Rais Kikwete asaini Muswada wa Katiba

Anadhani ameikomoa CDM lakini kumbe in future amehatarisha umaarufu wa chama chake!
Najua watu watashabikia sana rais kutia saini muswada huo kama vile ulikuwa hauna mapungufu!

Kama muswada una mapungufu itajionesha kwenye sheria. Na sheria hizi za kibinaadam hubadilika badilika kila mara na huwa "revised". Sioni hapa tatizo ni nini. Na kama bungeni majority ni wachama tawala unategemea utapata nini zaidi ya wanachokitaka wao? Inatakiwa hapa ndio wapinzani wawe wabunifu kwa kuweza kuwainisha wananchi wawachaguwe kwenye chaguzi zijazo na kuwa wabunifu pia kuwakinaisha wabunge "majority" wawe wanapigania maslahi ya nchi badala ya maslahi ya chama pekee.

Yote hayo yanawezekana ikiwa tu chama pinzani kitaanza kwa kukonga nyoyo za wananchi kwa siasa safi na uongozi bora na si kwa kuingia mitaani kuanza maandamano. Maandamano hayasaidii, jifunzeni kuwa wanasiasa na si wapiganaji.
 
Ni heri CDM waseme wazi wamekubaliana nini na Rais ili ikifika wakati wawaeleza wananchi kuwa JK amekiuka yale makubaliano a,b,c..

Mnakuwa na sapoti yenye nguvu ya hoja kwasababu mtawabana kwa ushahidi huo mtakaouweka wazi, ili ikifika JK akakiuka makubaliano,halafu mkawaambia wananchi,na wao wakachaguwa kuingia mtaani endapo mtawakumbushia hayo makubaliano...sasa tofauti na hapo mnaleta sintofahamu zisizo za msingi.

Kwanza inaonekana hamna ushirikiano mzuri nyie viongozi wa juu.
 
Jamani kwanini watu wanapenda kuzungusha maneno? CHADEMA wamepeleka mapendekezo Rais kawajibu, wamekubaliana kuwa muswada usainiwe lakini kama wana hoja za msingi zitashughulikiwa bungeni na Rais kwa uwezo wake atahakikisha kuwa sheria inakuwa ya haki.

Tatizo nini?
 
Mchakato huu wa Katiba unapakana (kama siyo) na usaliti wa demokrasia na uhaini dhidi ya Jamhuri. Hivi wamepata wapi madaraka ya kufuta Katiba iliyopo na kuleta mpya? Ni wapi kwenye Katiba hii ya sasa ambapo Rais au Bunge limepewa uwezo wa kufuta Katiba ya Sasa kwa kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya? Kutoa maoni kwenye tume na kushiriki kwenye mchakato chini ya sheria hii ni kuwa mshirika wa usaliti huu wa hakimiya ya wananchi wetu.
Act No. 15 of 1984, section 12.
Nani amekwambia katiba itafutwa?....
Constitution review.... it may stay the way it is or it may be amended. After amendment(s),and approval by the majority of Tanzanians, then it will become the New constitution of URT.
 
Kama muswada una mapungufu itajionesha kwenye sheria. Na sheria hizi za kibinaadam hubadilika badilika kila mara na huwa "revised". Sioni hapa tatizo ni nini. Na kama bungeni majority ni wachama tawala unategemea utapata nini zaidi ya wanachokitaka wao? Inatakiwa hapa ndio wapinzani wawe wabunifu kwa kuweza kuwainisha wananchi wawachaguwe kwenye chaguzi zijazo na kuwa wabunifu pia kuwakinaisha wabunge "majority" wawe wanapigania maslahi ya nchi badala ya maslahi ya chama pekee.

Yote hayo yanawezekana ikiwa tu chama pinzani kitaanza kwa kukonga nyoyo za wananchi kwa siasa safi na uongozi bora na si kwa kuingia mitaani kuanza maandamano. Maandamano hayasaidii, jifunzeni kuwa wanasiasa na si wapiganaji.

Maandamano ni sehemu ya raia (hasa pale maisha ya raia yawapo duni kitambo) kusemea mapungufu ya watawala SI MAPAMBANO kama ambavyo CCM wangependa ionekane - hivyo ni muhimu CDM wakaongeza msisimko wa kuanzisha ama na kuongoza maandamano ili raia washiriki katika kubadili mwelekeo wa nchi yao.
Pia CDM na waache kususia vikao vya Bunge maana huko ndio sehemu maalum ya kuwapa CCM kibano - nashangaa hata ngeu moja hatujaona (ngeu ni sehemu ya kueleimishana tu kwa mtu mbishi) ikiwa na maana CDM wanafyata mkia kiurahisi kwa CCM hasa huko Bungeni. Kususia ni sawa na kuwaachia CCM wafanye watakacho - CCM wakiendelea wakifanya kila kitu watakavyo kiulaini basi na tusitegemee madiliko yeyote hata baada ya miaka mingi ya utawala wao.
 
