Rais Magufuli, Punguza confrontation na Wazungu

Rais Magufuli, Punguza confrontation na Wazungu

Marehemu Castro alimwambia kiongozi Wa nchi moja amerika kusini kuwa wazungu sasa hiviwana utaalamu Wa kupandikiza cancer ugonjwa kwa viongozi wazalendo kwa nchi zao .Na muongo uliopita viongozi 6 waamerika kusini waliugua cancer na wrote walikuwa kosa lao ilikuwa kutetea maslahi ya nchi zao. George Bush aliwaambia waarabu wasidhani mafuta ni Mali yao Bali ni mali ya ulimwengu na wakijaribu kutumia silaha ya mafuta Marekani iko tayari kuingia vitani kuyachimba .Leo Sadam naGhadafi kilichowapata ni kwa sababu yauzalendo wao. Sisi ni wadogo mno . Silaha yetu watatumia kunyima misaada na kucteate civil unrest maana vibaraka Wa kutumika ndani watawpata kwa sababu tutakuwahoi kiuchumi Watu wanachukulia kuwa tunatishana, hapa tunatafakari kwa pamoja ili tujue adui yetu yukoje. Mzungu hana resources za kuishi bila kunyonya mataifa dhaifu. Tudeal na kwa tahadhari. EPA tumewagomea hill lipo kichwani . Madini tukiwanyima nalolitakuwa kichwani mwao. Ni mengi watawka kichwani maana wanatuumiza kila nyanja, Mwaka 1967 Tanzniania ilikuwa nauchumi unaokua haraka kuliko nchi zote za E .Afrika lakini Leo Kenya ana uchumi wakuendesha bajeti take bila misaada. Sisi tunategemea misaada ni kwa sababu wali tu hivi muda na baada ya Azimio.Kila Nina imani mheshimiwa rais anataka ajueu ukweli ili makubaliano mazuri kea maslahi ya taifa yawepo.Na ACACI A wamesemawako tayari kwa mazungumzo maana hats wao wanajua hats serikali zao wanajua huwa hazipendi kumfanya mnyonywaji Stoke damu afe . Kanuni ya Parasite haui h.Host maana na yeye atakufa KUNA NADHARIA KUWA BARALA AFRIKA LINGEKUWA NA MAZINGIRA KAMA AMERIKA MZUNGU ANGETUFANYA KAMA WAHINDI WEKUNDU AMBAO SASA WAEBAKIA NI ENDANGERED SPECIES. TUJADILI.
 
You're either with us or you are against us - George Bush Jr.

Ndiyo maana mara nyingi zinapokuja mada kuhus wawekezaji wa ki Magharibi huwa nnakumbusha kisa cha Tiny Rowlands na Nyerere.

Tiny alituumiza sana.
Ilikuaje kisa hicho?
 
Yule Hugo Chavez alikuwa na jeuri ya mafuta lakini bado alichutama kwa wazungu,ingia nao mikataba ukiwa na akili zako timamu,ulisaini halafu baada ya miaka kadhaa unaanza kuwaletea figisu!!watakumaliza wako very smart katika hilo utaburuzwa kwenye mahakama ya biashara ya kimataifa hadi uchanganyikiwe.
Mbali na kuburuzwa ktk mahakama za kimataifa za biashara hizo underground sabotage watakazokufanyia politically, economically tosha kabisa kikurudisha back to zero level. Kama nchi haya mambo historia inaonyesha tuliisha yapitia enzi za Mwl Nyerere na sera za azimio la Arusha.
 
MkamaP mzungu ni binadamu tu kama wewe, hupaswi kumuogopa binadamu mwenye akili na nguvu za kibinadamu.
Uliyoandika kwenye hii mada yako yanathibitisha kuwa shida ni inferiority complex iliopo kwa Waafrika wengi na ndiyo huu umaskini mkubwa ulowaganda na umejaa barani Afrika.

Huu ni umaskini wa kifikra na vile ni utumwa wa kifikra hakika ukiwa na mawazo kama ya mtoa mada huezi kuendelea milele na milele na Afrika haiendelei sababu ya hivi.

Hata kama huyo mzungu anaingia kuhatarisha uhai wako kwa haya uloandika utaendelea kupiga magoti na kusema acha aniue tu sababu ni mzungu!
Binadamu Mungu alikupa akili na nguvu hivi siyo mapambo anataka uvitumie upambane kwenye kipindi chote cha uhai wa maisha yako.

BADILIKENI KIFIKRA JAMANI MSIISHI NA FIKRA ZILIZOKUFA.
 
