Kwa upande mmoja uko sawa kwamba hela za serikali si za CCM (ingawa serikalini serikali ya CCM, inaongoza nchi nzima bila kujali vyama).
Kwa upande mwingine, hoja kwamba upinzani kutegemea fedha za serikali (ondoa za CCM) ni udhaifu ina mantiki.
Kwa sababu,ili chama kiwe na mizizi,inabidi kiwe chama cha watu. Na chamakikiwa cha watu, watu wana wajibu wa kuwekeza katika chama kwa hali na mali. Na kama upinzani haujaweza kuwashawishi watu kuwekeza katika chama kwa hali na mali, haujakomaa kuendesha nchi.
Kama upinzani haujaweza kubuni mbinu za kujiendesha bila kutegemea ruzuku za serikali miaka yote hii baada ya vyama vingi, upinzani huu haujakua vya kutosha.
Mimi si mshabiki wa CCM wala upinzani, nataka tu siasa za nchi ziende kwa viwango vya weledi wa kimataifa. Ninaona vyama vya upinzani kutegemea sana ruzuku ni tatizo, hasa kwa sababu ruzuku zinaweza kutumiwa kirahisi na watawala kuvuruga vyama.
Kwa hiyo, kwa upande mmoja mtu hatakiwi kufikiri kwamba hela za serikali zinazotakiwa kutolewa kwa wapinzani ni za CCM. Hatulipi kodi CCM.Mamlaka ya kukusanya kodi si ya CCM, ni ya Tanzania.
Kwa upande mwingine, wapinzani inawabidi waje na vyanzo mbadala vya mapato.Wajenge viwanda, viwanja vya michezo, walime mashamba etc. Pia wakusanye ada za wanachama wao.