Kuna jambo hapa nafikiri inabidi muelewe, katika hivi vyama nia kubwa ya CCM ni kuendelea kubaki kwenye madaraka kwa gharama yoyote na CDM nia yao ni kuchukua dola, katika hii mswaada wa sheria ya katiba inaonekana imekaa vizuri kwa chama tawala ambayo inaonekana inakibeba kiendelee kukaa madarakani hivyo basi CDM isitegemee hata siku moja kuwa mawazo yao yanaweza kufuatwa, ile kwenda ikulu ilikua sinema tu.Hata siku moja haiwezekani Paka wakawaelewana na Panya,labda Panya akikubali kuliwa na paka hapo ndio maelewano yatapatikana.

Kwa hiyo basi kama kunavimaelewano ambavyo wamefanya na wakasainishana na bado mswaada ukasainiwa na rais hapo hakuna makubaliano yoyote ni sinema tu, mie navyoelewa nia kubwa ya CDM kwenda ikulu ni walimtaka rais asisaini mswaana huo kwa sababu unamapungufu mengi na mswaada umesainiwa manake ni nini?hamna kitu hapo. Wasiwasi wangu CDM isije ikawa CCM-C na CDM ikishatekwa biashara itakua imekwisha na CCM itatawala milele bila upinzani wowote.
 
Ndugu zangu,

Pamoja na madhaifu yote yanayosemwa kuhusu JK watu lazima tutambue kuwa JK ni mamlaka ya urais yenye utashi wa kufanya lolote lile. Nina wasi wasi watu hapa ni mashabiki sana bila kuaangalia facts za upande wa pili. Hivi CDM walienda kumwambia Rais asisaini muswada au kumweleza kuwa apokee maoni ya wadau ili kuboresha muswada. Nimesikitika sana kuona hata watu ninaowaamini wametumbukia katika mtego huu.

Mimi nadhani kitendo cha JK kusaini muswada fasta anastahili kupongezwa ili kuwa na muda wa kutosha kupeleka maoni ili kama utarudishwa bungeni mwakani basi maoni ya wadau wengi yawe yamewasilishwa. Je angesaini mwezi mmoja kabla ya Bunge, je tungepata muda wa kutoa maoni?

Rais asingeweza kutosaini muswada uliopitishwa na Bunge kwa wingi wa kura impliedly wananchi wengi. Sasa CDM wao ni kikundi kidogo (uwakilishi Bungeni) na yet hawakupiga kura, JK kaamua kuwasikiliza na kuahidi kupokea maoni yao tatizo liko wapi.

JK kafanya ustaraabu sana kusaini huu muswada, maana kaanzisha mchakakato wa kupokea maoni. Subirini February 2011 bungeni kutakuwa na mabadiliko makubwa
 
Mnyika! Mlisaini nini pale? Hebu tujuze!!! Au mlienda kunywa chai na kufamiliarise mazingira ya ikulu kwa ajili ya 2015. Au ndo maana Dr. Slaa hakwenda maana anaujua usanii wa mtani wake jk.
 
Bwana Mkandara:

Mawazo yako ni mazuri sana. Isipokuwa tu unishindwa kuelewa jambo moja kwamba kila chama na kila asasi in mitazamo yake na mizingi yake. Hivyo isingewezekana kwa chama kikubwa kama CDM kuihusisha vyama au asasi nyingine kwenye hiyo mikakati yao ya kwenda Ikulu kuwasilisha maoni yao.

Kumbuka msemo huu kwamba, 'Palipo na mzoga ndipo tai(ndege) hukuzanyikia. Na pasina shaka CDM siyo mzoga. Ikulu iko wasi kwa kila chama, asasi au mtu binafisi kupeleka mapendekezo yake. Si lazima wapelekwa na CDM. Wajiamini tu wote watasikilizwa pasina shaka.
 
Ndiyo sisi yawezekana hatuna akili kiasi cha kutawala lakini si kweli kuwa ni wajinga kiasi cha kushindwa hata kuuliza wale wanaotutawala "Hivi mnatutawalatawalaje?" baba wa taifa aliwahi kuzungumza maneno yanayofanana na haya na leo naona yanatimia.

