KHALFANI 86
Member
- May 16, 2020
- 14
- 24
MH.RAISI JOHN MAGUFULI TUTAMLIPA NINI
Hili ni swali ambalo tunaweza kuyapata majibu yake ikiwa tutajituliza na kuipata tafakuli sahihi. Hakuna Mtanzania ambae hajaiona kazi ya Mh.Raisi toka mwaka 2015. Amejitoa kwa hali na mali kuhakikisha Tanzania inabadilika katika kila eneo lake.
Haikuwa kazi ndogo ujenzi wa barabara zinavyojengwa kwa kasi kiasi hiki ,namna Mahospitali na Vituo vya afya vinavyoboreshwa na kujengwa maeneo mbalimbali nchini, jinsi uboreshaji na ununuzi wa vyombo vya usafiri kuanzia Anga, nchi kavu na majini,Tunazo ndege kubwa na za kisasa tunaweza kwenda nchi yoyote Duniani tunaipasua anga, Reli ndio hizo zinazidi kujengwa na za kisasa ,Meli na vivuko vipya tunaona vinaingizwa majini kwa kuondoa kero ya usafiri huo majini jicho letu ziwa Victoria muda sio mrefu tutaishuhudia MV Mwanza bora na ya kisasa zaidi ,na mashule mengi yamejengwa kipindi hiki kifupi cha miaka mitano.
KHALFANI najiuliza hivi mtu wa namna hii unaweza kumlipa malipo gani ambayo anaweza kufurahishwa nayo kwa aina hii ya utumishi aliotutumikia watanzani? Naendelea kuiangalia TANZANIA ya toka mwaka 2015 mpaka sasa 2020 tumepiga hatua kubwa sana. Wananchi wanafurahia maisha sasa,na kujivunia utanzania wetu. Nenda polisi kituo chochote unapokelewa utadhani umewapelekea zawadi unahudumiwa kwa usawa heshima ipo pande zote ,nenda ofisi yoyote ya Serikali hakuna tena kuzungushana nenda kesho au rudi keshokutwa ni unahudumiwa kulingana na aina ya shida yako, ofisi zote zimeonekana sasa kuwa Mwananchi ndo muajiri.
Ukiamua kuyaongelea mabadiliko ya miaka 5 hapa nchini tutakesha ndugu zangu. Ubungo pale yatakuwa maajabu ambayo hatukuyafikiria kuyaona TANZANIA ni barabara juu ya barabara aiseeee! Tazara sahivi raha sana pale Mfugale ,Mbona pale ukitoka zako Coco kuwahi posta nikupita juu ya Bahari yaaani raha juu ya raha. Kodi zetu zinaonekana nini zinafanya.
Tukiangalia namna ya kumlipa kwa haya aliyotupigania Raisi wetu ni mtihani kwani kaifanya kazi kubwa mno. Tanzania kuna uhuru wa kuabudu na Uhuru huo haupo kwenye nchi nyingi tunazijua,ni Tanzania pekee ukianzisha dini ukafata taratibu za nchi hauna kizuizi kikubwa zingatia tu taratibu za nchi,hata uamue usiabudu uwepo tu hakuna atakae kuhoji.
Wazo langu tuhakikishe tunampa zawadi ya ushindi wa kishindo yaaani tumpe kura mpaka mwenyewe ajishangae hii itakuwa ndio ahsante yetu kwake. Na ili kuufanikisha ushindi huo tuamue kuachia uhuru kwa wagombea wa nafasi zingine turuhusu wagombea wanaokubalika kwa wananchi ili wananchi waingie kwenye uchaguzi vifua vyao havina kwanini ndani mwake wafanye kuzisukuma kura za kutosha. Namaanisha ndani ya chama chetu CCM wale watu wa maamuzi waangalie sana wananchi wanamtaka nani hii itatusaidia kutuweka pamoja Katika hatua za kushambulia msako wa kuzitafuta kura zile za kishindo na awamu hii wapinzani wetu hawatokaa wasahau watakacho kiona kwenye ubao wa matokeo ya kura za jumla.
