Raia Mwema na JamiiForums wanapotosha?

Nimekuwa nikifuatilia huu mjadala tangu mwanzo lakini kwa kifupi ni kuwa kilichoandikwa na mchambuzi aliyetuma thread hii ni wazi kuwa kinauhalisia na kimethibitishwa kwa mifano halisi aliyoitoa katika thread yake lakini pia upotopoto wa majibu na hoja zilizofuata katika kujaribu kuipinga na kuikanusha hoja hiyo ya msingi nao ni mfano mwingine kuwa msingi wa hoja za ALPHA ni imara sana. Inasikitisha kuona kuwa kwa kiasi kikubwa wachangiaji wa hoja hii ambao ni contemporary great thinkers of TZ..,bado wanaususuwavi wa fikra na ugubugubu wa mawazo. Sijui inahitajika lugha gani isemwe ili watu wafahamu kuwa hoja inajibiwa kwa hoja..,lakini ni kwa bahati mbaya kubwa iliyopo kwa great thinkers wa "jamiiyetu" kujibu hoja kwa porojo kisha kujinadi kuwa porojo zao zinanguvu kuliko hoja.

Na wewe uliye great thinker kuliko wengine, hoja hapa ni IPI?
 
Nimekuwa nikifuatilia huu mjadala tangu mwanzo lakini kwa kifupi ni kuwa kilichoandikwa na mchambuzi aliyetuma thread hii ni wazi kuwa kinauhalisia na kimethibitishwa kwa mifano halisi aliyoitoa katika thread yake lakini pia upotopoto wa majibu na hoja zilizofuata katika kujaribu kuipinga na kuikanusha hoja hiyo ya msingi nao ni mfano mwingine kuwa msingi wa hoja za ALPHA ni imara sana. Inasikitisha kuona kuwa kwa kiasi kikubwa wachangiaji wa hoja hii ambao ni contemporary great thinkers of TZ..,bado wanaususuwavi wa fikra na ugubugubu wa mawazo. Sijui inahitajika lugha gani isemwe ili watu wafahamu kuwa hoja inajibiwa kwa hoja..,lakini ni kwa bahati mbaya kubwa iliyopo kwa great thinkers wa "jamiiyetu" kujibu hoja kwa porojo kisha kujinadi kuwa porojo zao zinanguvu kuliko hoja.
 
Nimekuwa nikifuatilia huu mjadala tangu mwanzo lakini kwa kifupi ni kuwa kilichoandikwa na mchambuzi aliyetuma thread hii ni wazi kuwa kinauhalisia na kimethibitishwa kwa mifano halisi aliyoitoa katika thread yake lakini pia upotopoto wa majibu na hoja zilizofuata katika kujaribu kuipinga na kuikanusha hoja hiyo ya msingi nao ni mfano mwingine kuwa msingi wa hoja za ALPHA ni imara sana. Inasikitisha kuona kuwa kwa kiasi kikubwa wachangiaji wa hoja hii ambao ni contemporary great thinkers of TZ..,bado wanaususuwavi wa fikra na ugubugubu wa mawazo. Sijui inahitajika lugha gani isemwe ili watu wafahamu kuwa hoja inajibiwa kwa hoja..,lakini ni kwa bahati mbaya kubwa iliyopo kwa great thinkers wa "jamiiyetu" kujibu hoja kwa porojo kisha kujinadi kuwa porojo zao zinanguvu kuliko hoja.

Mtambo..
 
Tutumie elimu zetu kwa faida ya watu wetu kama ilivyokuwa ahadi za mwanatanu,mojawapo inasema "nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu kwa faida ya wote".tusijifanye ni wachambuzi kwenye mambo ambayo hayawasidii wananchi.
 
kuna kila sababu ya kuendelea kuamini kuwa elimu ya GreTa thINKERS tulionao hapa haitufikishi popote katika safari yetu ya kujiletea maendeleo. Utaligundua hili ukiangalia yale wanayoyasema na kuchangia humu.....!
 
Ngugi nimawazo yake ,kumbuka mantiki inasema ,maneno ya mtu ni mawazo yake hivyo ameonesha dhahiri wasifu wake wa ndani
 
Khe khe khe mchambuzi umerudi ... .... .... ... sasa vipi boss wako EL anasemaje? Wacha giriba zako hapa, naona unaanza kuvuta ngozi ili uwe karibu. Kama ujuavyo mwamba ngozi ... ... .. Hatukatai kwamba JF iko biased wewe unaonaje na biased ya magazeti ya chama na serikali? Hivi wewe unafurahia unapoona kodi za wavuja jasho zinavyotapwanya na vikaragosi wako?

