Rais Magufuli na msafara wa magari 4

Rais Magufuli na msafara wa magari 4

Upo sahihi mkuu. Anahitaji ulinzi mkubwa kuliko viongozi waliotangulia maana kazi aliyoianza sio rahisi, ni ya hatari. Atakuwa na maadaui wengi - mafisadi, wakwepa kodi, wafanyabiashara ya madawa ya kulvya. Hawa ni watu wenye nguvu ya fedha. Sio wa kuwachukulia poa. Binafsi kuwa na msafara mdogo namna hiyo inanitia wasiwasi juu ya usalama wake. Siombei, lakini tahadhari ni bora iwe kubwa.

Kweli mkuu good point
 
Eeh Mungu uishie najua wewe ndiwe ulietupa huyu Rais Magufuli...nakuomba umlinde umtunze umkinge na kila adui wa ndani na nje..umlinde atokapo umlinde aingiapo umlinde alalapo umlinde aamkapo..eee Bwana wa Mabwana hakuna linalokushinda tusaidie please...!

Amen, Mungu pokea dua zetu kwa kumlinda Rais wetu mpendwa Dr. John Pombe Magufuli uliyetuchagulia wewe mwenyewe.
 
Mungu atakulinda Raisi wangu, tunakuombea, KIla silaha inayoinuka juu yako Raisi wangu isifanikiwe. Mungu akupe nguu ya kusimamia yote uliyoyaahidi kwa dhati
 
siungi mkono hata kidogo jambo hili
magufuli ajijue yuko katika vita nzito na wezi wakubwa wa kalamu ambao wanaweza kununua wahalifu kwa pesa yeyote na kumdhuru rais.

tunamhitaji sana magufuli na hatuko tayari kumkosa kwa hiyo ulinzi wake yafaa uongezwe mara dufu kuliko hata wa JK
 
Rais wangu Rais wangu Rais wangu tafadhali sana soma alama za nyakati. usifanye mzaha kwa swala la ulinzi wako wakati huu ambapo unatengeneza idadi kubwa ya maadui.Bado tunakuhitaji na ndo kwanza kabisa umeanza. Mh tafadhali liangalie hili. Mungu yupo na atakusaidia lakini anza wewe kwanza then utakapoishia Mungu atamalizia..
nakuombea salama
 
Jamani ulinzi ni kitu muhimu sana. Mimi napendekeza tupate uzoefu wa USA katika maswala ya ulinzi maana wao rais Kennedy alipoteza maisha akiwa barabarani na hadi leo kuna hadithi ndefuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu ambayo hakuna aliyeweza kuitatua. Na Sweden marehemu Olof Palme ambaye alipendwa na wananchi wake.

Vile vile tusisahau yaliyotokea kwa waziri mkuu wetu mpendwa marehemu Edward Moringe Sokoine, tusibweteke tuna amani lakini dunia imebadilika. Hapa hatuongelei wauza unga wa Tanzania na Mafisadi yaliyopo ndani tunaongelea wigo la wengi ambao hawaitakii Tanzania neema sina haja ya kumung'unya maneno hapa namaanisha nchi majirani Rwanda, Kenya Uganda Burundi, Malawi na nchi kama vile oops huko ulaya na Asia ambao wanafaidi mali asili ya Tanzania kwa kulipa pesa kidogo sana, iwe kwenye mazao utalii nk.

Ulinzi wetu lazima uimarike kuanzia kwenye viwanja vya ndege, mipakani nk. kwenye mahoteli nk. Ulinzi wa magari manne ni mdogo sana kwa sababu hatuna rapid response ya helicopter nk. Nafikiri tu moyoni kwamba Watanzania wenzetu walioko TISS wanafanya kazi kubwa na waendeleza heshima yetu kwa kuongeza ulinzi maana kila Mtanzania ana matumaini na maisha bora huko mbeleni. Keki ya taifa iwe kwa wote sio wachache tu wanaopenda kuja kuvuna na kutudhihaki kwa kuwahonga wachache. Matumaini yangu wanaendelea kujifunza kila siku na kutumia mbinu bora kila uchwao. Kuna msemo unasema Usione vinaelea vimeundwa. Tumlinde rais wetu kwa hali na mali hivyo magari manne hayatoshi tusije kulaumiana huko mbele - Tunaomba ulinzi uimarishwe how? Tiss, They know better hilo ndio ombi letu.
 
Kwa kasi hii inabidi style hiyo ibadirike. Anahitaji ulinzi.
Upo sahihi mkuu. Anahitaji ulinzi mkubwa kuliko viongozi waliotangulia maana kazi aliyoianza sio rahisi, ni ya hatari. Atakuwa na maadaui wengi - mafisadi, wakwepa kodi, wafanyabiashara ya madawa ya kulvya. Hawa ni watu wenye nguvu ya fedha. Sio wa kuwachukulia poa. Binafsi kuwa na msafara mdogo namna hiyo inanitia wasiwasi juu ya usalama wake. Siombei, lakini tahadhari ni bora iwe kubwa.
Basi tuwe walinzi wa rais wetu kama anavyolindwa rais wa Uruguay.

