Baada ya ushindi wa kishindo tofauti na chaguzi zilizopita, siwaoni wana CCM wakisherehekea ushindi wala simuoni Mkiti wao akizunguka mikoani kuwashukuru wana CCM na wapigakura.
Ni yeye tu na msemaji wa serikali ndio wanasikika sioni wengine wakihangaika kumtetea.
Simuoni Makamu Mwenyekiti akimpongeza wala akimusaidia Mkiti wake kujibu au kutoa pole kwa wahanga.
Sijawasikia wastaafu, Kinana, Majaliwa, Makamba hata swahiba wake Kikwete.
Sijamsikia Katibu Mkuu akizungumza chochote kuhusu ushindi au kilichotokea baada ya uchanguzi.
Siwaoni wabunge kwenye majimbo yao wakiwashukuru wapiga kura wao kwa kuwapa ushindi wa kishindo.
Huku mitaani siwaoni wana CCM kindakindaki wakitamba ma pikipiki na baiskeli zilizomwagwa kabla ya uchaguzi sizioni labda huko kwenu.
Si Wenyeviti wa matawi, si Wenyeviti wa Wilaya wa CCM wala Wenyeviti wa Mikoa walioandaa mikutano ya kumpongeza Mwenyekiti wao.
Je, kawazuia, wanamuogopa, wanawaogopa wananchi au wamemsusia wasionekane na wao wamehusika na mauaji ya ndugu zao Watanganyika.
Ni yeye tu na msemaji wa serikali ndio wanasikika sioni wengine wakihangaika kumtetea.
Simuoni Makamu Mwenyekiti akimpongeza wala akimusaidia Mkiti wake kujibu au kutoa pole kwa wahanga.
Sijawasikia wastaafu, Kinana, Majaliwa, Makamba hata swahiba wake Kikwete.
Sijamsikia Katibu Mkuu akizungumza chochote kuhusu ushindi au kilichotokea baada ya uchanguzi.
Siwaoni wabunge kwenye majimbo yao wakiwashukuru wapiga kura wao kwa kuwapa ushindi wa kishindo.
Huku mitaani siwaoni wana CCM kindakindaki wakitamba ma pikipiki na baiskeli zilizomwagwa kabla ya uchaguzi sizioni labda huko kwenu.
Si Wenyeviti wa matawi, si Wenyeviti wa Wilaya wa CCM wala Wenyeviti wa Mikoa walioandaa mikutano ya kumpongeza Mwenyekiti wao.
Je, kawazuia, wanamuogopa, wanawaogopa wananchi au wamemsusia wasionekane na wao wamehusika na mauaji ya ndugu zao Watanganyika.