Raila Odinga: Kituo tunachoweka Tanzania ni cha kulinda kura zetu zisiibiwe

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
e58d202d60e5ec4a029225dfb825b58c.jpg
Mgombea Urais wa Muungano wa NASA, Raila Odinga, ametetea hatua ya muungano huo kuweka kituo sambamba cha kuhesabia kura nchini Tanzania akitaja kuwa ni mkakati wa kulinda kura zao.

Kwenye mahojiano Jumatatu, Bw Odinga alishangaa ni kwanini Jubilee ina wasiwasi kuhusu suala hilo, ilhali matangazo halisi yatatolewa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

"Sioni ni kwa nini wenzetu (Jubilee) wana wasiwasi. Lengo letu ni kuhakikisha kuwa tunalinda na kuthibitisha hesabu za kura zinazotolewa na IEBC. Hatuna njama zozote", akasema Bw Odinga akihojiwa na Radio Jambo.

Wakati huo huo, Bw Odinga aliilaumu Serikali kwa kuingilia urafiki wake na Rais John Magufuli wa Tanzania, akisema yeye ni rafiki wa Marais wengine barani Afrika

Marafiki wengine

"Rais Yoweri Museveni wa Uganda ni rafiki yangu wa muda mrefu, hata kuliko Bw Magufuli. Marais wengine kama Alassane Ouatara (Ivory Coast) na Jacob Zuma (Afrika Kusini) kati ya wengine ni marafiki wangu pia. Mbona wanawashwa na urafiki wangu na Bw Magufuli?" akashangaa

Urafiki wa wawili hao ulionekana wazi Bw Magufuli alipohudhuria mazishi ya mwanawe Raila, Fidel Castro, mnamo 2015

Bw Odinga ndiye aliyekuwa kiongozi wa kwanza wa kimataifa kuzuru Tanzania kumpongeza Bw Magufuli baada ya kushinda urais Novemba 2015.

Kwenye mahojiano hayo, Bw Odinga pia alilalamika kuhusu uamuzi wa Mahakama Kuu kuiruhusu kampuni ya Al-Ghurair kuchapisha karatasi za urais akisema mahakama ilifikia uamuzi huo baada ya kutishwa na Serikali

Alidai kuwa kesi yao ilikuwa na ushahidi wa kutosha kuwa kampuni hiyo ina uhusiano na watu wenye ushawishi Serikalini.

"Hata hivyo tuliamua kuheshimu uamuzi wake ili tusivuruge maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8", alisema Odinga.

Chanzo: TaifaLeo
 
Huku ni kuingilia uchaguzi wa nchi nyingine. 2015 CCM ilikataa na kuvamia vituo vya Chadema vya kuhesabia kura ambavyo vilikuwa nchini na kukamata watu na kuvunja vunja computer na watu kukamatwa na computer nyingine kuchkuliwa na polisiccm.

Inakuwaje leo hii Serikali inaiangilia uchaguzi wa Kenya tena kwa kusema uongo na kudai hakuna kituo cha NASA cha kuhesabia kura nchini wakati Raila anasema kipo? MACCM watakubali 2020 Chadema iweke kituo cha kuhesabia kura Kenya?

Acheni unafiki!

Mgombea Urais wa Muungano wa NASA, Raila Odinga, ametetea hatua ya muungano huo kuweka kituo sambamba cha kuhesabia kura nchini Tanzania akitaja kuwa ni mkakati wa kulinda kura zao.

Kwenye mahojiano Jumatatu, Bw Odinga alishangaa ni kwanini Jubilee ina wasiwasi kuhusu suala hilo, ilhali matangazo halisi yatatolewa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

"Sioni ni kwa nini wenzetu (Jubilee) wana wasiwasi. Lengo letu ni kuhakikisha kuwa tunalinda na kuthibitisha hesabu za kura zinazotolewa na IEBC. Hatuna njama zozote", akasema Bw Odinga akihojiwa na Radio Jambo.

