Rais Magufuli kakomesha upinzani

Rais Magufuli kakomesha upinzani

Hata ww nyumbani ukiwa baba wa amri na matamko huwezi kujenga familia imara... Lzm ukubali challenges kutoka kwa mkeo na watoto hata kama hela unatafuta wewe.
 
Anachofanya Magufuli ni kama kufunika Moto na majivu wakati Moto upo kwa ndani,Nyerere alifuta kabisa upinzani lakini hakufanikiwa,upinzani uliendelea kuwepo.
 
Kauli hii ya kifala niliwahiisikia kijiji fulani hivi nikadhani ni kwaajili ya iliteracy, kumbe kuna watumia Key board hapa nao wanaamini kuwa hela za nchi hii ni za CCM.
Kwa upande mmoja uko sawa kwamba hela za serikali si za CCM (ingawa serikalini serikali ya CCM, inaongoza nchi nzima bila kujali vyama).

Kwa upande mwingine, hoja kwamba upinzani kutegemea fedha za serikali (ondoa za CCM) ni udhaifu ina mantiki.

Kwa sababu,ili chama kiwe na mizizi,inabidi kiwe chama cha watu. Na chamakikiwa cha watu, watu wana wajibu wa kuwekeza katika chama kwa hali na mali. Na kama upinzani haujaweza kuwashawishi watu kuwekeza katika chama kwa hali na mali, haujakomaa kuendesha nchi.

Kama upinzani haujaweza kubuni mbinu za kujiendesha bila kutegemea ruzuku za serikali miaka yote hii baada ya vyama vingi, upinzani huu haujakua vya kutosha.

Mimi si mshabiki wa CCM wala upinzani, nataka tu siasa za nchi ziende kwa viwango vya weledi wa kimataifa. Ninaona vyama vya upinzani kutegemea sana ruzuku ni tatizo, hasa kwa sababu ruzuku zinaweza kutumiwa kirahisi na watawala kuvuruga vyama.

Kwa hiyo, kwa upande mmoja mtu hatakiwi kufikiri kwamba hela za serikali zinazotakiwa kutolewa kwa wapinzani ni za CCM. Hatulipi kodi CCM.Mamlaka ya kukusanya kodi si ya CCM, ni ya Tanzania.

Kwa upande mwingine, wapinzani inawabidi waje na vyanzo mbadala vya mapato.Wajenge viwanda, viwanja vya michezo, walime mashamba etc. Pia wakusanye ada za wanachama wao.
 
Tatizo lenu mmeishiwa hoja kiasi cha kuanzisha uzushi na matusi yasiyo na tija.

Sioni kama ni kweli usemalo maana sasa hivi mkiambiwa ukweli mnasema mmetukanwa kisa mna madaraka. Halafu mkiulizwa mmetukanwaje hamna maelezo yaliyonyooka. Hebu nitajie mpinzani aliyepelekwa mahakamani kwa matusi akafungwa, zaidi ya kutumia madarakana na dola vibaya kupeleka watu gerezani. Mnasema mna hoja, lakini mtu akiwasikiliza mnajivunia kupora hoja za wapinzani!! Nilitaraji ili ithibitike kwamba wapinzani wanatukana ilipaswa ifunguliwe kesi mahakamani kisha mtu akutwe na hatia. Kinyume na hapo kinachoendelea ni kucheza siasa chafu dhidi ya wapinzani wenu kisa mko madarakani.
 
Kwa upande mwingine, wapinzani inawabidi waje na vyanzo mbadala vya mapato.Wajenge viwanda, viwanja vya michezo, walime mashamba etc. Pia wakusanye ada za wanachama wao.

Haya ndio mawazo mujarabu kabisa kwa upinzani na inabidi wayafanyie kazi haya. Ila nadhani wakitaka kufanya hayo sasa kuna uwezekano wa kukutana na mkono wa siasa chafu na hujuma za kiitikadi.
 