Jana taarifa kwa vyombo vya habari imesema

kuwa Muswada ule muhimu sasa umesainiwa na umekua sheria, na rais anawakaribisha wote wenye maoni kuyatoa ili tuboreshe sheria hii itupe katiba tunayaitaka".


Hivi ujumbe huu ulitolewa na.... Una maana gani kwa mwananchi wa kawaida? Anaambiwa afanye nini?

Atoe maoni juu katiba mpya au juu ya sheria ya kuandika katiba?

Katika mkanganyiko huu mimi kama mtanzania najiuliza hivi dhamira ya viongozi wetu ni nini?

Nawasilisha!
 
Yawezekana hayo ndiyo yalikuwa sehemu ya makubaliano kwamba kwanza mswada usainiwe kuwa sheria?

Tanzania tumezoea vilaka kwenye kwenye sheria mpya hivyo sitachangaa mara tu Bunge lijalo kukutana, jambo la kwanza likawa kufanyia marekebisho sheria hiyo mpya.

Kumbe nilikuwa sahihi. Soma Raia Mwema|Novemba 30-Desemba 6, 2011| UK 3

“lakini katika makubaliano yale tumeona kinachopaswa kufanyiwa mabadiliko ni sheria na si muswada. Kwa hiyo kwa lugha nyingine, Chadema wamekubali Rais asini muswada lakini mara utakapokuwa sheria basi ifikishwe bungeni kwa ajili ya mabadiliko” Raia Mwema|Novemba 30-Desemba 6, 2011| UK 3
 
Mkuu ungemwacha tu!

wote tumeona majibu yake tukapuuza.
Nadhani deep down inside ana regret aliyoandika,ama la, ana psychological problems.
SOBY,

Kuna tatizo kubwa sana la watanzania wengi sana kugawanyika kivyama at the same time kimtazamo wa kidini.

Yani haya yananishangaza sana,utakuta waislam wengi either ni CCM ama CUF,na baadhi vyama vingine.

Ni mgawanyiko ambao umelazimishiwa na ni kama umekubalika na watanzania,maana sina la kusema,matokeo ya kura ndiyo yana onyesha wazi kabisa,na pia chuki za wazi humu kwa wale ambao wanajitambulisha kama ma anti CDM...Yani ni halali kutukana "Makafiri" wa CDM,utadhani CCM ni chama halali cha kiislam!

Nilitembelea Bongo like 3 yrs ago,i mean hapo Dar. Na nina rafiki yangu msomali nikawa namwambia mambo ya JF na CDM,haah,kutaja CDM nilijuta kwanini hata niliitaja,kutaja viongozi wa CDM tu,ni chuki mbaya sana na sikujua ni kwa nini...Maybe mapropagandist wa humu ndo wamehamaiza kazi mtaani na sasa humu?

Kuna watu wameaminishwa kabisa haya mambo na nyie ambao mko humu mmesoma na muna uelewa mkubwa zaidi,chuki za kidini zina manufaa gani kama hamataki civil war?

Na hayo yakitokea, ninyi ndo mtalaumiwa kwasababu mnachangia sana huu umaluuni.
 
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.

Hatua hiyo ya Mheshimiwa Rais kutia saini Muswada huo inakamilisha safari ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa na Serikali katika kikao kilichopita cha Bunge.

Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu katika safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.

Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.

Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

29 Novemba, 2011

Kwenye red:
Hayo maoni yanapokelewa kwa utaratibu gani? Kila mtu apayuke huku mtaani akiamini yatafika kunakohusika? Nielimisheni namna ya kufikisha maoni yangu mimi nisiye na uwezo wa kukusanya waandishi wa habari au kuomba kukutana na waziri yeyote

 
Jamani kwanini watu wanapenda kuzungusha maneno? CHADEMA wamepeleka mapendekezo Rais kawajibu, wamekubaliana kuwa muiswada usainiwe lakini kama wana hoja za msingi zitashughulikiwa bungeni na Rais kwa uwezo wake atahakikisha kuwa sheria inakuwa ya haki.

Tatizo nini?

