I am confused...Unasema JK kafanya uamuzi sahihi kumchagua Abdallah maana jamaa ni mtu safi na hataki upuuzi lakini at the same time unasema ni mwoga kufanya maamuzi!!!!!! Leadership is about making decision na mtu mwoga kufanya maamuzi hafai kuwa kiongozi. Kama ni kweli Abdallah ni mwoga kufanya maamuzi basi ofisi hii haimfai hata kidogo hata kama angekuwa mwadilifu kama malaika maana kuna wakati itabidi afanye maamuzi mazito na hatayafanya maana ni mwoga. Watu waoga wa kufanya maamuzi huwa wanatakiwa wawe chini ya mtu fulani ili wao wawe wanapokea orders tu na kuzifanyia kazi ili likitokea tatizo aseme boss ndo aliniambia nifanye
Kama Jakaya anataka kufanya replacement kwenye hiyo nafasi anatakiwa kutambua kwamba
so far hicho ndio kitengo pekee cha serikali ambacho wananchi wanaimani nacho, akiamua kukivuruga,
atafupisha siku zake magogoni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemeteua Bw. Mohammed A. Mtonga (52) kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali (Internal Auditor General).
Bw. Mtonga ni msomi mwenye Shahada ya Uzamili katika masuala ya Fedha (MSc in Corporate Finance) toka Chuo Kikuu cha Salford nchini uingereza.
Aidha Bw. Mtonga anayo Shahada ya Uhasibu ya CPA (T) inayotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) na Stashada ya Juu ya Uhasibu (Advanced Diploma in Professional Accountancy) toka Chuo cha Jamii Nyegezi ambacho kwa sasa ni Chuo Kikuu cha Mt. Augustine cha Mwanza.
Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mtonga amekuwa na utumishi wa miaka 32 katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Heasabu ambapo amewahi kushika nyadhifa mbalimbali.
Nyadhifa alizowahi kushika Bw. Mtonga ni pamoja na Afisa Masuuli na Mkaguzi wa Hesabu wa Kanda. Pia amewahi kuwa Mkaguzi wa Hesabu Mkazi katika mkoa wa Lindi, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Makao Makuu ya Jeshi (Ngome).
Uteuzi huu umeanza toka tarehe 06 Aprili, 2011.
source: Wavuti - Habari
Huyu ni dini gani?
ukisema nikweli masjid nisawa nakusema 'jamaa freshi sana sema tuu mmasai' huo ni mfano mzuri sana wa mawazo yakibaguzi. Inamaana watu wakiwa waislamu na wana qualifications zote zinazohitajika inakuwa poa JAPOKUWA ni waislamu!! Inasikitisha sana kuona kuwa Tanzania kweli kuna watu wanamawazo ya namna hii. Sijuii hii sumu inatokana na nini? Sinto toa ata onyo kwasababu madhara yake wote twayajua.Ni kweli Masjid lakini jamaa shule iko na uzoefu.Mpeni haki yake
ukisema nikweli masjid nisawa nakusema 'jamaa freshi sana sema tuu mmasai' huo ni mfano mzuri sana wa mawazo yakibaguzi. Inamaana watu wakiwa waislamu na wana qualifications zote zinazohitajika inakuwa poa JAPOKUWA ni waislamu!! Inasikitisha sana kuona kuwa Tanzania kweli kuna watu wanamawazo ya namna hii. Sijuii hii sumu inatokana na nini? Sinto toa ata onyo kwasababu madhara yake wote twayajua.
Mimi pia nahitaji hiyo sheria kwa kweli maana kama sielewi hivi, kwani Controller and Auditor General (CAG) pia anafanya audit kwa kuwa internal audit ni sehemu ya audit. Nahisi kama hatujuwi tunachofanya hapa sana sana tunazidi kumwongezea mzigo masikini mlipa kodi (nchi hii inaendeshwa kwa PAYE) pasipokuongeza efficiency yeyote kama tulivyofanya kwenye EWURA, SUMATRA na upuuzi mwingine unaofanana na huo.
Ni nani amesema kwamba tatizo letu ni kutokufanyika kwa audit? Hili si kweli kwani kila mwaka CAG anareport upotevu wa mabilioni na hakuna kinachofanyika, reports zake tunaishia kufungia vitumbua Kwamtogole.Tungekuwa serious kufanyia kazi reports na recommendations za CAG wala tusingehitaji ofisi mpya ya internal audit, huu ni upotevu wa pesa usio na sababu.
Kuna watu wanapaswa waaishie kwenye ngazi flan za uongozi, hii inatokana na uwezo wao mdogo wa kubeba majukum, kama mtu ni mwoga basi ubora wake unaoonekana kwa sasa ni kwa sababu anariport kwa mtu. Aishie hapo tu. Atafutwe mtu mwingine mwenye kifua cha kufanya maamuzi mazito.
Mwislam Safi, ulamaa aneyejua kazi yake na misingi ya uislam, hongera JK kwa uteuzi huu.