Hivi mnaochangia hapa,au apiyeibua hili anajua kuwa mkataba wa uchimbaji na usafirishaji umekaa je au unasemaje.

Makaburi yasifukuliwe ili mizimu isije kutugharikisha,
tafadhali
 
You're either with us or you are against us - George Bush Jr.

Ndiyo maana mara nyingi zinapokuja mada kuhus wawekezaji wa ki Magharibi huwa nnakumbusha kisa cha Tiny Rowlands na Nyerere.

Tiny alituumiza sana.
Kwa hili ninakuunga mkono. We are going to be armtwisted sasa sijui kama maumivu tutaweza kuyavumilia.
 
Ilikuaje kisa hicho?

Hizi ni habari ambazo wengi hawapendi kuzisikia na haziandikwi hapakwetu kama historia ya uongozo wa awau ya kwanza ili zitusaidie kwenye maamuzi ya hivi sasa. Tuliokuwepo tunazifahamu na ukizitafuta kwenye tovuti ya "Tanzania events" utazikuta kwa uchache.

Kwa ufupi, Nyerere alimnyang'anya (taifisha) mali zake Tiny Rowlands zilizokuwa hapa kwa jina LONRHO, yakiwepo mashamba na kampuni ya kuunda (assembly) matrekta. Sababu zikiwa Nyerere alimfukuza Tiny kwa kuwa eti anai "support" Rhodesia (ya wazungu) wakati Waafrika walikuwa wanadai uhuru.

Tiny akamwambia "rudisha bwana", Nyerere akatangaza hadharani kuwa "akigeuka nyuma atageuka jiwe" akimaanisha harudishi chochote. Na tukafanyishwa aandamo kumlaani Tiny na kusifia hatua aliyochukuwa Nyerere.

Tiny Rowlands akaanza kampeni kupitia familia kubwa zinazoongoza dunia zilizo nje na ndani ya serikali za kimaharabi, matokeo? Tukabaniwa kila kitu kimya kimya, tukawa hohe-hahe. Haikupita muda marehemu Nyerere akageuka nyuma, bahati nzuri hakugeuka jiwe. Akakubali kulipa (kimya kimya) kila hasara aliyomtia Tiny.

Wazungu wanawekeza kwako kwa maslahi yao, ukiwakorofisha basi serikali zao zinawa-support. Hapo sasa!

TANZANIA ANTI-LONRHO DEMONSTRATION | AP Archive

The Nationalization of Lonrho’s Business Interests in Postcolonial Tanzania | Itinerario | Cambridge Core
 
Ni suala la stratejia na mbinu stahiki. Ni kweli wazungu wanaishi kwa kunyonya mataifa masikini. Lakini tutaendelea kuitikia "hewala bwana" mpaka lini. Inabidi kuanzia mahali. Sidhani lengo la Magufuli ni kugombana na wazungu bali anajitahidi kuona kama TZ itaweza kupata a fair deal kwenye madini yetu badala ya kubakia kulalamikia mashimo baada ya migodi kufungwa.
...kosa kubwa tulilofanya kama taifa ni kukubali sera za IMF na World Bank. Hapo ndipo palikuwa mwanzo wa kufungwa pingu na wazungu. Hili pia liliendana na sisi kukubali liberalism na democracy. Hizi zote ni constructs za wazungu; inamaanisha hapo ndipo tulifunga ndoa kabisa na wazungu.

...kuna njia mbili za kufanya ili kufaidika kama taifa. Moja, ni kutumia mbinu na mikakati ya kuona namna gani tunafaidika katika hali hii iliyopo sasa. Hapa masuala ya sheria na uchumi yanachukua nafasi yake. Inahusu namna tunavyoingia mikataba ya uwekezaji na wazungu. Mikataba inabidi itengenezwe kwa terms zetu. Botswana wamefanikiwa sana katika hili. Sisi bado tunaingia mikataba nao kinyonge mno, as if hatuna kitu. Wao wana pesa na teknolojia, siye tuna maliasili. Hivyo, hapo ni 50-50, wala siyo 4-96 au 30-70!
Pili, ni kujitoa kwenye hizo pingu na ndoa. Hii ni extreme na radical way. Inahitaji kiongozi revolutionary, ila aliye smart kama Nyerere. Na Magufuli is quite the opposite, siyo revolutionary na wala smart. Kujitoa pia kutategemea na jinsi gani sisi kama taifa tupo tayari kwa aftermath ya kujitoa huko. Itakuwa balaa, maana tutagemea sanctions na isolations za kufa mtu. Itabidi tuwe katika hali ya kuweza kufanya deals kupitia South-South cooperation. Hili linawezekana, angalia uwepo wa BRICS (Brazil, India, China na ZA).