Wakati huo huo, Bw Odinga aliilaumu Serikali kwa kuingilia urafiki wake na Rais John Magufuli wa Tanzania, akisema yeye ni rafiki wa Marais wengine barani Afrika

Marafiki wengine

"Rais Yoweri Museveni wa Uganda ni rafiki yangu wa muda mrefu, hata kuliko Bw Magufuli. Marais wengine kama Alassane Ouatara (Ivory Coast) na Jacob Zuma (Afrika Kusini) kati ya wengine ni marafiki wangu pia. Mbona wanawashwa na urafiki wangu na Bw Magufuli?" akashangaa

Urafiki wa wawili hao ulionekana wazi Bw Magufuli alipohudhuria mazishi ya mwanawe Raila, Fidel Castro, mnamo 2015

Bw Odinga ndiye aliyekuwa kiongozi wa kwanza wa kimataifa kuzuru Tanzania kumpongeza Bw Magufuli baada ya kushinda urais Novemba 2015.

Kwenye mahojiano hayo, Bw Odinga pia alilalamika kuhusu uamuzi wa Mahakama Kuu kuiruhusu kampuni ya Al-Ghurair kuchapisha karatasi za urais akisema mahakama ilifikia uamuzi huo baada ya kutishwa na Serikali

Alidai kuwa kesi yao ilikuwa na ushahidi wa kutosha kuwa kampuni hiyo ina uhusiano na watu wenye ushawishi Serikalini.

"Hata hivyo tuliamua kuheshimu uamuzi wake ili tusivuruge maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8", alisema Odinga.
 
Aisee nchi yangu serikali yang chama changu cha mapinduzi rais wang magufuli tumefikia huko sasa..hapana hii nchi ni yetu wote tusitafute kuchukiwa na wakenya na kuvunja amani yao kwa ajir ya uswahiba wako na odinga ili hari wengine tunajua odinga hawez kupenya pale ni kelele nying tu kama za lowassa na ukawa 2015
.
.
.
kyenekyaka nkighanile une

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mgombea Urais wa Muungano wa NASA, Raila Odinga, ametetea hatua ya muungano huo kuweka kituo sambamba cha kuhesabia kura nchini Tanzania akitaja kuwa ni mkakati wa kulinda kura zao.

Kwenye mahojiano Jumatatu, Bw Odinga alishangaa ni kwanini Jubilee ina wasiwasi kuhusu suala hilo, ilhali matangazo halisi yatatolewa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

"Sioni ni kwa nini wenzetu (Jubilee) wana wasiwasi. Lengo letu ni kuhakikisha kuwa tunalinda na kuthibitisha hesabu za kura zinazotolewa na IEBC. Hatuna njama zozote", akasema Bw Odinga akihojiwa na Radio Jambo.

Wakati huo huo, Bw Odinga aliilaumu Serikali kwa kuingilia urafiki wake na Rais John Magufuli wa Tanzania, akisema yeye ni rafiki wa Marais wengine barani Afrika

Marafiki wengine

"Rais Yoweri Museveni wa Uganda ni rafiki yangu wa muda mrefu, hata kuliko Bw Magufuli. Marais wengine kama Alassane Ouatara (Ivory Coast) na Jacob Zuma (Afrika Kusini) kati ya wengine ni marafiki wangu pia. Mbona wanawashwa na urafiki wangu na Bw Magufuli?" akashangaa

Urafiki wa wawili hao ulionekana wazi Bw Magufuli alipohudhuria mazishi ya mwanawe Raila, Fidel Castro, mnamo 2015

Bw Odinga ndiye aliyekuwa kiongozi wa kwanza wa kimataifa kuzuru Tanzania kumpongeza Bw Magufuli baada ya kushinda urais Novemba 2015.

Kwenye mahojiano hayo, Bw Odinga pia alilalamika kuhusu uamuzi wa Mahakama Kuu kuiruhusu kampuni ya Al-Ghurair kuchapisha karatasi za urais akisema mahakama ilifikia uamuzi huo baada ya kutishwa na Serikali

Alidai kuwa kesi yao ilikuwa na ushahidi wa kutosha kuwa kampuni hiyo ina uhusiano na watu wenye ushawishi Serikalini.

"Hata hivyo tuliamua kuheshimu uamuzi wake ili tusivuruge maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8", alisema Odinga.
.


