PostGE2025 Jaji Chande: Thamani ya mali zilizoharibiwa na ghasia za Oktoba 29 ni Bilioni 125. Sekta binafsi thamani yake Bilioni 89, za Serikali ni Bilioni 36

PostGE2025 Jaji Chande: Thamani ya mali zilizoharibiwa na ghasia za Oktoba 29 ni Bilioni 125. Sekta binafsi thamani yake Bilioni 89, za Serikali ni Bilioni 36

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
1,125
Reaction score
3,611
Wakuu

Akizungumza Jaji Chande leo wakati anakabidhi anakabidhi Ripoti ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025, tarehe 23 Aprili, 2026, Dar es Salaam

 
Jaji Chande amesema hayo wakati Dkt. Samia Suluhu Hassan, akipokea Ripoti ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Yaliyotokea Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025, tarehe 23 Aprili, 2026, Dar es Salaam

"...Madhara ya kiuchumi. Madhara makubwa ya kiuchumi yaliyotokea ni yale yanahusu mali za watu binafsi na mali za serikali kuharibiwa. Tume imebaini kutoka vyanzo mbalimbali kuwa mali iliyoharibiwa ina thamani ya shilingi bilioni 125.

Kati ya mali hizo, mali za sekta binafsi ambazo ni watu binafsi, vituo vya mafuta, CCM na benki, zina thamani ya shilingi bilioni 89 sawa na 71.2%. Na mali za umma ambazo ni mali za serikali na taasisi kama zile shule, TRA, mahakama, polisi, DART, TANROADS, TANESCO, TTCL, zina thamani ya shilingi bilioni 36 sawa na 28.8%.

Lakini sekta binafsi ndio imepata madhara makubwa kuliko sekta ya umma. Ushahidi na waathirika wengi waliopoteza mali binafsi unaonyesha machungu waliopata na wanaendelea kuwa nayo. Mfano mmoja ni mstaafu..."

 
Huyu mzee na washirika wao wote mafala, mali zina umuhimu kuliko maisha ya watu waliowaua na kuwazika kusikujulikana?

Matako yake
 
Akizungumza wakati wa kupokea ripoti hiyo, Mheshimiwa Rais alitambua kwa uzito mkubwa madhara yaliyolikumba Taifa, akipokea maelezo kuwa matukio hayo yalisababisha vifo vya takribani watu 518, majeruhi zaidi ya 2,390, na uharibifu wa mali unaokadiriwa kufikia zaidi ya shilingi bilioni 125. Hasara hizi zimeacha majeraha makubwa ya kijamii, kiuchumi na kisaikolojia. #RipotiYaChande
Tume Ya Uchunguzi
 
Back
Top Bottom