Ni kweli ndugu yangu, wanawake wana kazi sana katika kuyashinda majaribu,
Wakati nipo chuo kuna mwalimu aliniletea hilo zengwe, nilivyomtosa akasema nitakuonesha, nikadhan masikhara, siku naenda kusign course work yake naambiwa sijakamilisha, nikashangaa sana,
Nakumbuka ilikua Ijumaa halafu Jumatatu mtihani, nahoji kwanini anasema jeuri mwenzie kiburi.
Nikasema kumbe hunijui wewe, nilimuangushia kilio cha kujigalagaza, watu wakajaa nikajielezea, aibu ikawa juu yake.
Hiyo ndio ilikua pona yangu, je unadhani ni wangapi wanafanyiwa hayo mambo??