Pwani: Polisi wakamata noti bandia za milioni 13

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,568

Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limekamata noti za fedha zenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 13 za bandia pamoja na Mtambo wa kutengeneza pesa hizo Maeneo ya Goba jijini Dar es salaam ambapo baadhi ya noti hizo zilishaanza kutumika mitaani ikiwemo Msata, Chalinze Mkoani Pwani

Tukio hilo limekwenda sambamba na kuwakamata watu wanne wanaotuhumiwa kuhusika na mnyororo wa matumizi na uzalishaji wa noti hizo bandia.

Baadhi ya wakazi mjini Kibaha wamesema hawajui noti bandia ni ipi na halali ni ipi kutokana na kutojua utofauti wake kirahisi machoni.
 
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limekamata noti za fedha zenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 13 za bandia pamoja na Mtambo wa kutengeneza pesa hizo Maeneo ya Goba jijini Dar es salaam ambapo baadhi ya noti hizo zilishaanza kutumika mitaani ikiwemo Msata, Chalinze Mkoani Pwani
Kwa jinsi walivyo, hizo noti hata wao watakuwa wamezitumia bila kujua
 
Hata me nataka huo mtambo wa kufyatua pesa bandia. Maisha magumu nimechoka nkipata nafyatua trillion 50 naenda deposit bot ama world bank
Pesa bandia haipelekwi benki mkuu.
Ukiwa na huo mtambo we print noti, kuwa unaenda kwa wakala tofauti tofauti, wale wadogo ambao hawana mashine za kuhesabu hela, unadeposit elfu 50 au pungufu ya apo, kuwa na line kama 5 au 10, fanya hivyo maeneo tofaut tofaut using'ang'anie eneo au mji mmoja utakuja kamatwa kizembe
 
Mambo yote yaliyokuwa yamekithiri katika utawala wa Kikwete yamesharudi katika utawala huu

Pesa bandia kufyatuliwa
Mizigo bandarini haitoki Kwa wakati
Umeme kukatika katika ovyo
Ajali za barabarani
Watumushi wa uuma hawana nidhamu
Ujambaazi

R.I.P Magufuli
 
Back
Top Bottom