Kumbe msiba sio faragha tena, kumbe msiba sio suala la familia tena, kumbe nguzo na misingi ya ndoa za kikristo sio muhimu tena, kumbe msemaji wa familia sio muhimu tena kuliko kile kinachoazagaa mitaani, na muhimu zaidi; kumbe mtu mwenye cheo cha juu zaidi tulimpa pia madaraka ya kuyaongea yale yanayogusa maisha binafsi?
Wasomi wanatofautisha personal life na public life ya mtu. Personal life ya mtu haiongelewi publicly unless mwongeaji amepata concent ya mtu anayeongelewa. Ukiachia hayo personal life inaficha mambo mengi kadhalika mambo mengi yanakuwa sensored kabla hayajaenda hadharani. Katika mazingira ya kifo familia ndio inayofanya sensoring ya mambo ambayo marehemu kayafanya na kukubaliana yapi yasemwe na kwa tune na busara gani. Manake hapa FAMILIA KWANZA SIASA BAADAYE.
Sasa viongozi wetu ambao tunaamini wamesoma na kujuwa na kuheshimu personal life, wa mtu na mfu, na kuheshimu uamuzi wa wafiwa walitakiwa wakemee kwa nguvu zote pale kiongozi moja anapovaa joho la familia ya mfu kwa kutumia cheo. Viongozi hawa walitakiwa wawe wakwanza kujuwa kwamba kutaja idadi ndogo ya wake na watoto wa marehemu kamwe haina maana kutowatambuwa watoto wengine na kushirikiana nao. Kama kiongozi ameguswa na ugomvi miongoni mwa watoto na wake bado ana nguvu kubwa sana na uwezo mkubwa wa kuwasaidia watoto na wake wote anaoamini ni wake na watoto halali wa marehemu. Bado angefanya utafiti akapata idadi kamili ya watoto na wake (kuliko alivyokuwa anabahatisha idadi kwenye hotuba, hakutakiwa kubahatisha kwa uwezo alionao).
Lazima kuwe na jitihada ya kuheshimu personal life and individual liberty. Tuwakemee viongozi wetu wanapoacha kutekeleza majukumu ya kitaifa na badala yake kuingilia kwa undani individual liberty na kujikuta tumegawanyika kimtazamo na fikra kwenye mambo ambayo tuliungana tangu uhuru.