii kama kuna watu wameshawekeza maisha yao Dar sasa hafla anataka wahamie dodoma. Sijui wangapi watawacha kazi na wangapi watakwenda dodoma
 
Naongelea uwanja wote, ambao rais anaruhusiwa kucheza! Magufuli ana mapungufu lakini Kikwete alikuwa ni zaidi. BTW wanaopiga kelele Tanzania sasa hivi kumlaumu Magufuli ni wale watu waliokuwa wanafaidika na mfumo dhaifu wa Kikwete. Watu wa kawaida maisha bado ya yale yale na hakuna kilicho badilika.
Mimi nineondoka Tanzania Tangu mwaka 1999. Na sijanufaika na utawala wa Kikwete. Na naona mabaya ya Magufuli.

Utasemaje wanaoona mabaya ya Magufuli ni wale waliofaidika na utawala wa Kikwete?
 
Obviously Heisenberg's Uncertainty Pronciple hujaifahamu ama hujaelewa inaenda mpaka kwenye kukinganisha marais.

Ni hivi, jinsi inavyozidi kuwa general ndivyo unavyozidi kuwa inaccurate. Ndiyo unavyozidisha margin of error.

Ili kuwa accurate zaidi inabidi uwe soecific zaidi.

Kwa mfano, Kikwete kampita sana Magufuli kwenye kuheshimu demokrasia na uhuru wa habari.

Magufuli anaweza kuwa kampita Kikwete kwenye kurudisha nidhamu katika utumishi wa umma na kukusanya kodi.

Watu wasio na uhuru wa demokrasia hata kuwa na nidhamu yabkweli ni shida. Hivyo Magufuli anaweza juwa anaendesha nchi kwa kutia watu woga zaidi.

Hapo utapimaje nani zaidi ya mwenzake bika kutaja specifics?
BTW mimi sikubali kabisa kabis kwamba Kikwete alikuwa anaheshimu demokrasia. Kikwete hakuheshimu demokrasia ila alikuwa legelege na anaachia mambo yajiendee. Hiyo sio demokrasia!
 
Rais wetu mwema ana speed Kali kupita rocket ya kivita.
 
Kaaa kimya boss au utafute supportive doc za multiplier effect... zinaongelewa effects na syo unavyodhani.

Aliyeleta hoja ya multiplier effect nimemuuliza ni ipi ya hiyo multiplier effect anayoingelea. Mpaka sasa yuko kimya. Midhali wewe unaonekana unaifahamu si vibaya unifafanulie ili tujenge mjadala wenye hoja.

Maana ili ziongelewe effects lazima tujue hiyo multiplier effect inayohusika kwanza. Na mwenye kuleta hizo "supportive doc" ni aliyeleta hoja.
 
Mimi nineondoka Tanzania Tangubmwaka 1999. Na sijanufaika nanutawala wa Kikwete. Na naona mabaya ya Magufuli.

Utasemaje wanaoona mabaya ya Magufuli ni wale waliofaidika na utawala wa Kikwete?
Mimi sikusema Magufuli hana mabaya. Na sipingi watu kuona mabaya yake kwani hata mimi nayaona tena ni mengi tu! Ninachosema ni kuwa wengi wa wanaopiga kelele sasa wakati wa Kikwete (ambao alikuwa mbovu mara milioni moja kuliko) walikuwa kimya lakini sasa wanapiga kelele. Kulikoni?
 
BTW mimi sikubali kabisa kabis kwamba Kikwete alikuwa anaheshimu demokrasia. Kikwete hakuheshimu demokrasia ila alikuwa legelege na anaachia mambo yajiendee. Hiyo sio demokrasia!
Aliyekataa kuiba kwa sababu ni mwoga na legelege na aliyekataa kuiba kwa sababu anaheshimu haki kwangu mimi hakimu naona wote wawili wamekataa kuiba na nikiulizwa huyu kaiba au hajaiba nitasema hajaiba.