Kazi kwako Rais Magufuli!
 
Hapa kazi Tu. aroo no one is allowed to steal our national
Umeandika pumba tupu. Ukoloni mamboleo hauna nafasi karne hii ya 21. Mugabe aliwakomalia na sasa ana miaka 94 na bado anadunda pamoja na mizengwe yao. Walizuia silaha zake zilizotoka China bandarini Durban Afrika Kusini akaamrisha zirudishwe China halafu zikatumwa kwa ndege. Kontena zifunguliwe na kama kuna udanganyifu mkataba uvunjwe na mgodi uuzwe kwa wawekezaji wengine. JPM go ahead kwa hatutishwi.
 
Hizi ni habari ambazo wengi hawapendi kuzisikia na haziandikwi hapakwetu kama historia ya uongozo wa awau ya kwanza ili zitusaidie kwenye maamuzi ya hivi sasa. Tuliokuwepo tunazifahamu na ukizitafuta kwenye tovuti ya "Tanzania events" utazikuta kwa uchache.

Kwa ufupi, Nyerere alimnyang'anya (taifisha) mali zake Tiny Rowlands zilizokuwa hapa kwa jina LONRHO, yakiwepo mashamba na kampuni ya kuunda (assembly) matrekta. Sababu zikiwa Nyerere alimfukuza Tiny kwa kuwa eti anai "support" Rhodesia (ya wazungu) wakati Waafrika walikuwa wanadai uhuru.

Tiny akamwambia "rudisha bwana", Nyerere akatangaza hadharani kuwa "akigeuka nyuma atageuka jiwe" akimaanisha harudishi chochote. Na tukafanyishwa aandamo kumlaani Tiny na kusifia hatua aliyochukuwa Nyerere.

Tiny Rowlands akaanza kampeni kupitia familia kubwa zinazoongoza dunia zilizo nje na ndani ya serikali za kimaharabi, matokeo? Tukabaniwa kila kitu kimya kimya, tukawa hohe-hahe. Haikupita muda marehemu Nyerere akageuka nyuma, bahati nzuri hakugeuka jiwe. Akakubali kulipa (kimya kimya) kila hasara aliyomtia Tiny.

Wazungu wanawekeza kwako kwa maslahi yao, ukiwakorofisha basi serikali zao zinawa-support. Hapo sasa!

TANZANIA ANTI-LONRHO DEMONSTRATION | AP Archive

The Nationalization of Lonrho’s Business Interests in Postcolonial Tanzania | Itinerario | Cambridge Core
That was in the 20th century. Karne hii watu wameamka na 'options' ziko nyingi.
 
Mwache Rais apambane na hao wanyonyaji wakubwa wa dunia
Mh Rais Magufuli, ktk mambo mengi upo sahihi na kama ni makosa basi ni ya kibinadamu. Ila nafikiri kuna kitu ambacho wenda hujakipatia sawa sawa ama bado hujapata habari kwa usahihi wake.

Mosi, lazima tukubaliane na ukweli kabisa kwamba kutokana na mazingira halisi ya ulaya hawawezi kuishi kwa amani wasiponyonya kwa nguvu nchi za afrika na Karebean na uarabuni. Na hivyo, hakuna fair trade ktk vitu ambavyo wanavyovihitaji kuendesha maisha yao na kizazi chao, na ya kwamba ni lazima wachukue vitu kwa bure ama bei inayokaribia na hapo.

Cha mhimu kujiuliza je tuna nguvu za kuwasimamisha kivita ama ktk ku control financial system? Sasa tukipata majibu inabidi kuchukua tahadhari sahihi hasa tunapo deal na yalipo masilahi yao. Siyo kwamba naandika haya kwa sababu tunawaogopa ila hali halisi yenyewe inanisukuma kuandika haya. Wazungu wao wanasema "wako radhi kufanya kazi na shetani palipo na masilahi yao".

IMF, UN, World bank, mahakama za dunia na vyombo vya habari ni mali za wazungu. Na wazungu ni wamoja sana kupita kipimo. Hivyo ukizuia mali za wazungu, tuseme dhahabu, umezuia mali ya IMF ama World bank.Na hivyo hawa (IMF, World bank, UN, court zote)hawatakuja kufurahia hata kidogo, watakufanyia hujuma na kukwamisha karibu ktk kila kitu.