Naomba kukubaliana na kila mmoja wenu wakuu. Na hasa wewe ndugu Bukwabi. Njia nzuri ni kurudia mtindo wa Kambarage, ingawa mazingira yamebadilika kiasi fulani kadri ambavyo nimesikia. Wakati ule wanasema fedha nyingi sana ilitumika kujenga mtandao wa kitengo cha intelligence. Ofisa wa Usalama wa Taifa alilipwa Mshahara mzuri, halaf alipewa cha juu kuwa posho kwa ajili ya Mtu mwingine ambaye ni Nusu Ofisa lakini hajui ofisi ya huyu anayemlipa iko wapi, na huyu nusu ofisa anapewa fedha ya kumlipa asiyekuwa ofisa ambaye anaripoti kwa nusu ofisa akidhani ndiye ofisa, halaf huyu asiyekuwa ofisa ambaye anaripoti kwa nusu ofisa anapewa malipo kulipia taarifa kutoka kwa mtu asiyekuwa ofisa ambaye anadhani asiyekuwa ofisa ni ofisa. Hapa kazi tu! Mwenye kutaka kumdhuru huyu mtume wetu tutamjua tu!
 
Namwamini Sana Mkuu Mzee MASHIBA Wa PSU Kuwa ATAWAONGOZA Vizuri Vijana Wake Ktk KUTULINDIA Vizuri Na Kwa Uhakika Rais Wetu Kipenzi Na Kipenzi Changu Haswa Dr. John Pombe Joseph MAGUFULI.

vitu vingine uwe unakaa kimya hata kama unawajua hao watu
 
Hili sio jambo la kushangilia wala kuendekeza!
Mwambieni yupo vitani kuikomboa Nchi dhidi ya mafisadi!
Ulinzi kwake ni mhimu kuliko maono aliyonayo juu ya Tanzania yake.

Halaf mmwambie anatuudhi sana sisi wazalendo wa nchi hii......asisahau once mtu anapochaguliwa kuwa kiongozi hasa rais wa nchi.....maisha yanakuwa si ya kwake tu bali taifa zima hivyo tafadha mh rais acha masihara na maisha yetu.......jiongezee ulinzi tafadhali!!
 
Angestahili msafara wa magari mangapi?

Wewe ni mgeni hapa nchini? Kama mama Salma alikuwa anatembea na msururu wa magari 10 mmewe unafikri alikuwa anatembea na msururu wa magari mangapi?
 
Amen, Mungu pokea dua zetu kwa kumlinda Rais wetu mpendwa Dr. John Pombe Magufuli uliyetuchagulia wewe mwenyewe.

Wacha kutudanganya kwamba MUNGU aliwachagulia, alipigia kituo gani hiyo kura yake? Hebu tusimsingizie MUNGU bwana, Gufuli alishindishwa na Lubuva full stop! Kama anaongezewa ulinzi aongezewe tu, yasijekutukuta ya kutukuta tukaanza kumlalamikia MUNGU kwamba alikuwa wapi!! Kinga ni bora kuliko tiba!!
 
vitu vingine uwe unakaa kimya hata kama unawajua hao watu

Kama DG Anajulikana Kuna Tatizo Gani Huyo Akijulikana? Je Nimemtaja Kwa Uzuri au Ubaya? Halafu Tambua Ya Kwamba Zama Za Sasa Hivi Za Digital Hakuna Kitakachofichika Mkuu Na Hizi Siyo Zile Zama Za Hayati Baba Wa Taifa Kwamba Kila Kitu Tu Tunafichwa. Usalama Pia Unabadilika Kwa Kiasi Kikubwa Kutokana Na Mazingira Ya Kipindi Husika. Kama Watu Walinzi Wa Wakubwa Hao Tunaburudika Nao Sehemu Mbalimbali Na Tena Hawana Noma Itakuwa Huyu Niliyemtaja? Acha USHAMBA Halafu UKOME Na UKOMAE Kunipangia Nini Cha Kusema Humu Sawa? Kwahiyo Umenisema au Kunipiga Mkwara Ili Nijue Kuwa Na Wewe Ni Mwana UWT? Najua Wajibu Wangu Na Mwisho Wa Mipaka Yangu KIMAADILI Swine Wewe!
 
eeh mungu uishie najua wewe ndiwe ulietupa huyu rais magufuli...nakuomba umlinde umtunze umkinge na kila adui wa ndani na nje..umlinde atokapo umlinde aingiapo umlinde alalapo umlinde aamkapo..eee bwana wa mabwana hakuna linalokushinda tusaidie please...!

magufuli oyeeeeeeeeeeeeeee
kikwete oyeeeee
mkapa oyeeee
mwinyi oyeee
kinana oyeeeeeeeeee
mangula oyeeeeeee
asanteni s kwa kumkata lowassa n kutuletea tingatinga.
 
Eeh Mungu uishie najua wewe ndiwe ulietupa huyu Rais Magufuli...nakuomba umlinde umtunze umkinge na kila adui wa ndani na nje..umlinde atokapo umlinde aingiapo umlinde alalapo umlinde aamkapo..eee Bwana wa Mabwana hakuna linalokushinda tusaidie please...!

Dah! Nimesoma hii Sala nimejikuta mwili unasisimka.... Ameeni!
 
Du nimesoma hii post kuna vitu nimejifunza na nimejua kuna watu mambo wanayajua na wanaipenda nchi yao na wabampenda Rais wao.
 
Back
Top Bottom