Tunafaham kuna watu wanaingia kwenye mchakato wakiwa na nia tofauti na mheshimiwa Raisi hao ndio tatizo ambao tunatakiwa kuwawahi mapemaaaa, kwani wakati tukiwaruhusu wajipenyeze tutatembea na kirusi cha kuzififisha juhudi za kuendelea kuijenga Tanzania mpya. Kuna watu hawapendeki lakini kwa kuwa wanahela wanaamini watafanya vyovyote wajipenyeze ili waende kufanya biashara zao kwenye siasa kitu ambacho ni kuidhohofisha kasi ya JPM .
Wananci wanahitaji wabunge wafuatao
Wabunge watakao ishauri vizuri serikali kuwapatia huduma stahiki kupata vituo vya afya na vyenye kuzitoa huduma bora,kuwapigania kuupata umeme ili waweze kujikita kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwenye maeneo yao, kuwajengea ushawishi wa kuwa na vyuo mbali mbali vya ufundi kwenye maeneo ili waweze kuwazalisha wataalam mbali mbali na kuchochea vijana kujiajili, kushirikiana na jamii kuondoa ujinga ,umaskini na maradhi. Wananchi wanahitaji maji barabara na huduma mbali mbali. Mbunge aguswe na maisha ya wana jimbo lake.
Wananchi hawataki wabunge wafuatao
Wabunge wa msimu wa uchaguzi baada ya hapo kukutana majaaliwa hawahitaji wabunge wenye mipango yao nje ya changamoto za kijimbo.Wabunge wa kuchagua hii kata siipendi napenda kata ile wabunge wa kugawa watu ,Wananchi hawahitaji wabunge wa kulitumia jimbo kujinufaisha wao binafsi.
Naomba nikishauri chama changu CCM, kwakuwa naamini wanayo mikakati mizuri siku zote ya kuwapata viongozi bora na makini ,basi wazingatie sana wananchi wanataka akina nani hii itatusaidia kufuta upinzani hapa nchini. Wale wanaojiaminisha kushinda ushindi wa kipesa na si ushindi wa kimapendo ya wapiga kura hao tuwa delete kabisaaaa.
Khalfani mwana wa ABUBAKARI mjukuu wa FADHILI namaliza kwa kusema ,ZAWAD ya ushindi wa kishindo kwa Mh.Raisi JOHN MAGUFULI itamuongeza nguvu katika kutupigania Wataanzania.
CHAGUA MAGUFULI 2020 KAZI IENDELEE
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili ni swali ambalo tunaweza kuyapata majibu yake ikiwa tutajituliza na kuipata tafakuli sahihi. Hakuna Mtanzania ambae hajaiona kazi ya Mh.Raisi toka mwaka 2015. Amejitoa kwa hali na mali kuhakikisha Tanzania inabadilika katika kila eneo lake.
Haikuwa kazi ndogo ujenzi wa barabara zinavyojengwa kwa kasi kiasi hiki ,namna Mahospitali na Vituo vya afya vinavyoboreshwa na kujengwa maeneo mbalimbali nchini, jinsi uboreshaji na ununuzi wa vyombo vya usafiri kuanzia Anga, nchi kavu na majini,Tunazo ndege kubwa na za kisasa tunaweza kwenda nchi yoyote Duniani tunaipasua anga, Reli ndio hizo zinazidi kujengwa na za kisasa ,Meli na vivuko vipya tunaona vinaingizwa majini kwa kuondoa kero ya usafiri huo majini jicho letu ziwa Victoria muda sio mrefu tutaishuhudia MV Mwanza bora na ya kisasa zaidi ,na mashule mengi yamejengwa kipindi hiki kifupi cha miaka mitano.
KHALFANI najiuliza hivi mtu wa namna hii unaweza kumlipa malipo gani ambayo anaweza kufurahishwa nayo kwa aina hii ya utumishi aliotutumikia watanzani? Naendelea kuiangalia TANZANIA ya toka mwaka 2015 mpaka sasa 2020 tumepiga hatua kubwa sana. Wananchi wanafurahia maisha sasa,na kujivunia utanzania wetu. Nenda polisi kituo chochote unapokelewa utadhani umewapelekea zawadi unahudumiwa kwa usawa heshima ipo pande zote ,nenda ofisi yoyote ya Serikali hakuna tena kuzungushana nenda kesho au rudi keshokutwa ni unahudumiwa kulingana na aina ya shida yako, ofisi zote zimeonekana sasa kuwa Mwananchi ndo muajiri.
