Nimeona mtoa hoja hapo amejichanganya vya kutosha kama vile hajui anachoongea.
1. Anafananisha uchumi wa Tanzania na Marekani (yaani nchi ya kwanza duniani kwa utajiri na ya mwisho kwa umaskini) Hata tofauti haoni? Hata hivyo sishangai kwa utamaduni uliokuwepo huko Tanzania kulinganisha kila kitu na Marekani.....mbona haulinganishi uwajibikaji uliopo hapa na huko Tanzania kuona kama kweli wanaolipwa hicho kima wanastahili?
2. Magufuli (mimi sio mshabiki wake) amesema wafanyakazi wa serikali na mashirika yake (parastatal organization-kama vile NSSF, PPF, TAWIRI, TANAPA,NHC, N.K, N.K) kuwa mishahara yao itapunguzwa na wasiotaka waondoke- rais kama kiongozi wa nchi ndiyo mkubwa wa serikali yaani kwa maana nyingine ni zaidi ya CEO wa serikali mwenye maamuzi ya mwisho ambayo hayawezi kuingiliwa na aina yoyote ya board of directors au yoyote yule. Hivyo uamuzi wa mwisho ni wake kwa mujibu wa katiba, hivyo akisema anapunguza mishahara yupo sawa, akisema anapunguza wafanyakazi hakuna wa kumwingilia au kumzuia.
3. Mwandishi anafaninisha serikali na viongozi wa makampuni ya GE, GC,Walmart, GM, Microsoft na mengineyo ya hapa Marekani. KAKA UNAKOSEA SANA UTACHEKWA KAMA HUJACHEKWA BADO. Haya makampuni hayahusiki na serikali na wala serikali haina aina yoyote ya hisa kwenye kampuni hizi hata zile zinazotengeneza vifaa vya kijeshi kama Lockheed Martin, GD au Northrup Grumman, haya yanalipa kodi kama kawaida, uhusiano wake na serikali ya hapa ni pale yanapotaka kuuza silaha nchi za nje zinatakiwa ziwe na kibali cha serikali. Sasa kama ni mashirika binafsi wana haki ya kupanga kumlipa kiasi chochote mkubwa wake wa kampuni bila kuulizwa na serikali ili mradi wanalipa kodi stahiki.Mashirika ya serikali kama EPA na mengineyo mengi ya hapa yanatumika mishahara ya scale ya serikali ambayo ni mdogo sana kulinganisha na mashirika binafsi madogo kama ya radio na TV's za States tofauti.
4. Mengi ya mashirika makubwa kama TOYOTA, MACY's, Marriot,Microsoft n.k na mengineyo uliyoyataja ni ya kifamilia, hivyo hata CEO's wake wanayamiliki wenyewe hivyo usitegemee walipwe fedha kiduchu....unategemea ujilipe kidogo kwa mali yako? Au unaangalia na ku-project faida utakayoipata ndiyo ujipangie mshahara wako? Ma-CEO wa makampuni binafsi hawaongozwi na boards au hata kama boards zipo zinakuwa na ndugu watupu wengi wakiwa share holders.
5. Makampuni katika nchi tajiri yanatumia mfumo wa hisa ambazo zinagawanwa kwa kadiri ya faida iliyopatikana, hivyo mengi yanatengeneza faida ya kutisha hivyo migawanyo yao ya fedha inakuwa mikubwa
6 Kwa serikali na nchi yetu tunategemea zaidi kwenye faida ambayo inazalishwa kwa kuzungushwa kwa fedha aidha za serikali au za wafanyakazi siyo mtaji uliopatikana kama inavyokuwa kwa makampuni binafsi.......SASA KWA NINI TUWAZAWADIE WAFANYAKAZI AMBAO HAWAKUTOA JUHUDI ZAO KATIKA KUTAFUTA MITAJI NA HAWAKUANZISHA MAKAMPUNI YAO WENYEWE BALI TUNAWALIPA MALIPO MAKUBWA KWA KAZI AMBAZO WAO NI WAAJIRI WA SERIKALI KAMA WENGINE?
HITIMISHO:
Wanaolipwa fedha nyingi na makampuni makubwa ...aidha wanayamiliki au ni mali ya familia zao, changamoto walizonazo ni kubwa ambazo ni pamoja na kutafuta fedha kwenye mabenki, kutafuta masoko na mambo mengine mengi ambayo unapaswa kuyafanya ukiwa na mali yako binafsi. Sasa hawa wenzetu mnaotaka walipwe sawa na makampuni binafsi ya nje, wanapata fedha serikalini au kwenye mifuko ya jamii huku serikali ikiwa guarantor, wanafanya kazi kwa kufuata plan ya serikali iliyowekwa na wataalam wa serikali, SASA TUWALIPE MAMILIONI HAYO KWA MWEZI SAWA NA MASHIRIKA BINAFSI KWA MIPANGO IPI? Magufuli yupo sawa kukata hiyo mishahara na asiyetaka aache kazi.