Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,998
Itokee siku moja Rais Wa Jamhuri yetu kwa makusudi na katika kulipiza kisasi amtie kisu mtu Ikulu wakati wa kazi (yaani akiwa ofisini), je aweza kushtakia kwa kosa la jinai? Kama siyo ni kitu gani basi kinaweza kisimzuie kuua mtu yeye mwenyewe akijua hawezi kushtakiwa hadi pale Bunge lianzishe mashtaka ya Kibunge (Impeachment procedure).
Hii ni hatari ya Katiba yetu!!
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inatoa ulinzi dhidi ya mashtaka kwa rais aliyepo madarakani na aliyestaafu katika Ibara ya 46(3) ya katiba.
Ibara hiyo inasema; "Isipokuwa kama hataacha kushika madaraka ya rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya rais kwa mujibu wa Katiba hii".
Ufafanuzi unaopatikana katika kifungu cha 46A (10), unasema kuwa rais mstaafu anayeweza kushtakiwa kwa kosa la jinai au madai ni yule aliyeondolewa madarakani kwa azimio la bunge baada ya mashtaka dhidi yake (bungeni) kuthibitika.
Kifungu hicho kinasema, "Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha rais, spika atawafahamisha rais na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi juu ya azimio la bunge, na hapo rais atawajibika kujiuzulu kabla ya siku ya tatu tangu bunge lilipopitisha azimio hilo
Sasa kama chama chake hakiko tayari kuimpeach na hivyo baada ya kupiga kura, zikakosekana kura za kumuondoa madarakani ina maana a president can get away with murder, rape, embezzlement n.k?
Wazo fikirishi
Back and forthvipi tena mbona umeamua kufukua makaburi.......
Dah imebidi nicheke tu maana makaburi unayoyafukua wewe kweli mtaalamuWazo fikirishi
Lipia kodi ya kicheko, hamna kitu ya bure etiDah imebidi nicheke tu maana makaburi unayoyafukua wewe kweli mtaalamu
heheh nkamo leo naona umeamua kufukua makaburiWazo fikirishi
Sasa kama chama chake hakiko tayari kuimpeach na hivyo baada ya kupiga kura, zikakosekana kura za kumuondoa madarakani ina maana a president can get away with murder, rape, embezzlement n.k?
Itokee siku moja Rais Wa Jamhuri yetu kwa makusudi na katika kulipiza kisasi amtie kisu mtu Ikulu wakati wa kazi (yaani akiwa ofisini), je aweza kushtakia kwa kosa la jinai? Kama siyo ni kitu gani basi kinaweza kisimzuie kuua mtu yeye mwenyewe akijua hawezi kushtakiwa hadi pale Bunge lianzishe mashtaka ya Kibunge (Impeachment procedure).
Hii ni hatari ya Katiba yetu!!
Nina yakufyaheheh nkamo leo naona umeamua kufukua makaburi
Tuna utajiri wa miungu au mimungu au mamungu katika nchi hii.MKJJ
Kwa kadri Sheria ndani ya katiba yetu zilivyo. Rais wa Tanzania ni Mungu Mtakatifu asiye takiwa kubughudhiwa na binadamu na hata malaika. Rais ni mwenye enzi yote na mapenzi yake yatimizwe mahali popote Tanzania.
Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kumshauri Mrema kuhusu kuimarisha nguvu za upinzani Bungeni, si Mrema tu ambaye hakumwelewa, watanzania wengi hatukumwelewa. Mimi pia wakati ule nilimwona Mwalimu hamnazo kabisa.
Leo hii naomba kukiri kwamba mimi ndo nilikuwa hamnazo. Mwalimu aliona makosa mengi aliyo yafanya ambayo alijua hakuna mtu mmoja awezaye kuyatatua ila Bunge lenye uwingi wa wa wabunge wa upinzani wenye upinzani Chanya.
Mpaka tutakapo badiri sheria za nchi ndani ya katiba, mtu yeyote aliye wahi kuwa Rais wa Tanzania atendelea kuwa Mungu katika Tanzania.