Rais Kikwete aenda Marekani

Baada ya uhusiano wa karibu na Uingereza, Israeli, nadhani Tanzania ni ya TATU sasa!
Nini kinaendelea hapa? hatuna mafuta, hatumo kwenye ukanda wa UGAIDI au tunayo URANIUM?
 
NAAM, tunatambua kwamba hivi sasa kwa matakwa ya Bwamkubwa mwenyewe Tanzania imeanza kujiandaa kuwa koloni la Marekani -kwa heri na shari!

Ninachokijua mimi ni kwamba misaada ya Marekani kwa Tanzania ni kitu kidunchu sana ukifananisha na misaada toka Sweden, Norway, Denmark lakini angalia hotuba ya Bwamkubwa imejaa Marekani, mariakani, Marekani tena na tena lakini wafadhili wa kweli hawapo.

Bila shaka huu ni mtego wa Marekani kujipromoti mbele ya mabaya yake iliyoifanya kwenye nchi za Kiislamu na kwingineko ili Waislamu waliopotea njia na ambao wameanza kukubali sasa misaada ya Marekani wawafanyie Mabwana zao Kazi ikiwa ni pamoja na kuihujumu elimu ya Kiislamu, Kurani na Uislamu wenyewe! Astaghafirulillahi- na someni Kuul audhu biraki falaki mara elfu kumuondoa dhalimu huyu!

Kila mtu anajua sasa kwamba nchi za Kushikana nazo ni China, Russia, India, Brazili, Venezuela, nchi mbalimbali za Kiarabu na hasa UAE lakini tunawashangaa CCM kutuchimbia Watanzania kaburi kwa kutuweka kwenye makwapa ya Marekani ili tuwe kama Vietnam, Iraq, Lebanon na shemu nyingine kama hizo.... ee Mola tuepushe na ujinga wetu!

Baba wa Taifa alishatuambia tuwaogope Marekani kuliko ukoma maana hicho ni kisima cha kufanya mabaya na dhuluma sehemu kubwa duniani-Iraq, Kongo, Ulaya ya Mashariki, Marekani ya Kati na kUsini na kisha kujaribu kukosha madhambi yao kwa kusaidia nchi pumbavu kama Tanzania ya sasa!

Hivi kweli dhahabu makampuni ya Marekani yanayoiba Tanzania haiwezi kutuingizia mabilioni mara 10 ya kile tunachodanganywa na Marekani kama misaada? Wewe unapewa shangaa unatoa almasi saizi ya chungwa -yaleyale ya mababu zetu.....hatutafika, tutafikwa ama kwa hakika na ukweli wa TBC!

Ujanja katika miaka hii ya GLOBALAIZESHENI sio kujiweka mzegamzega kwenye mikono ya mbabe mmoja tu duniani bali kuwachanganya wote kwa kula na huyu na yule bila kumuamini mtu yeyote katika dunia hii ya mtu kula mtu eti!

Ningeweza kukuunga mkono endapo usinge usinge mzushia uongo Mwl. Nyerere eti alisema tuiogope Marekani kama ukoma (huu ni uongo mkubwa) pia umeingiza suala la udini.
 
This is really terrible.
Hivi jamani hatuwezi kuandamana kupinga hizi ziara zisizokuwa na mbele wala nyuma?
Huyu jamaa naona yeye alichofuata ikulu ni kutanua tu hana jingine.
Huwezi kufuata bil 20 wakati kuna bilion 133 na nyinginezo zinaachwa kupotea.
Kwanza gharama ya kusafiri na kukaa huko is more than atakazoahidiwa na sio kupewa
 
nenda nenda mtalii wetu, angalia tu usiuze nchi maana sina imani na wewe
 
This is really terrible.
Hivi jamani hatuwezi kuandamana kupinga hizi ziara zisizokuwa na mbele wala nyuma?
Huyu jamaa naona yeye alichofuata ikulu ni kutanua tu hana jingine.
Huwezi kufuata bil 20 wakati kuna bilion 133 na nyinginezo zinaachwa kupotea.
Kwanza gharama ya kusafiri na kukaa huko is more than atakazoahidiwa na sio kupewa

Tunaweza kuandamana kupongeza hotuba ya JK na sio kwenye hili la masilahi ya Taifa.
 
