Rais anapoua mtu Ikulu - Shitaka la Kihalifu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,998
Itokee siku moja Rais Wa Jamhuri yetu kwa makusudi na katika kulipiza kisasi amtie kisu mtu Ikulu wakati wa kazi (yaani akiwa ofisini), je aweza kushtakia kwa kosa la jinai? Kama siyo ni kitu gani basi kinaweza kisimzuie kuua mtu yeye mwenyewe akijua hawezi kushtakiwa hadi pale Bunge lianzishe mashtaka ya Kibunge (Impeachment procedure).

Hii ni hatari ya Katiba yetu!!
 
Leo hii mtu akiua mtu ofisini kwake siyo katika kujikinga au kwa bahati mbaya bali kwa makusudi kabisa kwa vile juzi yake alikorofishana naye na aliapa "nitakuaa" na watu walisikia kiapo hicho. Mtu huyo akimuua huyo mbaya wake, Polisi hawawezi kumuachilia aendelee na kazi wakati kesi inafanyiwa uchunguzi na sidhani kampuni yoyote inaweza ikamuacha aendelee na kazi... sasa Kama Rais akiua mtu na Watanzania wote wakajua amefanya hivyo kama hataki kujiuzulu mnajua kuwa ataendelea kuwa Rais na shughuli zake kama kawaida ikiwemo kutia sahii wauaji wengine wanyongwe?
 
MKJJ

Kwa kadri Sheria ndani ya katiba yetu zilivyo. Rais wa Tanzania ni Mungu Mtakatifu asiye takiwa kubughudhiwa na binadamu na hata malaika. Rais ni mwenye enzi yote na mapenzi yake yatimizwe mahali popote Tanzania.

Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kumshauri Mrema kuhusu kuimarisha nguvu za upinzani Bungeni, si Mrema tu ambaye hakumwelewa, watanzania wengi hatukumwelewa. Mimi pia wakati ule nilimwona Mwalimu hamnazo kabisa.
Leo hii naomba kukiri kwamba mimi ndo nilikuwa hamnazo. Mwalimu aliona makosa mengi aliyo yafanya ambayo alijua hakuna mtu mmoja awezaye kuyatatua ila Bunge lenye uwingi wa wa wabunge wa upinzani wenye upinzani Chanya.

Mpaka tutakapo badiri sheria za nchi ndani ya katiba, mtu yeyote aliye wahi kuwa Rais wa Tanzania atendelea kuwa Mungu katika Tanzania.
 


...Isipokuwa kama hataacha kushika madaraka ya rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A (10) !!! ...au wanasheria mnalichambuaje hili???
 
Sasa kama chama chake hakiko tayari kuimpeach na hivyo baada ya kupiga kura, zikakosekana kura za kumuondoa madarakani ina maana a president can get away with murder, rape, embezzlement n.k?
 
Sasa kama chama chake hakiko tayari kuimpeach na hivyo baada ya kupiga kura, zikakosekana kura za kumuondoa madarakani ina maana a president can get away with murder, rape, embezzlement n.k?

...kwa mujibu wa katiba ndivyo hivyo ndugu yangu, ushaambiwa NI MARUFUKU!!! kwa hiyo fingers crossed na mswalie mtume nyingi Mheshimiwa asije teleza akamlipua mtu ubongo, au kumtoa utumbo mwananchi. ndio maana kwa katiba hiyo hiyo NI MARUFUKU kumshtaki Mheshimiwa mstaafu Bw BWM dhidi ya 'tuhuma' za rada nk alipokuwa madarakani, milele na milele -Ameen!.

...La kujiuliza ni, hiyo katiba ya 1977 (baada ya miaka 30) inakidhi mahitaji ya Taifa la Tanzania kwenye mfumo wa vyama vingi haswa kwenye uwajibikaji wa/accountability ya VIONGOZI? na kama jibu ni HAPANA, TANZANIA tufanye nini ili Viongozi 'majahili' wapate kushitakiwa bila 'kulindwa' na wabunge wa chama tawala au chama kilicho na nguvu bungeni? nadhani wakati umefika kila mtanzania ajifunze haki zake za uraia, na somo la kuchambua katiba lianze kufundishwa kuanzia primary schools, kila mtu ajue HAKI zake za URAIA!
 
Sasa kama chama chake hakiko tayari kuimpeach na hivyo baada ya kupiga kura, zikakosekana kura za kumuondoa madarakani ina maana a president can get away with murder, rape, embezzlement n.k?

Tz wonders !
CCM mbele kwa mbeleeeeeeeeeeeee!.
Hii ndiyo kiasi gani tuwaumini feki wa kesho yetu.
 


Raisi wa JMTZ yuko juu ya Sheria za JMTZ, kuna sababu kwa nini iko hivyo, ni kama British Royal Familly, Malkia wa Uingereza ambaye ndiye Mkuu wa nchi yuko Juu ya Sheria zote za nchi hiyo, sasa swali kwako kwa nini Uingereza hawabatilishi hilo? Usiniambie Waingereza ni wajinga kwa maana kama ni kuelewa Sheria wao wana uelewa mkubwa wa Sheria klk sisi kwani hata Sheria zetu ni Utamaduni wao!

Hivyo kila jambo lina sababu inawezekana baadhi yetu hatuzijui sababu lkn haimaanishi kwamba hazipo na labda siku moja tutakuja kuelewa kwa nini iliamriwa iwe hivyo!

Binafsi napendekeza kama vile swala la kofia mbili yaani Uraisi na Uwenyekiti wa Chama vyote vibakie kama vilivyo kwa sasa!
 
Tuna utajiri wa miungu au mimungu au mamungu katika nchi hii.
 
Mbona mambo mengine ni rahisi kuyajadili; theoretically swali hili bado halijajaribiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…