Hii mada ungeleta wakati anakaribia kumaliza kipindi chake cha pili ndiyo tungeweza kuchangia vizuri. Bahati nzuri uchaguzi ujao hana mpinzani kwa hiyo uhakika wa kuendelea anao. Hifadhi huu uzi na urudishe hapa wakati anamalizia muhula wa pili tutachangia vizuri. Kwa wale waandishi wa vitabu, kuna fursa nzuri sana ya kuhandika kitabu cha utawala wa Rais Magufuli maana utawala wake ni wa peke yake na kuna mengi ya kuandika na kitabu kikapata soko ndani na nje ya nchi.
km Ndege alizonunua, kuhamia Dodoma, Miradi miwil mikubwa ya kujenga Stiegler's Gorge Dam na reli ya SGR, Tumbua tumbua kwenye kipindi chake, Afya na elimu kwa hiki kipindi chake, nidhamu kazini, alivyo deal na mafisadi, alivyokabiliana na upinzani, Anavyosifiwa, Alivyo deal na corona, Impact ya utawala wake kwenye uchumi wa Tanzania ukiangalia both positively and negatively na kufanya analysis kidogo, na mengine mengi. Unaweza kuanza research sasa hivi na mpaka anamaliza utawala wake ukawa na data za kutosha kuandika kitabu.
Unfortunately mimi si mwandishi, nilifanya makosa nkadharau lugha nikawa ninapenda mahesabu nikashindwa ku balance na imekuja kuni cost mbeleni maaana kazi ninayofanya mehesabu nina apply kama 30% hivi. Kujua lugha vizuri katika kuongea na kuandika ni zana nzuri sana na inaweza kukuinua sana huko mbeleni.