Ni kwa miaka mingi siasa za vyama vingi nchini zimeshuhudia upinzani wa Hali ya juu baina ya ccm na chama kikuu cha upinzani kwa wakati husika. Lakini mara zote sababu kuu ya msuguano na udhaifu kwa chama tawala ukiwa ni kulaumiwa kushindwa kusimamia rasilimali za umma na kuwa na sera legelege zinazofumbia macho wabadhirifu.
Kwa zaidi ya miaka 30 sijui kama yupo anayeweza kuelezea jambo kubwa lililofanywa na vyama vya upinzani nje ya kupiga kelele dhidi ya ubadhirifu wa viongozi wa umma!
Kwa upande wa Zanzibar angalau chama cha cuf kwa kuwa kiliwahi kuwepo madarakani wao Kuna vijimambo vichache walivitenda!
Nguvu ya siasa za upinzani sio za kitaasisi, ni watu wachache ambao hawajawahi jubadilika for ages, hapa nawazungumzia kina Lowasa, Lissu, Zito, Slaa, Mbowe etc ambao Kweli wapo very strong wakiwa mmoja mmoja Lakini si kama taasisi.
Now, mkuu wa Nchi wa sasa Dr. J.P. Magufuli, yeye kwanza hafanyi makosa ya kucheka na wabadhirifu, sio legelege na wala haonekani kwenye kashfa za kijinga.
Upande mwingine kama role model, yeye anawashinda kimsimamo wanasiasa Wengi na hivyo kuiba agenda almost zote za upinzani na kuwaacha hawana cha kufanya.
Sasa watu waliokuwa wanamtaka kiongozj jemedari, mkali na jeuri asiyeogopa wawekezaji wahuni na mzalendo, Leo wamegeuka na kuitaka demokrasia, mtu akiiba akaulizwe kama anataka kuhojiwa ili tusijepoteza wawekezaji!
Alichofanya Magufuli ni kukomesha upinzani wa kichama na sasa kuwekea upinzani wa kimaslahi baina ya wabadhirifu na wanaokula Mali za umma vs wale walio waadilifu!
Toa mwaka mmoja tuambie hiyo miaka ishirini na tisa kati ya thelathini iliyobaki CCM ilifanya nini, wapinzani hawana bajeti ulitaka watumie pesa za Freemasons?
 
Dah....hao wenye hasira [emoji13] [emoji13]
Wataje tu, au unajishuku na hasira zao?

Unaweza kuona hasira kumbe sura zao zinafanana na avatar yako tu ndivyo walivyozaliwa.

Na Scotch Whisky zikichanganywa na vitabu na BBC World Service lazima mtu akiongelea particle mpya iliyovumbuliwa leo na Magufuli katika sentensi moja uone ana hasira.
 
Tanzania hakuna vyama vya siasa, kuna magenge ya kutafuta ulaji tu.

Si CCM wala upinzani.

Na Magufuli ni gubegube ambalo linafunga kamba vitoto mikono na kuvicharaza mpaka vitokwe damu.

Huwezi kulisifia kwamba limekomesha vitoto.

Hili jitu ni hayawani lisilona simile wala rehani.
Asee!Sidhani kama uko nchi hii!maana kwa hii comment yako,Noah inakuhusu!
 