Maoni yangu, we have to know our place. Ya kwamba tu deal na mafisadi wetu, hawa mafisadi wa dunia jaribu ku negotiate nao objectively na wakati huohuo tukiangalia maeneo mengine yatoyotunyanyua ktk maendeleo. Kukwaruzana nao hasa ktk madini, wanaweza turudisha ktk nyakati za ujima. Hawa jamaa kwa hujuma wame qualify kwa kiwango cha juu sana.

Ushauri, kaa nao mezani mkubaliane nao amicably the way forward. Hiyo kamati uliounda hata wakikuta dhahabu wazungu wanaiba, na imejaa kwenye macontena, naamini kwenye vyombo vyao hawataandika wala kuonesha kwamba wazungu wanaiba africa. Wao watachokifanya ni ku potray wewe, wao wanavyotaka uonekane ktk jamii ya dunia. Again, chochote kamati uliyoiunda itakachokuta kwenye makontena kaa nao ukubaliane kwa mazungumzo mezani.
 
That was in the 20th century. Karne hii watu wameamka na 'options' ziko nyingi.


Tazama yaliyowakuta Saddam wa Iraq na Ghaddafi wa Libya.

Unafikiri kwanini wameangushwa wakati Saudi Arabia ambayo tuliambiwa ndiyo magaidi wote waliobomowa twin towers kwa madege haijaguswa wala kulaumiwa.
 
Halafu utayauzia wapi kama utakataa ku-negotiate nao? mtoa mada yuko sahihi kwa asilimia 100%. Ndio maana kikwete alisema ukitaka kula na wewe uliwe. Unadhani yeye hakuwa akijua kwamba wazungu wanatula? Kawaulize Zimbabwe walipochukua ardhi yao na mali yao. Wamekuwa Blacklisted na Taasisi zote kupata mikopo, si WB, IMF, IFC, IDA, nk. Hao watu waitwao wazungu wasikie tu lakini wanatisha kuliko njaa.
Kwani sasa Zimbabwe haiko? Kwa taarifa yako maisha bado yanaendelea na sasa wanatumia sarafu ya Marekani( usd dollar). Ila utu wao unaheshimika.
 
Mkuu, Kuna wapupuyu haya Mzungu akimtusi atamjibu "thank you sir".
Kama tungekuwa tunathamini UTU WETU toka mwanzo TUSINGEINGIA HII MIKATABA TATA

Rais WETU alikuwa MBUNGE NA WAZIRI kipindi cha mswada hadi SHERIA iliyotumika kusaini MIKATABA
 
Hizi ni habari ambazo wengi hawapendi kuzisikia na haziandikwi hapakwetu kama historia ya uongozo wa awau ya kwanza ili zitusaidie kwenye maamuzi ya hivi sasa. Tuliokuwepo tunazifahamu na ukizitafuta kwenye tovuti ya "Tanzania events" utazikuta kwa uchache.

Kwa ufupi, Nyerere alimnyang'anya (taifisha) mali zake Tiny Rowlands zilizokuwa hapa kwa jina LONRHO, yakiwepo mashamba na kampuni ya kuunda (assembly) matrekta. Sababu zikiwa Nyerere alimfukuza Tiny kwa kuwa eti anai "support" Rhodesia (ya wazungu) wakati Waafrika walikuwa wanadai uhuru.

Tiny akamwambia "rudisha bwana", Nyerere akatangaza hadharani kuwa "akigeuka nyuma atageuka jiwe" akimaanisha harudishi chochote. Na tukafanyishwa aandamo kumlaani Tiny na kusifia hatua aliyochukuwa Nyerere.

Tiny Rowlands akaanza kampeni kupitia familia kubwa zinazoongoza dunia zilizo nje na ndani ya serikali za kimaharabi, matokeo? Tukabaniwa kila kitu kimya kimya, tukawa hohe-hahe. Haikupita muda marehemu Nyerere akageuka nyuma, bahati nzuri hakugeuka jiwe. Akakubali kulipa (kimya kimya) kila hasara aliyomtia Tiny.

Wazungu wanawekeza kwako kwa maslahi yao, ukiwakorofisha basi serikali zao zinawa-support. Hapo sasa!

TANZANIA ANTI-LONRHO DEMONSTRATION | AP Archive

The Nationalization of Lonrho’s Business Interests in Postcolonial Tanzania | Itinerario | Cambridge Core
Mimi mwenyewe niliandamishwa, nilkuwa kidato cha nne mwaka huo. Nakumbuka tulikuwa na munkari kweli, tulikuwa tunalaani ubeberu kwa nguvu na akili zetu zote.
 
Back
Top Bottom