Rais Kikwete safarini Marekani

Rais Kikwete safarini Marekani

Mkuu jogi, nafikiri hujasoma vizuri maana Ikulu imeshafafanua kuwa hii sio sawa na anazofanyaga bali ni kwa ajili ya matibabu.
Japo swali langu mimi lilikuwa ni kama nayo tuiongeze kwenye idadi ya zile ambazo zimeshavunja rekodi ya Obasanjo au la!?
Rais Kikwete amewasili Dubai usiku jana akiwa njiani kwenda marekani kwa ajili ya matibabu na kufanya check up ya afya yake.
Maafisa wa ikulu wamethibitisha kuwa safari hii ni kwa ajili ya matibabu tu ingawa haijasemwa anasumbuliwa na nini
Tulikosea sana kumchagua huyu baba. kila siku kiguu na njia!!!
kwa kweli tuna kila sababu ya kuichukia ccm.
 
Katiba mpya ikataze madudu haya! Huyu jamaa hachoki kusafiri? Ana pepo wa safari huyu naapia!
Rais kivuli Dr.Slaa anafuta nyao zake majuzi alikuwa Marekani, Ujerumani, Italy.
 
Nyie pro-Chadema najua mna chuki sana na rais wetu JK hata kama anakwenda kutibiwa tatizo lipo wapi acheni unafiki basi, juzi hapa kiongozi wenu Dr.Slaa kaongozana na girlfriend wake Josephine kwenda Ujerumani kuangaliwa afya mlishangilia sana leo JK mnaanza kuponda acheni siasa za makengengeza.

JK ana uwezo wa kuirekebisha Muhimbili na akaenda kutibiwa pale! Sasa badala ya kutumia fedha. hizo anazosafiria kuboresha hospitali zetu anawapelekea akina Obama, kisha atadai kuwa hajui kwa nini nchi yake ni maskini! Nyimwa vyote lakini si akili!
 
Last edited by a moderator:
Jamani eeeh huyu ni Raisi wetu tuache atibiwe popote pale maana ikitokea shida itatigharimu sana kama Nchi
 
aiseeee babayangu ingekuwa obama anawapokea marais. angempokea JK mara nyingi kumbe masikini ya mungu jk anapokelewa na balozi wa tanzania nchini marekani na kama huyo hayupo hatapokelewa na balozi wa nyumba kumi marekani
 
Jamani hivi hawa mamechanics wa ndege ya rais wanapata muda wakuifanyia service kweli ndege yetu sababu kila siku ipo route tuu.Ok get well soon my prezidaa.Atarudi lini au mpk new year......................?
 
Wakitibiwa wapinzani nje ni raha tu, wakienda kutibiwa CCM ni majanga, yani siasa za nchi hii ni za kipuuzi!
 
Duh. Naona safari zimekuwa nyingi hata mi nahisi kuna issue kafatilia sio kila safari tuambiwe kunanini
 
Hivi Muhimbili walimjengea nani? Mtu aweza kupika msosi akausifia mtamu sana kisha hataki kuula! Shame on JK!

Sasa hayo angeanza kuulizwa Nyerere, Kwani ni yeye alitibiwa na hata kufia UK. Je muhimbili ilikuwa wapi? Kwanini mumsakame JK au muna lenu jambo!

Shame on u!

 
Back
Top Bottom