Lakini tukumbuke hakujiendea tu huko, bali kaalikwa jamani, huwezi kuacha kuendelea kutafuta eti kwa vile unadai 400M.....sidhani kama marekani ni mbaya kwa kila taifa, kuna nchi kibao zimenyookewa kwa sababu ya marekani, mfano S. korea, Taiwan, China yenyewe nk...wachina walikuwa na kasumba hiyo ya kumuona kila mtu adui au anahira, lakini baadaye wakagundua kuwa huwezi kundelea bila marekani...Tatizo sisi weusi hatujui tumia nafasi za wazi wanazotupa hao watasha kufunga magori, na tatizo la kupaisha mipira halipo kwa viongozi tu, hata sekta binafsi, mbaya zaidi kila mtu kageuka kuwa mwanasiasa, mpondaji, do we really analyse issues at au ndio JF imekuwa attacking machine dhidi ya JK au serikali? Let us be creative...tuambiane jamani isije ikawa huu nao ni mtandao wa mtu mwenye malengo ya 2010....
Mkuu una haki ya kuandika kile ambacho unaamini. Hoja ya msingi inayofanya wananchi wengi isipokuwa wewe pengine kuhoji utendaji wa mkwere ni namna anavyoshindwa kusimamia na kushughulikia kero nzito zinazoididimiza kaya hii lakini kutwa akisafiri huko na kule safari ambazo zinaigharimu serikali yetu fedha nyingi. Umewahi kufikiria kwamba msafara wake unasheheni watu wangapi na kiasi gani cha pesa kinatumika? unafahamu ni zahanati ngapi zingejengwa kwa kutumia pesa hizo? unafahamu kwamba GW Bush amemualika jamaa kwasababu anajua JK ni mpenzi wa safari? Lakini kikubwa unafahamu namna wananchi walalahoi wanavyobugudhiwa kuchangia ujenzi wa madarasa huku hao wakubwa unaowatetea wakila safari zinazoigharimu nchi?
Tuwe wakweli wa nafsi na roho zetu JK anatakiwa ajisahihishe sana katika miaka miwili iliyobaki kuweza kustand chance ya kupata hata 55% ya kura mwaka 2010 kama mbinu za medani hazitotumika!(level playing field)
JF si mtandao wa mtu mwenye malengo ya 2010 hata kidogo,ila ni mtandao uliosheheni wazalendo wa kweli wa nchi ambao hawako tayari kuita shoka jembe! at JF we call a spade a spade!