Kila kitu kinawezekana!. Nenda Arusha, mitaa yote mbele ya soko la Arusha ni nyumba za wasomali watupu!, wamezaliwa Arusha, wamekulia Arusha na watafia Arusha! ni Watanzania Wenzetu!.
Nenda umasaini eneo la Ngaramtoni, utashuhudia Wasomali pure, wanaongea Kimasai safi!, wamezaliwa umasaini, wamekulia umasaini na watafia umasaini, ni Watanzania wenzetu!.
Nenda uhindini, kuna watoto wamezaliwa uhindini, wamekulia uhindini lakini hawazungumzi Kiswahili ila ni Wanzania wenzetu!.
Rage ni Msomali Mtanzania mwenzetu!, Kinana ni Msomali Mtanzania mwenzetu na Bashe ni Msomali Mtanzania mwenzetu!. Tusiwasakame bure kutokana na rangi zao!, kuna Warundi, Waganda, Wakenya, Wanyarwanda, Wajaluo, Wazaire, Wamalawi, Wazambia, Wamsumbiji kibao wako kwenye madaraka makubwa serikalini tena wengine mpaka idara nyeti!, wamepose kama Watanzania, hatuwasakami kwa sababu tuu wamefanana na sisi!, kitendo cha kuwasakama Wasomali na Wahindi tuu, huu pia ni ubaguzi mbaya!.
Pasco.