Mimi kila wakati nikisikia Rais wetu ana mahusiana ya aina yeyote ikiwa kama ni kwenda Marekani kwa ziara au kiongozi yeyote wa Marekani kaja Tanzania roho inaniuna sana.Sijui watanzania tuna akili za namna gani.Tumeshindwa kabisa kujifunza kutokana na historia.Wamarekani hawana rafiki wa kweli.Urafiki wa Marekani ni circumctantial.Kwa maana kwamba, kama huna maslahi kwa Marekani wewe huwezi kuwa rafiki yao.Bado urafiki wa Marekani na Tanzania kwangu ni kitendawili.Nchi yeyote ambayo imekuwa rafiki wa marekani baadae imesambaratika vibaya.Wamarekani wanapata faida gani kwetu?Sisi tunasema, wametupa kinachoitwa msaada wa dola za kimarekani kama mil.700 hivi.Hata hivyo kwangu mimi huo sio msaada kabisa kwa vile they are just returning back what they stole from us.Tunachohitaji kuambiwa kwa uwazi ni kwamba urafiki huu wa Rais Kikwete ambao unaoneka uko kwenye ngazi za juu sana, una faida gani kwa wamarekani?No body offers something for nothing especially for the Americans.Rais amekwenda Marekani na ajenda za afya,elimu na uchumi.Kwa bahati mbaya hizi ndizo nyanja ambazo watanzania wanalia usiku na mchana kwamba zinazidi kuzorota.Na inasemakana kwamba World Bank,IMF,mashirika ya Umoja wa Mataifa na Marekani yenyewe yana mkono katika uzoroteshaji wa nyanja hizo.Sasa kwa Rais wetu kuwa karibu kiasi hicho na Marekani tutegemee, nini kama sio kuzorota zaidi kwa nyanja hizo?Mungu atusaidie.
 
JK inabidi awe makini kama sio kuwa strategic,hawa jamaa wako ktk mchakato wa kutafuta raisi mwengine mambo ya kujipendekeza kwa uyu Bush sasa yapungue kwani republican wanaweza pigwa chini then tukakosa mwana na mbeleko.
Vitrip vya uko sasa vipungue mpaka kieleweke
 
Wamekwenda kupanga mikakati ya kufyatua mishale ya mwisho kwa watanzania,Mungu awabariki sana!
 
Last edited:
Wandugu ndio uongozi huo......juzi tu alikuwa anapiga misele mikoani kwenye vumbi ili wadanganyika muache kidomodomo; sasa anaenda kupata 'bubble bath' na mai waifu wake mamtoni. Sisi tutaendelea kumshikia nchi yake tu pindi awapo safarini. Akirudi libeneke kama kawa....kwikwikwi!!
 
Ukute ameenda na mkwewe...kumpa maisha kidogoo..maana najuaa itaunganishwa humox2 ili wakale kuku...hawaii hukoo.....hamuamini??ok lets dig out
 
Wandugu ndio uongozi huo......juzi tu alikuwa anapiga misele mikoani kwenye vumbi ili wadanganyika muache kidomodomo; sasa anaenda kupata 'bubble bath' na mai waifu wake mamtoni. Sisi tutaendelea kumshikia nchi yake tu pindi awapo safarini. Akirudi libeneke kama kawa....kwikwikwi!!

Nani anasema alikwenda mikoani kwa manufaa ya watanzania?
Mwenzenu alikua keshaanza kampeni kisirisiri kabla hata wenzake wapinzani hawajui, ili aongezewe muda wa kula.

Kama alikwenda mikoani kuangalia miradi iliyowekwa na serikali inaendeleje kwanini anawauliza watu wa Mombo kwamba shida zenu ninini?

Kuna diwani wa serikali
Mbunge wa serikali
Diwani anapeleka shida za wananchi kwa mbunge
Mbunge anapeleka shida bungeni zipatiwe ufumbuzi
Mtu yeyote aniambie kama kuna diwani na mbunge kwanini aje kuulizia wananchi shida za Mombo?


Halafu watu mnalalamika eti watu hawaandamani lakini watanzania wengi wameamka sasa.
Juzi nilikua Mombo pale kuelekea Lushoto tukasimamishwa eti msafara wa mheshimiwa unataka kupita. Mheshimiwa alipokua anakwenda Lushoto wengi waliokuja kumlaki walikua watoto wa sekondari na msingi.
Jamaa anayekusanya alikua anawatafuta watu anasema jamani kusanyikeni kwa wengi akiona tuko wengi atasimama, wapi kila mtu anaendelea na shughuli zake.