Kikwete hakuminya demokrasia, kama ni kwa sababu yeye ni legelege au kama anaheshimu demokrasia hilo si swali muhimu kwangu. Swali muhimu ni kwamba hakuminya demokrasia (angalau kwa kiwango cha kumlinganisha na Magufuli).

Obviously tunaongea in relative terms. Huwezi kusema Magufuli kaachia demokrasia Zaidi ya Kikwete.

Kikwete hajakataza watu kufanya mikutano ya siasa, mikutano ambayo wana haki ya kikatiba kuifanya.

Magufuli kaapishwa kuilinda katiba. Anachofanya ni kuivunja.

Huyu ni dikteta, usimtete kwa kusema hataki ulegelege. Kuna kukataa ulegelege kwa kufuata sharia na kuna udikteta.

Magufuli ni dikteta.
 
Kauli zake hizi Dr Rais Magufuli tumuiteje?
Usiogope wewe
Beleshi iitwe Beleshi wala sio Kijiko kikubwa
"Mikutano ya kisiasa hadi 2020"
Lkn yy anafanya mikutano
DIKTETA UCHWARA huyu


Mmmmmmh
 
Mimi sikusema Magufuli hana mabaya. Na sipingi watu kuona mabaya yake kwani hata mimi nayaona tena ni mengi tu! Ninachosema ni kuwa wengi wa wanaopiga kelele sasa wakati wa Kikwete (ambao alikuwa mbovu mara milioni moja kuliko) walikuwa kimya lakini sasa wanapiga kelele. Kulikoni?

Hivi kuna kiongozi wa Tanzania ambaye keshawahi kupingwa na kukosolewa humu kumzidi Kikwete?

Uhai karibu wote wa JF Kikwete ndo alikuwa rais na watu tumemsema sana humu.

Sasa sijui unazungumzia watu gani hasa ambao walikuwa kimya wakati wa enzi zake.
 
Laiti kama tungekuwa na chaguzi huru na haki
laiti kama tungekuwa na tume huru ya uchaguzi....
na vingekuwepo hivyo vyote hata yeye asinge endesha mambo hivi
angekumbuka wapiga kura wanamsubiri 2020...

right now hata tufanyaje....atabaki Rais hadi 2025 unless itokee 'intervention'
Silaha zake kuu ni hizo...sasa ana sababu gani ya kujifanya anajali mwelekeo Wa nchi...?
Ingawa juna watu amenunyooshea na wamenyooka kama suruali ya kaki iliyopigwa pasi na askari aliyepo mafunzoni CCP Moshi.
 
Mimi sikusema Magufuli hana mabaya. Na sipingi watu kuona mabaya yake kwani hata mimi nayaona tena ni mengi tu! Ninachosema ni kuwa wengi wa wanaopiga kelele sasa wakati wa Kikwete (ambao alikuwa mbovu mara milioni moja kuliko) walikuwa kimya lakini sasa wanapiga kelele. Kulikoni?
Wengi kina nani?

Mimi nimepiga kelele tangu Enzi za Mkapa.
Rais yeyote aliye madarakani atapigiwa kelele tu. Urais una mengi, na rais hawezi kupatia yote hata siku moja.

Kila siku inayopita kutakuwa cha kukosoa kuhusu serikali. Sasa watu wakimpigia kelele utasemaje kwamba walikuwa kimya wakati wa Kikwete?
Hao wengi kina nani? Unaweza kuwataja majina?

Na kwa nini huangalii hoja zao wanazomkosoa Magufuli tuzichambue kama zina msingi au hazina msingi unaanza kuangalia nani kasema nini?
 
..watanzania tulitaka rais wa aina ya magufuli, tulitaka rais ambaye ana maamuzi magumu, mwenye kutoa amri na kusimamia anachokiamini,ndiye huyu sasa tumempata! M ungu alisikiliza sala zetu! wewe na vulijimaswali lako kama ulishatumbuliwa au ndugu zako wa karibu wamekubwa pole sana!..mimi niko na magufuli 100% hapa kazi tu! kaandamane uone cha mtema kuni!
Mlimtaka wewe na nani? Ulifanya utafiti? Tupia hapo basi.
 
Back
Top Bottom