Rais Magufuli afuta safari ya UN General Assembly

Rais Magufuli afuta safari ya UN General Assembly

wakati mwingine hii nchi naona giza, ngoja tusubiri walau ipite miaka miwili, ikifika 2020 tutafanya maamuzi katika ballot.
 
Huo mkutano una faida gani kwa Tanzania ? UNAIINGIZIA nchi pato la shilingi ngapi mwisho wa mkutano?

Viongozi hawaendi UN kwa sababu ya faida, ni sharti kwa mwanachama kuhudhuria.
 
Kutokana na janga la tetemeko la ardhi, kwa mara nyingine Mheshimiwa Rais wetu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania analazimika "kuvunja" safari ya kwenda kuhudhuria Mkutano wa 71 wa Umoja Mataifa ambao unaanza kesho tarehe 20.09.2016 hadi 30.09.2016

Kwa mujibu wa Ms. Mindi Kasiga aliyehojiwa na gazeti la The Citizen Mheshimiwa Rais amelazimika kutoenda kuhudhuria mkutano huo ili kushughulika na matokeo ya maafa ya tetemeko hilo lililochukua maisha ya Watanzania wenzetu takribani 19 huku wengine takribani 200 wakiachwa majeruhi.

NOTE: Mada mbalimbali zitajadiliwa kwenye mkutano huo lakini moja ya mada ambayo inatarajiwa kuwa na msisimko ni ile itakayozungumzia wimbi la Wakimbizi na Wahamiaji duniani. Kwa mujibu wa tovuti ya Umoja wa Mataifa, hii ni mara ya kwanza Mkutano Mkuu wa UN kukutanisha wakuu wa nchi kujadili suala hilo.

Pamoja na hilo la Wakimbizi na Wahamiaji, pia kutakuwa na kikao muhimu sana ambacho kitachukua takribani 70% ya mkutano wote kutokana na umuhimu wake. Huu ni mdahalo unaolenga kuzungumzia malengo ya maendeleo endelevu na nafasi yetu katika kusukuma mabadiliko ya kufikia malengo hayo.

United Nations

View attachment 402894

View attachment 402895
Nadhani kafanya vyema ili aokoe gharama kunawakilishi watakaonda.
 
Viongozi hawaendi UN kwa sababu ya faida, ni sharti kwa mwanachama kuhudhuria.

Udhuru unaruhusiwa acha uongo.Kama una udhuru ruksa.Kuna nchi 54 duniani ambazo sio wanachama wa Umoja wa MATAIFA na wanadunda na kuendelea na maisha kama kawaida
 
Back
Top Bottom