Bwahaaaaa na kile kidiwani cha Mombo bomu kabisa, kimeulizwa maswali na JK kinatetemeka na wala hata hakijui shida za watu wake.
Sasa fikiria diwani wa CCM hajui shida za wananchi wake
Mbunge wa CCM hajui shida za wananchi wake, nilipopeleleza nasikia huyo Mbunge wa jimbo lile toka apate chake mapema [kura] hajawahi kufika Mombo

Kiujumla safari ya Tanga ilikua balaa kwake,
Alitaka kwenda Pangani kufika kwenye kivuko kimeharibika
Wananchi wakamuambia ndugu mheshimiwa mbali ya kwamba maisha ni magumu lakini hata hiki kivuko chetu kwa mamiaka sasa hakina ufumbuzi.
Wanachi wengi wa Pangani walifurahi kwamba mhe kuliona hilo na wengine walikasirika kwamba angepata kuvuka ili aje kuona na shida nyingine huku ng'ambo.

Tanzanians we have a long way to go
 
Aliesema kuwa ni Vasco da Gama hakukosea. Anaendelea kuvumbua kwa ujinga wake. Hovyoooooo.

At least Vasco da Gama alitembea nakuvumbua mambo ambayo yaliwasaidia hata wazungu wenzake huko Ulaya.

Je JK anavumbua mambo gani ambayo yanalisaidia taifa lake?

Kwenda safari yakuomba milioni 20? wakati kuna milioni 400 ambazo hazijulikani kwamba zitapatikana au hazitapatikana.

Au mheshimiwa sio mswahili nakujua ule usemi wakusema bora ndege mmoja kwenye mkono kuliko mia moja wanaoruka hewani
 
Siamini kama mkuu huwa anapata hata muda wa kupitia mafile kwa kuwa kila siku youko on board. Kwa hali hii hawezi tambua kama kuna matatizo ya wananchi, ndiyo maana alipofanya ziara huko mombo (kama mmoja wetu hapo juu alivyotuambia) aliuliza juu ya shida za wananchi. Hivi kweli mkuu hajui kwamba kuna inflation karibu katika kila kitu, barabara mbovu, Less than ten percent ya watanzania ndio wanapata huduma ya nishati ya umeme, bara bara ni mbovu na kwamba watanzania wanasubili maamuzi ya serikali juu ya Richmond, EPA, etc. Hoja za kujibu anazonnyingi, ila hawezi kukata mti aliokalia na ndo maana anauliza wananchi kama wana matatizo wayataje ingawa yote anayajua. Born voyage mwanakwetu, NY.. hiyo ni asili yako. Mbona Sarajevo huendi?
 
Usikute hata Ridhiwani yumo katika msafara kwa kisingizio cha kwenda honeymoon! Jamaa haeleweki huyu!
 
Duuu!! Jamani, mimi nadhani kwa kweli hatujatulia sisi waafrika. Umeona jinsi atakavyopekwa kwanza kuahidiwa misaada kisha siku ya mwisho ndio anakwenda kuzungumza na mwanaume Bush. Kuna kitu atakataa hata kama akiambiwa Jusuits wanataka kuimarisha base yao hapa nchini.
Bado namsaka rais wangu!!!
 
Kazi tunayo watz,kwani kama Rais anaenda kuanzisha diplomasia ya mchezo wa kikapu na timu mbili zikiwa uwanjani haya ni mauzauza.....

Mbona haionyeshi kama ataweza kukutana na viongozi wa mpira huo?ama wote lazima wanakuwepo hapo uwanjani?

Aenda furahisha macho, subirini picha. Najua alitamani sana angekuwa kama Bush na kuwa kwenye ile timu ya Beach Volleyball au Tanzania ingelkuwa na Beach Volleball, macho yake na tabasamu vinone kwa kushangilia misamba ya kiafrika....

Mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan unaanza Jumapili, aenda chafua macho kwa mara ya mwisho kabla ya kufunga 30!
 
Lakini tukumbuke hakujiendea tu huko, bali kaalikwa jamani, huwezi kuacha kuendelea kutafuta eti kwa vile unadai 400M.....sidhani kama marekani ni mbaya kwa kila taifa, kuna nchi kibao zimenyookewa kwa sababu ya marekani, mfano S. korea, Taiwan, China yenyewe nk...wachina walikuwa na kasumba hiyo ya kumuona kila mtu adui au anahira, lakini baadaye wakagundua kuwa huwezi kundelea bila marekani...Tatizo sisi weusi hatujui tumia nafasi za wazi wanazotupa hao watasha kufunga magori, na tatizo la kupaisha mipira halipo kwa viongozi tu, hata sekta binafsi, mbaya zaidi kila mtu kageuka kuwa mwanasiasa, mpondaji, do we really analyse issues at au ndio JF imekuwa attacking machine dhidi ya JK au serikali? Let us be creative...tuambiane jamani isije ikawa huu nao ni mtandao wa mtu mwenye malengo ya 2010....
 
Back
Top Bottom