.Wakenya ni wajanja sana. Wanapiga kura na kuhesabu wenyewe, hawasubiri kuhesabiwa na tume. Mwaka 2015 watz, muungano flani wa manyumbu walijaribu 'kuhesabu kura' wao wenyewe wakakiona cha mtema kuni. hawakukua kuwa kuhesabu kura ni kazi ya tume ya uchaguzi,
NASA hapa wanataka kuondoa uwezekano wa kuingiliwa na mamlaka kwa kufanya kosa la kuhesabu kura wakati si mamlaka yao. watavuka mipaka ya nchi na hivyo kuondoa uwezekano wa kuzuiwa na vyombo vya usalama katika harakati zao.
Nashangaa nyumbu wa tz hadi leo wanapiga kelele, wakati ni kosa la wazi kuingilia mamlaka ya tume. NASA watafanikiwa kufanya mahesabu ya kura zao kama watatoka nje ya mipaka ya kenya na kupata nchi rafiki.
 
.


.Wakenya ni wajanja sana. Wanapiga kura na kuhesabu wenyewe, hawasubiri kuhesabiwa na tume. Mwaka 2015 watz, muungano flani wa manyumbu walijaribu 'kuhesabu kura' wao wenyewe wakakiona cha mtema kuni. hawakukua kuwa kuhesabu kura ni kazi ya tume ya uchaguzi,
NASA hapa wanataka kuondoa uwezekano wa kuingiliwa na mamlaka kwa kufanya kosa la kuhesabu kura wakati si mamlaka yao. watavuka mipaka ya nchi na hivyo kuondoa uwezekano wa kuzuiwa na vyombo vya usalama katika harakati zao.
Nashangaa nyumbu wa tz hadi leo wanapiga kelele, wakati ni kosa la wazi kuingilia mamlaka ya tume. NASA watafanikiwa kufanya mahesabu ya kura zao kama watatoka nje ya mipaka ya kenya na kupata nchi rafiki.
Hueleweki. Unawasifia wakenya kuwa wajanja na unawaponda watz kwa kilekile ulichowasifia wakenya, hapo ndipo usipoeleweka
 
Hueleweki
  1. NASA ni chama cha siasa nchini kenya
  2. Mgombea uraisi wa NASA ni Raila Odinga
  3. tz ni nchi ya Tanzania
  4. watz ni watanzania
  5. manyumbu ni muungano wa vyama vya siasa tz -UKAWA
  6. Tume ni tume ya uchaguzi Tanzania NEC na tume ya uchaguzi kenya IEBC
  7. mipaka ya nchi ni kuwa nje ya nchi husika
  8. kukiona cha mtemakuni ni kuonja joto ya jiwe ya dola
 
Hili jambo sio jema kwa mustakabali wa taifa letu na jirani zetu. Ni jambo la hatari sana. Ikifika uchaguzi wetu tusililie tu! Nayaona mambo ya Idd Amin, Obote, Nyerere na mgogoro wa TZ na UG. Au DRC , Rwanda, Uganda na M23 na Banyamulenge. Au Liberia, Siera Leone, Charles Tailor, na Vita vya Siera Leone ile ya "blood diamonds". Kuna haja ya kutafakari sana viongozi wangu kama mna mapenzi ya kweli na Tanzania yetu. Ndio maana siku za karibuni kuna migogoro ya chini kwa chini ya kuwekeana ngumu na Kenya kuhusu biashara!!! Nina imani na viongozi wetu mtachukua hatua za busara.
 
July 24, 2017
Nairobi, Kenya

Raila Odinga Interview On Radio Jambo Today With Gidi Na Ghost 7/24/17 (Part 2) | Kenya Election

Question and answer about NASA's parallel tallying plans and centres outside Kenya, please start listening from 26:14'' (minutes)



Source: Raila Odinga Vs Uhuru Kenyatta 2017

c.c Ghazwat
 
  1. NASA ni chama cha siasa nchini kenya
  2. Mgombea uraisi wa NASA ni Raila Odinga
  3. tz ni nchi ya Tanzania
  4. watz ni watanzania
  5. manyumbu ni muungano wa vyama vya siasa tz -UKAWA
  6. Tume ni tume ya uchaguzi Tanzania NEC na tume ya uchaguzi kenya IEBC
  7. mipaka ya nchi ni kuwa nje ya nchi husika
  8. kukiona cha mtemakuni ni kuonja joto ya jiwe ya dola
Amka ukakojoe nje! Usijekuloanisha godoro
 
Back
Top Bottom