Ni kwa miaka mingi siasa za vyama vingi nchini zimeshuhudia upinzani wa Hali ya juu baina ya ccm na chama kikuu cha upinzani kwa wakati husika. Lakini mara zote sababu kuu ya msuguano na udhaifu kwa chama tawala ukiwa ni kulaumiwa kushindwa kusimamia rasilimali za umma na kuwa na sera legelege zinazofumbia macho wabadhirifu.
Kwa zaidi ya miaka 30 sijui kama yupo anayeweza kuelezea jambo kubwa lililofanywa na vyama vya upinzani nje ya kupiga kelele dhidi ya ubadhirifu wa viongozi wa umma!
Kwa upande wa Zanzibar angalau chama cha cuf kwa kuwa kiliwahi kuwepo madarakani wao Kuna vijimambo vichache walivitenda!
Nguvu ya siasa za upinzani sio za kitaasisi, ni watu wachache ambao hawajawahi jubadilika for ages, hapa nawazungumzia kina Lowasa, Lissu, Zito, Slaa, Mbowe etc ambao Kweli wapo very strong wakiwa mmoja mmoja Lakini si kama taasisi.
Now, mkuu wa Nchi wa sasa Dr. J.P. Magufuli, yeye kwanza hafanyi makosa ya kucheka na wabadhirifu, sio legelege na wala haonekani kwenye kashfa za kijinga.
Upande mwingine kama role model, yeye anawashinda kimsimamo wanasiasa Wengi na hivyo kuiba agenda almost zote za upinzani na kuwaacha hawana cha kufanya.
Sasa watu waliokuwa wanamtaka kiongozj jemedari, mkali na jeuri asiyeogopa wawekezaji wahuni na mzalendo, Leo wamegeuka na kuitaka demokrasia, mtu akiiba akaulizwe kama anataka kuhojiwa ili tusijepoteza wawekezaji!
Alichofanya Magufuli ni kukomesha upinzani wa kichama na sasa kuwekea upinzani wa kimaslahi baina ya wabadhirifu na wanaokula Mali za umma vs wale walio waadilifu!
Huu Uzi ulioleta,umetumwa kutafuta roho za watu?Wamenyamaza hamuwaonei huruma?Au hamjui kama wao pia wana familia zao?Acha hizo mkuu,tuishi kwa upendo tu,madhari watu wameamua kunyamaza,si vema kuwachokonoa
 
Huu Uzi ulioleta,umetumwa kutafuta roho za watu?Wamenyamaza hamuwaonei huruma?Au hamjui kama wao pia wana familia zao?Acha hizo mkuu,tuishi kwa upendo tu,madhari watu wameamua kunyamaza,si vema kuwachokonoa
Anayoyasema Lema ipo siku yatatimia na hapo dio heshima itarudi.
 
Kuuza nyumba za serikali kwa vimada wake
Kuvunja petrol station Mwanza na serikali kulipa
Kung'oa mabango ya mtangazo pemneni ya barabara na kunyima halmashauri mapato
Kukamata meli ya uvuvi kwa tambo na serikali kulipa bilioni kadhaa
Kutaka kuvunja ghorofa la TANESCO Ubungo
Fikiri kabla ya kupost.
 
Peoples kuweni Na akili japo kidogo basi, upinzani Ni fikra, Mbowe, Maalim Seif, Zitto nk Ni viongozi wa makundi yenye fikra zinazofanana ambayo makundi hayo yamejipa majina Kama CHADEMA, cuf, act-wazalendo nk, hata hivyo vyama vikifa leo, fikra za upinzani zitabaki hai kwa wananchi kusubiri muunganiko wenye jina jingine la kisiasa, kimsingi upinzani Ni kitu cha asili katika jamii yoyote, kinachotokea Ni kwamba upinzani hufifia au kuimarika kutegemeana Na ufanisi wa chama kinachotawala. Lakini kwa sasa ukitaka kujua ukweli afya ya upinzani ikoje, mwambie uncle Magu aruhusu mikutano, utakachokiona linganinisha Na zamani halafu ulete matokeo hapa.
Mkuu, you have made my weekend.
Kama multiple like zingekuwa zinakubali ningegonga nyingi tu,hata hivyo ubarikiwe kwa sana.
 
Hivyp watanzania wanaofurahia kufa kwa upinzani wana akili gani? Na kwa nini unalaumu viongozi kwa kufa kwao na siyo serikali. Unadhani vikifa ni faida kwa jamii ya Tanzania?
 
Back
Top Bottom