Rais Magufuli: Hata kama umekula hela si unyamaze!!

Rais Magufuli: Hata kama umekula hela si unyamaze!!

Tunajiingiza kwenye ushabiki wa kisiasa na wala sio hoja. Ni vyema rais aheshimiwe na ashauriwe
 
Definition ya uzalendo TZ ni kumtii Rais na kukubaliana naye kwa kila jambo.
 
Hii nchi sasa inakwenda kubaya..

Lazima nchi yote tuimbe na kumsifu Mkulu kwa kila afanyalo!

Yeyote anayekwenda kinyume, atabatizwa majina ya msaliti, siyo mzalendo na umenunuliwa na hao wezi wetu!
Tusaidiane kujibu na haka kaswali kakichochezi, samahani lakini...
....JE ZITTO ALIVYOITWA MSALITI NA MBOWE ILIMAANISHA MBOWE HAKOSOLEWI??
 
Na Zito akidhurika tutamuuliza Magufuli, period, maana keshaanza kama alivyofanya kwa Lisu. Siasa ni kuhoji.
Ukweli ni kuwa wewe pia huna data zinazoonyesha kuwa watu hawakufa njaa.
Kwa akili yako potofu unataka kutuambia kuwa Magufuli ndiye ana siasa za ukweli!! "NILIPOINGIA MADARAKANI NILIIKUTA SUKARI INAUZWA SHILINGI 6,000/-.........." Ndiyo siasa ya ukweli na uzalendo hiyo. Mkome kabisa nyie wachimvi. Mteteeni kwa hoja zenye mashiko!!!
Unahangaika bure kumjibu huyo mwendawazimu jingalao.
 
Kwa kweli haya ni maajabu ya rais wetu wa sasa ukitofautiana naye tu unakuwa msaliti, sio mzalendo, umehongwa, duh safari hii tumepata rais untouchable.
Mkuu huyo huyo zito alifukuzwa cdm na kuitwa msaliti. Je hiyo unaikumbuka? Kubali zito amekosa mwelekeo
 
"Mtu anasimama,anatoka mapovu,unaweza kujiuliza uzalendo wake uko wapi?,hata kama umekula hela si unyamaze".......John Pombe Magufuli, October 23, 2017

Swali
Ukitofautiana na rais sio mzalendo? Lakini kina Zitto wakati wanapambana na mikataba ya Buzwagi,Rais wakati huo alikuwa wapi. Tuseme alilipwa fedha na wawekezaji kunyamaza? Tuvumiliane tubishane kwa hoja na majibu ya nidhamu. Raia kuwaambia wengine wanatoa mapovu sio ustaarabu
Shida yao hao wapinzani hawaeleweki nini wanataka kwa manufaa ya taifa hili. Haya yote anayofanya mkulu waliyapigia kelele wao kwa miaka mingi. Sasa anayatekeleza tena mayo wanapiga. Ili kuwaelewa wapinzani wa sasa inabidi uwe umepata kilevi kidogo.
 
Hoja ni kula pesa na kutupigia kelele...kwa data za uongo.

Kosoa kwa facts sio kupotosha umma kwa maslahi ya Tumbo lako.

Kumbuka huyu huyu kibaraka ndiye aliyetaka Rais kutangaza baa la njaa kwa data zake za kughushi.

Akiachwa ataendelea...ifike mahala siasa ya uongo uongo ife kabisa nchini.


SWALI KWA MLETA MADA....JE ZITTO ALIVYOITWA MSALITI NA MBOWE ILIMAANISHA MBOWE HAKOSOLEWI??
swali lingine je makusanyo kweli 600b kwa mwzi?
"Mtu anasimama,anatoka mapovu,unaweza kujiuliza uzalendo wake uko wapi?,hata kama umekula hela si unyamaze".......John Pombe Magufuli, October 23, 2017

Swali
Ukitofautiana na rais sio mzalendo? Lakini kina Zitto wakati wanapambana na mikataba ya Buzwagi,Rais wakati huo alikuwa wapi. Tuseme alilipwa fedha na wawekezaji kunyamaza? Tuvumiliane tubishane kwa hoja na majibu ya nidhamu. Raia kuwaambia wengine wanatoa mapovu sio ustaarabu
 
Rais mtoa povu,

Zito amejiandaaje kuhusu ulinzi wake binafsi yasije yakamkuta yaliyomkuta Lisu.
 
Huyu mzee ni wa hovyo sana, hataki kukosolewa kabisa.

Anaboronga mwenyewe, akikosolewa anasema watu sio wazalendo.

Akiona ameharibu anakuja kutafuta huruma kwa wananchi, anaongea kwa hisia huku akijifanya ni mcha Mungu.
je kweli makusanyo yetu ni 600bi kama alivyosema zitto au na wew ni kasuku usiejiongeza
 
JPM na watu wa chama chake huwa wanashindwa kujibu hoja za wenzao na kuamua kutoa sababu/hoja za kitoto eti wanaowakosoa siyo wazalendo na wamehongwa ! Sasa swali ni kwamba, Ikiwa Serikali inajua km wamehongwa kwa nn kutokwa na mapovu, siwawafungulie mashitaka!?
mkuu zitto kasema haya haraka haraka kwa muda mfupi
1.makinikia pale bandarini yamerudishwa mgodini
2.mapato yameshuka hadi 600b
3.tumepewa milion 300usd ili bombadia iachiwe
ni lipi la ukweli hapo
 
Tatizo la Magufuli ni mshamba sana habari za barrick na Accacia unazipata kila siku kwenye web zao sasa anadhani watanzania ni wale wa zamani awe mpole tu sasa at Ali wa kila siku
 
Mkuu huyo huyo zito alifukuzwa cdm na kuitwa msaliti. Je hiyo unaikumbuka? Kubali zito amekosa mwelekeo
Tunazungumzia issues sio Zitto, Zitto anaweza kuwa yule yule lakini akazungumza issue tofauti.
 
Hoja ni kula pesa na kutupigia kelele...kwa data za uongo.

Kosoa kwa facts sio kupotosha umma kwa maslahi ya Tumbo lako.

Kumbuka huyu huyu kibaraka ndiye aliyetaka Rais kutangaza baa la njaa kwa data zake za kughushi.

Akiachwa ataendelea...ifike mahala siasa ya uongo uongo ife kabisa nchini.


SWALI KWA MLETA MADA....JE ZITTO ALIVYOITWA MSALITI NA MBOWE ILIMAANISHA MBOWE HAKOSOLEWI??
.
Siasa za uongo zikifa tu hapa nchini kuna mfalme flani atapotea kabisa kwenya media.
 
Back
Top Bottom