"kwa uwezo wake atahakikisha sheria inakuwa ya haki" Teh! Ever wonder. Kama mwanzo muswada wenyewe ulikua "tila lila", na leo hii umeishakuwa sheria kipi kipya cha haki hapo atakacho jitahidi kwa uwezo wake kukiweka sawa, iwapo mpaka wamepigiwa keleke ndo'wakakubali kubadili hayo machache, na kujifanya wamesahau hayo mengine. My take mshauri apanue ukubwa wa magereza ya tz na kuongeza magurunet, bila kusahau risasi za moto na yale magari ye2 ka ya zima moto.
 
kwani watatunga katiba kimyakimya? mie nafikiri kuna hatua fulani watenda kwa wananchi kwa kura za maoni, hapo si mnaweza ipiga chini katiba iliyotengenezwa na tume?

ama hakuna tena kura ya maoni ?
hata kura ya maoni ikiwepo, tatizo ni kuwa hii sheria, kwa jinsi ilivyo, inampa mamlaka rais ku-overide baadhi ya mambo. Akiona kuwa hiyo kura ya maoni italeta gozi gizo anaweza kufanya namna fulani ya kuhakikisha haiwi kikwazo.
haya mamlaka ya rais ku-ccontrol process ya kuandika katiba ndio moja ya madai makubwa ya wanagarakati na Chadema kuwa sheria haitatuletea jatiba wanayoitaka watanzania
 
hata kura ya maoni ikiwepo, tatizo ni kuwa hii sheria, kwa jinsi ilivyo, inampa mamlaka rais ku-overide baadhi ya mambo. Akiona kuwa hiyo kura ya maoni italeta gozi gizo anaweza kufanya namna fulani ya kuhakikisha haiwi kikwazo.
haya mamlaka ya rais ku-ccontrol process ya kuandika katiba ndio moja ya madai makubwa ya wanagarakati na Chadema kuwa sheria haitatuletea jatiba wanayoitaka watanzania

na c wanaharakati wa chadema 2. 2po wanaharikati 2co wa kisiasa. Bado Rais, anamamlaka makubwa juu ya sheria yenyewe. So unategemea kutajakuwa na usawa au haki juu ya sheria yenyewe?
 
Imeandikwa kwenye gazeti la Mwanahalisi la leo kuwa JK aliieleza timu iliyotumwa na chadema kuwa asingeacha kusaini
kwakuwa hali ya chama chake si nzuri kwake na ingeweza kumletea matatizo toka kwa wanaCCM. Je, hii ni kweli?

Nilipoisoma habari hii yenye kichwa cha Chadema Yatikisa Ikulu nimekuwa na mawazo toifauti kuwa ama JK:
  • aliwalisha peremende majemedari wa Chadema ili walegee na kuondoka,
  • anataka kujionesha kuwa yeye ni mtu mzuri na wabaya ni wanaCCM (chama chake),
  • anataka kutuambia kuwa chama chake kinamsaidia kufikiria ata kwa kile anachoona ni kibaya basi akiamriwa na wanachama anatekeleza
  • hasomi magazeti, kuangalia tv, makongamano, nk. mpaka chadema waende ikulu
 
Hapa imekula kwetu wananchi. Hakuna cha maana hapo. Mwageni huo muswada uliosainiwa tuusome na kuuelewa kwanza kabla hatujatoa comments. Kwa mawazo yangu ya awali kabla sijausoma ni kwamba nashangazwa na cdm walivyosaini yale makubaliano haraka haraka. Tena makubaliano yenyewe hayajaainishwa na kuwekwa wazi. Document niliyoiona ina para 2 tu.

Nashindwa kuelewa cdm walifuata nini ikulu iwapo hakuna cha maana kilichobadilika katika muswada uliopitishwa na wabunge wa ccm + ccm(b) na wala hawajamshawishi kikwete kutousaini. Lakini ninachoshangaa zaidi ni vile cdm walivyolainishwa na kusaini makubaliano ambayo hayana tija.

Haya maneno ya kusema muswada utaendelea kuboreshwa ni propaganda za kawaida za magamba. Nimesikia kuwa kuna kifungu kinachokataza kuhoji vinginevyo unaswekwa lupango. Sasa hii "tunakaribisha maoni ya wananchi kwa ajili ya kuuboresha" ni danganya toto.

Lugha ya kusainiwa kwanza halafu, halafu, halafu, hii ni kuwafanya watu hawana akili au hawazitumii akili kama magamba wanavyotufikiria siku zote. Nilitegemea cdm wakakamae muswada huo ufanyiwe kwanza marekebisho yanayostahili kabla haujasainiwa vingine cdm wangeondoka ikulu bila kusaini muafaka wowote na magamba yote yawe a au b.

NASEMA CHADEMA MMETUANGUSHA
 
Jamani kwanini watu wanapenda kuzungusha maneno? CHADEMA wamepeleka mapendekezo Rais kawajibu, wamekubaliana kuwa muiswada usainiwe lakini kama wana hoja za msingi zitashughulikiwa bungeni na Rais kwa uwezo wake atahakikisha kuwa sheria inakuwa ya haki.

Tatizo nini?

Raisi yupi huyo???
 
Back
Top Bottom