Hahahaaaaa wewe kiboko!Tunaomba Rais ahamasishe watu kupima HIV kwa mfano huu.
Ili iweje? Au kuna commission nini!Tunaomba Rais ahamasishe watu kupima HIV kwa mfano huu.
Subirini vituko siku yakuzimwa..zitazimwa hata zilizosajiliwa....subiriniRais anachemka kwa kutosemea hawa jamaa wa NIDA, zoezi hili linaenda taratibu sababu ya hawa wapuuzi wa NIDA wananchi wa vijijini wanasumbuka mno sijui kwanini mradi mkubwa wa hivi uendeshwe kijinga kiasi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Subirini vituko siku yakuzimwa..zitazimwa hata zilizosajiliwa....subirini
Huyu jamaa anaemsajili tangu lini kawa wakala jamani.
Acha nikae kimya kwanza
Tunaomba Rais ahamasishe watu kupima HIV kwa mfano huu.
Tuko kwenye lait traki kuelekea uchumi wa katikatiRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Desemba, 2019 amefanya usajili wa laini yake ya simu kwa kutumia alama za vidole na kuwasisitiza Watanzania wote wahakikishe laini zao za simu zinasajili kwa alamu za vidole kama ilivyoelekezwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Mhe. Rais Magufuli amefanya usajili huo Chato Mjini katika Mkoa wa Geita.
Hata hivyo, Mhe. Rais Magufuli ameongeza siku 20 kuanzia tarehe 01 Januari, 2020 hadi tarehe 20 Januari, 2020 kwa wote ambao watashindwa kusajili laini zao katika kipindi cha kuishia tarehe 31 Desemba, 2019 kama ilivyotangazwa na TCRA kutokana sababu mbalimbali zikiwemo kuugua na kukamilisha upataji wa namba ama Vitambulisho vya Taifa. Mhe. Rais Magufuli amesisitiza kuwa baada ya muda huo hakuna kisingizio chochote kitakachokubalika na ameagiza TCRA kuhakikisha laini ambazo hazijasajiliwa zinazimwa.
Amefafanua kuwa usajili wa laini za simu kwa alama za vidole ni muhimu kwa usalama wa nchi ikiwemo kuepusha vitendo vya utapeli na ujambazi vinavyofanywa na wahalifu, ambao licha ya wengi wao kukamatwa na vyombo vya dola wameendelea kusababisha usumbufu na upotevu mali za wananchi hususani fedha.
Pamoja na kuwasalimu wananchi wa Chato Mjini waliojitokeza kushuhudia wakati akisajili laini yake kwa alama za vidole, Mhe. Rais Magufuli amewasalimu na kusikiliza maoni yao kuhusu zoezi hili na pia mwananchi Steven Joseph Wandwi anayefanya biashara ya kuuza chipsi na mishikaki akawaongoza wenzake kumuombea Mhe. Rais Magufuli na kumshukuru kwa utumishi wake mzuri ulioongeza kasi ya maendeleo kwa Taifa hasa vijana ambao sasa wanachapa kazi bila bughudha.
Kabla ya kwenda kusajili laini yake ya simu, Mhe. Rais Magufuli ametembelea Mtaa wa Chato Kati na ametoa pole kwa familia ya Marehemu Atanasi Masansa Mnaku aliyefariki dunia juzi tarehe 25 Desemba, 2019 na mazishi yake yamepangwa kufanyika kesho.
View attachment 1304650
View attachment 1304651
View attachment 1304652
View attachment 1304653
Kumbe rais naye ni mzee wa deadline?? Alikuwa wap siku zote?? Ila hicho ni kiinimacho tu, rais hawez kusajili line mtaani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Rais ametumia urais kwa maslahi binafsi.Mgongano wa maslahi wa wazi kabisa.Alikuwa hajasajili! Amesajili leo? Kumbe kunafamilia ilikuwa na msiba.
Kama rais mwenyewe kasajiri leo raia nao wafanyeje.Mentality ya wabongo, watarelax kisha tarehe 16 ndio wataanza kujazana tena.
Sisi ambao hatuna Muda wa kwenda kusajili leo Wala kesho tunacheeeeeka tuWataongeza tu...nasema wataongezaaa!!!
Kwani si kawaida yao tu...michakato yote ya usajili huanzaga na mabiti.
Nchi ya viwonders hiiKuongeza siku bila kulikabili na kutatua tatizo la msingi ni kujidanganya. Hapa tatizo kubwa ni vitambulisho vya taifa. Inashangaza kuwa suluhu ilikuwa 'NIDA wapeni namba za vitambulisho wanaoomba vitambulisho vya taifa'! Hii ilikuwa ni suluhu ya ajabu...ikiwa mtu umemsajili na kumpa namba kwa nini husimpe kitambulisho chake? Hata suluhu hiyo ya nama nayo imeshindwa kutatua tatizo kikamilifu! Hakuna anayetuambia ni kwa nini NIDA wanashindwa kutoa vitambulisho? Hii inaathiri hata wanaotaka huduma zingine kama vile maombi ya passport. Bado tuna kumbukumbu za huko nyuma tulipoaminishwa kuwa watendaji wakuu waliokuwepo hawakuwa mafisadi tu bali ndio walisababishwa watanzania wote kukosa vitambulisho- na mfano mzuri ulikuwa tume ya taifa na vitambulisho vya mpiga kura! Je kumetokea nini sasa tofauti na huko nyuma?
Tunaambiwa hata RITA nao wanatoa vyeti vya kuzaliwa kwa kuandika kwa mkono. Waxiri mhusika anatuaminisha hii ni sawa na kuwataka wanahitaji hati hizo kwa shughuli zingine wazikubali kuwa ni sahihi!
Nilijua aongeza mshara bana 😕😕Rais John Magufuli ameongeza siku 20 kuanzia kuanzia Januari 1-20 kwa watu wote watakaoshindwa kusajili laini zao za simu ifikapo Desemba 31.
Pia, leo Desemba 27 Rais amefanya usajili wa laini yake kwa kutumia alama za vidole
Mwananchi
====
View attachment 1304669
Baadaye ahamasishe na matumiz ya kondom na Arv.Ili iweje? Au kuna commission nini!