Angalia Brazil jinsi Lula alivyofanya au Chile ambako walimuondoa dictactor? Kuwa mkweli na muungwana au ndio recession imekuumiza na kuamua kurudi?


Khe khe khe enjoy lakini kumbuka hatuwezi kukusahau kwa kutetea makuwadi na mafisadi papa ambao tunawajua.
 
Ukianza kuona mtu mzima analia,basi tafakari sana maana sio kazi rahisi lazima kuna jambo
Hivi mbona hamtaki kusoma nyakati na majira?wanamacho lakini hawaoni,wanamasikio wanajifanya ni viziwi..uuwiiiiiiiiiiii
kama JF ni ero kwao si nao watafute chichiemu forums ili wadiscuss wanayotaka,mbona kila kitu kiko wazi tu jamani...
mfa maji....:A S thumbs_up:


Habari kwa hisani ya Said kinyozi(0716-679116) na Ahmad Mikole(0772-235918)

[I]MWANADIPLOMASIA NGULI NCHINI ATOA KARIPIO KALI KWA RAI MWEMA, MWANAHALISI, JAMII FORUMS[/I]

Lile sakata la vyombo vya habari kutumiwa na wanasiasa kwaajili ya kueneza propaganda za vyama limezidi kushika kasi baada ya leo hii mida ya saa nane mchana msasani jijini Dar es salaam mwanadiplomasia nguli ambaye ana uzoefu wa siku nyingi katika maswala ya kitaifa na kimataifa kuweka wazi kuwa kuna waandishi ambao ni dhahiri kuwa kazi imeanza kuwashinda kwa kuvunja viapo vya taaluma yao na kuanza kutumika kama vyombo vya propaganda vya baadhi ya vyama vya siasa.

SASA HAWA HAWAKUONA DAILY NEWS.......... TOA MAONI JAMAN
Mwanadiplomasia huyo ambaye ameijengea jina Tanzania kutokana na uwajibikaji wake uliotukuka kimataifa alionyesha dhahiri kukerwa na vyombo hivyo vya habari. Huku mkononi akiwa na gazeti la Raia Mwema ambalo linaongozwa na Saed Kubenea na gazeti la Raia Mwema ambalo linaongozwa na Jenerali Ulimwengu ambayo yote hutolewa siku ya jumatano ,gwiji huyo aliyebobea katika mahusiano ya kimataifa anawataja waandishi Johnson Mbwambo,Lula wa Ndali Mwananzela, Godfrey Dilunga na Mwandishi anayetumia jina bandia la msomaji raia ambao wote ni waandishi wa Raia Mwema kuwa waandishi hao hawana hata chembe ya utaifa wala uzalendo kwa maana habari zao zimejikita kwenye kubomoa chama Fulani na kujenga kingine hakuishia hapo alimtaja pia Evarist Chalali ambaye anaishi uingereza kwa kusema kuwa huyu hana nia njema na Tanzania kwani habari zake zinazochapwa kwenye Raia Mwema zina harufu ya uchochezi.

Mwanadiplomasia huyo akiongea kwa masikitiko makubwa alisema waandishi hawa ambao amewataja kuwa wamesahau misingi na kanuni ya uanahabari badala yake kwa staili ya kujadili kwao hoja wamejipambanua kuwa ni wapiga debe wa CHADEMA na Dr slaa huku wao wakiendeleza wakiwaghilibu wasomaji wao kuwa wao ni neutral na hawaegemei upande wowote.

Kwa upande wa Mw3anahalisi mwanadiplomasia huyo anamtaja Saed Kubenea kuwa anataka kujitafutia umaarufu baada ya umaarufu wake kuporomoka kwa kasi ya ajabu na kiwango cha kutisha baada ya watanzania kubaini kuwa habari za gazeti lake la Mwanahalisi nyingi ni za kutengenezwa kutoka redio mbao na ndio sababu kwenye machapisho mbalimbali ya gazeti hilo waandishi huwa hawatajwi badala yake wasomaji wanafanyiwa danganya toto kwa kuandikiwa Na Mwandishi wetu, vilevile anawataja Ndimara Tegambwage ,Joster Mwangulumbi, Mwanakijiji na Ezekiel Kamwaga kuwa wana uandishi mtindo jazba kwani hushindwa kupangilia hoja zao ipasavyo na mara zote hongelea mambo mabaya tu na kamwe hawaandiki kuhusu mema………….. labda tuwaulize wanafanya hivi kwa faida ya nani? anahoji gwiji huyo. Mwanadiplomasia huyo anaenda mbele Zaidi na kuweka wazi kuwa anasikitishwa sana na tabia ya magazeti hayo kujinadi na habari zinazokwenda na vichwa vya habari Na Mwandishi Wetu ambazo mara nyingi huwa ni tetesi zisizo na kichwa wala miguu anatanabaisha gwiji huyo.

