Mfano mzuri ni nchi ya Zimbabwe, baada ya Rais Mugabe kuwanyanganya mashamba leo hali ya uchumi wa nchi hiyo imekuwa mbaya sana, mfano mwingine ni Venezuela baada ya hayati Hugos Chaves aliyekuwa Rais wa nchi hiyo kutaifisha makampuni ya mafuta leo hii nchi hiyo pamoja na utajiri wa mafuta maandamano kila siku kutokana na hali mbaya ya uchumi, hawa wazungu walishusha bei ya mafuta kutoka dola 110 mpaka dola 50 ikawa ni vigumu kwa serikali ya Venezuela kuendelea kutoa huduma ilizokuwa inazitoa kwa wananchi wake
Mfano mkubwa ni wa hapa hapa Tanzania baada ya Azimio la Arusha mwaka 1967 Rais wa awamu ya kwanza alitaifisha makampuni, mashamba, viwanda za hawa wazungu kilichofata walituhujumu kiuchumi mpaka Mwalimu aliamua kuondoka madarakani mwaka 1985. Chukua mfano mzuri hawa majirani zetu wa Kenya walivyopiga hatua kwa kuwa na ushirikiano na hawa wazungu. Tatizo ambalo serikali ya awamu ya tano iliyorithi ni mikataba mibovu iliyosainiwa na serikali ilizotangulia ambazo inatambuliwa kimataifa.