Mkuu ktk comment yako hii inaonyesha ni kwa kiasi gani binaadamu tumekosa ile hali ya kuwa binaadamu kwa kuwapenda binaadamu wenzetu bila kujali dini/rangi/kabila/itikadi za kivyama na vingine vya kufanana na hivyo ,kwa comment yako hii inatupa picha ni kwa kiasi gani kwa baadhi ya wanachama wa ccm(wengi wao) walivyo hatari kwa kuangamiza maisha ya binaadamu mwenzio eti kisa ni mpinzani wao.
Mungu ni mkubwa mnaendelea kujifunua na mtaendelea kujifunua kadiri ya muda unavyokwenda ,binafsi nilikuwa ktk mkutano wa kufunga kampeni zile pale Soweto na mlipuko ulivyotokea nilikuwa ktk eneo la tukio na kwa jinsi ukiona miili na damu za watu zilivyokuwa zimetapakaa(kilikuwa ni kitendo cha kigaidi) dah!.Nnawapa pole wahanga wote wa tukio lile ,ni tukio ambalo sidhani kama ninaweza kulisahahu ktk maisha yangu..Hivi kweli siasa ndio iwe kigezo cha kumwaga damu za watu!!!?Kwa tuliokesha na kuomba Mungu ipo siku maombi yetu yatajibiwa......