Gwiji huyo anatoa karipio pia kwa Jamii Forums kwa kusema kuwa hawapawsi kujiita Jamii Forums badala yake wajiite CHADEMA Forums kwani hoja zinazojadiliwa kwenye mtandao huo hazina hata chembe ya utaifa bali ni matusi kwa serikali na ni kama wimbi la propaganda chafu zinazoendeshwa na CHADEMA.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa mwanadiplomasia huyo anasema vichwa vya habari kama …………Laiti CCM ingetenda ya Nyerere japo robot u……………iliyoandikwa na Johnson Mbwambo kwenye gazeti la Raia Mwema la leo haina tafsiri nyingine ya kifalsafa bali kupandikiza chuki dhidi ya CCM ambacho ni chama kinachoongoza serikali kwaq sasa.

Mwanataaluma huyo aliyebobea katika diplomasia anaweka wazi kuwa waandishi wa habari ni mhimili wa nne wa jamii yoyote duniani lakini ni mhimili wa kwanza wa kujenga taifa lolote duniani hivyo wanahabari wasikubali kutumika kueneza propaganda za vyama vya siasa badala yake wajikite kwenye kuibua hoja za kujenga taifa pia waandike habari za kitafiti ambazo zitasaidia watanzania kujiletea maendeleo na mwishowe amewaasa watanzania kuwapuuza watu hao ambao amesema hawana hadhi ya kusikilizwa kwani wamedhihirisha kuwa hoja zao ni za kubomoa sio kujenga na hawana hata chembe ya uzalendo wala utaifa.
 
Aisee
nimeitembelea hiyo source. jamaa hata heading zao zinakufanya ulie maana hawajui hata nini wanaandika.
Unakuta post kibao lakini comment ni moja tu ambayo inatolewa na mwenye blogu. na nimechunguza nimegundua kwamba mwenye blogu anapost humo kwa majina tofauti maana aina ya uandishi wake haina tofauti na hao news posters wake.

Nadhani alipewa hela na ccm akaaendeleze blog ya kufagilia chama tawala.
Msipoteze muda kujadili hii hoja maana hainamashiko wala reliable source. Wala hayupo huyo mwanadiplomasia Nguli wanayemsema. wala hakuna mazingira ya kuhojiana wala kupeana briefings. Halafu huko msasani wanakokutaja wanajenga chati tu la kufikirika. naamini hii story waliiandaa viunga vya manzese kwenye net cafe. na wameshavuta mkwanja.

Naongezea kusema kwamba. juko kwenye blogu yao hakuna chama chochote kinachotajwa against zaidi ya CHADEMA. yaani jamaa ni wa kupuuzwa big time

Bora umenihabarisha mkuu nilikuwa naelekea huko kwenye hako kablog niangalie kuna nini, kumbe hakuna la maana.
 
https://jamii.app/JFUserGuide you mwanadipromasia..sorry Mod usinifungie ila kaniudhi huyu...TUMECHOKA NA CCM, https://jamii.app/JFUserGuide YOU MWANADIPLOMASIA....

Hii kweli imeenda shule. Bwaahhhaahaaa!
A%20S%20thumbs_up.gif
 
Sijaona majibu stahili ya post hii.Ukweli ingekuwa wakubwa wa jamii forums watoe majibu ya kina na muafaka.Majibu ya" hatudanganyiki" hayana uzito kwa sababu hayakujibu hoja iliyowekwa mbele yetu.

kuna kila sababu ya kuendelea kuamini kuwa elimu ya GreTa thINKERS tulionao hapa haitufikishi popote katika safari yetu ya kujiletea maendeleo. Utaligundua hili ukiangalia yale wanayoyasema na kuchangia humu.....!

I have been crying over the very same issue. JF imekuwa kijiwe, hoja huwa hazijibiwi kwa hoja, ushabiki umejaa, ukiwaza kinyume wewe umekuwa adui!! nadhani baada ya uchaguzi wanaweza kubadilika tena, tukafikiria kama zamani! aibu tupu! mpaka ile ladha ya kuwa unagain kwenye forums imeisha. JF imevamiwa but believe me, real great thinkers will arise, makapi yatajitenga pembeni na jukwaa letu litasonga mbele, yaani imefika muda hata wa kujua nani umjibu na nani usimjibu! kuna tatizo somewhere na hii inaendelea kuzaa mi-blog mingi sana maana watu wanakuwa hawapati ile ladha.

JF will rule, these whacky members will die naturally, you wait!
 
CCM wanasema hatudanganyiki
Chadema nao wanasema hatudanganyiki

sasa nani anadanganyika???????????????
 
Back
Top Bottom