Rais Magufuli na msafara wa magari 4

Rais Magufuli na msafara wa magari 4

tabia ya ufujaji kwa misafara mirefu ya rais ilianza wakati wa utawala wa mkapa. Nyerere na mwinyi walikuwa na misafara midogo kama huu wa jpm. Na ikumbukwe misafara mirefu siyo suala la usalama bali ni makeke (show off), ufahari (extravagance) na kiburi (arrogance) vya kijinga vya watawala wengi wa kiafrika.

'like"
 
manne ni mengi sana ili kuokoa pesa ya serikali ilifaa magari mawili yni lake na la walinzi na pikipiki moja ya mwongoza msafara
 
Na usishangae kumuona siku nyingine anaendesha mwenyewe pikipiki akiwa na msafara wa pikipiki tatu tu moja ya kwake na zingine za polisi na hakuna kufunga njia kama marais wengine.

Tehe tehe tehe, ihii hiii hii, kwikwikwikwi, ihiiiii, 😀😀😀:beer:
 
We tulia hii vita ya safisha safisha aliyoianza muda si mrefu ataongezewa ulinzi
 
Naanza kuelewa kwanini kila hotuba yake anasisitiza "...naomba mniombee na Mungu anisaidie"

atakayemdhuru magufuli ajue hata shetani atamkataa kuwa ndiye kamtuma. kila kukicha nafurahia kabumbu analolicheza rais wetu toka goli hadi goli na mpira ghafla bao limefungwa.
 
Basi tuwe walinzi wa rais wetu kama anavyolindwa rais wa Uruguay.


YES YES YES.
Tushirikiane kwa kumlinda, anayo yafanya ni kama vile ndoto. Hakika ipo siku watanzania watakua na masha mazuri, hata kama sio mazuri saaana kama ya ulaya lakini angalau basic needs zitapatika kwa wote, Kuna watu wanaishi kwa mlo mmoja kwa siku, hata huo mlo mmoja ni shida kupatikana
 
Hayo safi kabisa yanatosha...hii nchi ina amani ya nini kutembea na msururu wa migari 20!?!

Kweli Dkt Magufuli ni chaguo la Mungu. Na Mungu pekee ndiye atamlinda mja wake.
Mbona mzee Ruksa alikuwa anatembea mtaa bila ulinzi?Haya ni mazingira tu ya kujitengenezea.Tunatakiwa kutengeneza marafiki wengi kuliko maadui, I hope this is the most important formulae of life.
 
Mlinzi wa kila mtu ni Mungu,kwani Omari Juma makamu wa Raisi alifia barabarani ni kitandani.Magari mia au manne ni kumwombea Mungu yeye si anakuwa kwenye gari moja tu
 
YES YES YES.
Tushirikiane kwa kumlinda, anayo yafanya ni kama vile ndoto. Hakika ipo siku watanzania watakua na masha mazuri, hata kama sio mazuri saaana kama ya ulaya lakini angalau basic needs zitapatika kwa wote, Kuna watu wanaishi kwa mlo mmoja kwa siku, hata huo mlo mmoja ni shida kupatikana

Kweli kabisa , ni kama ameshushwa kutoka mbinguni.
Mungu wetu katuona tulivyopata shida.
Ametupa kiongozi tuliyekuwa tunamtafuta kwa muda mrefu.
 
Wewe umejuaje kama ni magufuli.? Au kila msafara unajua ni magufuli.
 
Napenda Tu NIKUHAKIKISHIE Mkuu Hayo Mambo Yameweza Kufanyika Ktk Nchi Zingine ILA Tambua Ya Kuwa Tanzania IMEBARIKIWA Kuwa Na Very Strong INTELLIGENCE Machinery Ambayo Kidogo Unaweza Kuifananisha Na Ya ISRAEL, US, CHINA Na KOREA Ya KUSINI Na Haswa Haswa KITENGO Cha Presidential Security Unit Cha TANZANIA Ni Cha KUTUKUKA Mkuu Na Kiko Very Loyal, Dedicated, Patriotic Na Committed. Bila Uimara Wa Hawa Jamaa Basi Marehemu Mchonga au Mwinyi au Mkapa au Kikwete Wasingekuwa Hai Leo Hii Kwani Tanzania Tuna MARAFIKI WANAFIKI Ambao Kwa Upande Wa Pili Ni Maadui Zetu Lakini Wanaposhindwa Ni Sehemu Moja Tu Nayo Ni Kupambana Na UIMARA Na Shirika Letu Kuu La UJASUSI ( SSIT ).

Shikamoo Mkuu
 
Ndugu zangu,Rais Magufuli anahitaji sala na dua zetu wote.Aidha anatakiwa aimarishiwe ulinzi kwasababu kwa haya anayoyafanya anagusa maslahi ya wengi.Tumpe moyo afanye makubwa zaidi ya haya.
 
Nasikia kuna jamaa mmoja ana magari ya kukodi pale ikulu, JK aliwapa ulaji wengi sana
 
Eeh Mungu uishie najua wewe ndiwe ulietupa huyu Rais Magufuli...nakuomba umlinde umtunze umkinge na kila adui wa ndani na nje..umlinde atokapo umlinde aingiapo umlinde alalapo umlinde aamkapo..eee Bwana wa Mabwana hakuna linalokushinda tusaidie please...!

Amina ...ahsante sana
 
Back
Top Bottom