Ukiamua kuyaongelea mabadiliko ya miaka 5 hapa nchini tutakesha ndugu zangu. Ubungo pale yatakuwa maajabu ambayo hatukuyafikiria kuyaona TANZANIA ni barabara juu ya barabara aiseeee! Tazara sahivi raha sana pale Mfugale ,Mbona pale ukitoka zako Coco kuwahi posta nikupita juu ya Bahari yaaani raha juu ya raha. Kodi zetu zinaonekana nini zinafanya.
Tukiangalia namna ya kumlipa kwa haya aliyotupigania Raisi wetu ni mtihani kwani kaifanya kazi kubwa mno. Tanzania kuna uhuru wa kuabudu na Uhuru huo haupo kwenye nchi nyingi tunazijua,ni Tanzania pekee ukianzisha dini ukafata taratibu za nchi hauna kizuizi kikubwa zingatia tu taratibu za nchi,hata uamue usiabudu uwepo tu hakuna atakae kuhoji.
Wazo langu tuhakikishe tunampa zawadi ya ushindi wa kishindo yaaani tumpe kura mpaka mwenyewe ajishangae hii itakuwa ndio ahsante yetu kwake. Na ili kuufanikisha ushindi huo tuamue kuachia uhuru kwa wagombea wa nafasi zingine turuhusu wagombea wanaokubalika kwa wananchi ili wananchi waingie kwenye uchaguzi vifua vyao havina kwanini ndani mwake wafanye kuzisukuma kura za kutosha. Namaanisha ndani ya chama chetu CCM wale watu wa maamuzi waangalie sana wananchi wanamtaka nani hii itatusaidia kutuweka pamoja Katika hatua za kushambulia msako wa kuzitafuta kura zile za kishindo na awamu hii wapinzani wetu hawatokaa wasahau watakacho kiona kwenye ubao wa matokeo ya kura za jumla.
Tunafaham kuna watu wanaingia kwenye mchakato wakiwa na nia tofauti na mheshimiwa Raisi hao ndio tatizo ambao tunatakiwa kuwawahi mapemaaaa, kwani wakati tukiwaruhusu wajipenyeze tutatembea na kirusi cha kuzififisha juhudi za kuendelea kuijenga Tanzania mpya. Kuna watu hawapendeki lakini kwa kuwa wanahela wanaamini watafanya vyovyote wajipenyeze ili waende kufanya biashara zao kwenye siasa kitu ambacho ni kuidhohofisha kasi ya JPM .
Wananci wanahitaji wabunge wafuatao
Wabunge watakao ishauri vizuri serikali kuwapatia huduma stahiki kupata vituo vya afya na vyenye kuzitoa huduma bora,kuwapigania kuupata umeme ili waweze kujikita kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwenye maeneo yao, kuwajengea ushawishi wa kuwa na vyuo mbali mbali vya ufundi kwenye maeneo ili waweze kuwazalisha wataalam mbali mbali na kuchochea vijana kujiajili, kushirikiana na jamii kuondoa ujinga ,umaskini na maradhi. Wananchi wanahitaji maji barabara na huduma mbali mbali. Mbunge aguswe na maisha ya wana jimbo lake.
Wananchi hawataki wabunge wafuatao
Wabunge wa msimu wa uchaguzi baada ya hapo kukutana majaaliwa hawahitaji wabunge wenye mipango yao nje ya changamoto za kijimbo.Wabunge wa kuchagua hii kata siipendi napenda kata ile wabunge wa kugawa watu ,Wananchi hawahitaji wabunge wa kulitumia jimbo kujinufaisha wao binafsi.
Naomba nikishauri chama changu CCM, kwakuwa naamini wanayo mikakati mizuri siku zote ya kuwapata viongozi bora na makini ,basi wazingatie sana wananchi wanataka akina nani hii itatusaidia kufuta upinzani hapa nchini. Wale wanaojiaminisha kushinda ushindi wa kipesa na si ushindi wa kimapendo ya wapiga kura hao tuwa delete kabisaaaa.
Khalfani mwana wa ABUBAKARI mjukuu wa FADHILI namaliza kwa kusema ,ZAWAD ya ushindi wa kishindo kwa Mh.Raisi JOHN MAGUFULI itamuongeza nguvu katika kutupigania Wataanzania.
CHAGUA MAGUFULI 2020 KAZI IENDELEE
Sent using Jamii Forums mobile app