Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,488
- 13,608
Wewe ni muumini wa JPM na awamu ya tano tena wa wazi kabisa. Nadhani pia huna biashara yoyote unayofanya yenye kukuweka karibu na bandari.Kuna trend ya wahuni kutaka marudio ya kubinafsisha mali na mashirika ya taifa halafu wanakula dili na wawekezaji feki kupora mali za umma kama walivyofanya awamu ya Mkapa.
Mama wengi hatumuamini kutokana na utashi wake kupapatikia wafanyabiashara binafsi na uwekezaji wa nje bila kuona tija kwa maendeleo ya watanzania.
Tangu aingie tumeona anafikiri kushirikisha watu binafsi kwenye mashirika ya umma bila kuona hatari ya ubabaishaji na utapeli wa wawekezaji wababaishaj.
Alipokuwa anamtumbua CEO wa bandari ametaja kwamba anakwamisha wawekezaji kama sababu kubwa.
Hapo naona ni maagizo ceo mpya awasikilize wahuni wanaojidai kutaka kuwekeza wakati nia yao ni kuja kuidumaza bandari.
Sera yetu tangu zamani ni kuhakikisha sekta muhimili za uchumi kama bandari reli mawasiliano etc zinabakia mikononi kwa umma na pia kua na mamlaka imara za kudhibiti uchumu wa taifa.
Nina mashaka na uelewa wa mama wa mambo ya uchumi. Yafaa washauri wawe na uzalendo kumuongoza vizuri.
Umeandika ulichoandika ukiongozwa na chuki zaidi kuliko uhalisia. Nenda kawaulize wenye malori namna walivyoteseka na zile foleni wakiambiwa mitambo ndani imeharibika na hakuna namna mizigo yao inaweza kushushwa.
Bandari inamhitaji mchumi wa kweli na mwenye uzoefu wa masuala ya bandari. Mtu mwenye akili za kibiashara ili iweze kuingiza pesa zinazopotea kwa kukosa usimamizi makini.
Kusema kuwa mama anawapapatikia wafanya biashara ni mtazamo duni wenye kuongozwa na akili za mfumo dume zenye kutesa waafrika wengi. Nadhani chanzo pia ni ukosefu wa upeo wa masuala ya kawaida tu.
Mama ni rais ukumbuke hilo, vyombo vyote vya ulinzi na usalama vinampa matokeo ya kazi wanazozifanya.