bravocharlie
JF-Expert Member
- Feb 1, 2020
- 861
- 849
Huu ushauri naweza ufata hata nikiwa siumwi kama brother hapoAcha kutumia stimulants zozote iwe kahawa, energy drinks, bangi mpaka uondoe hiyo vasocontriction hasa kwenye coronary arteries. Badala yake tumia kitunguu saumu.
Uwe unasaga kitunguu saumu (punje mbili kabla ya kulala) halafu unaweka paste yake kwenye kisahani na kukinusa kwa dakika 15 - 20, yaani unakishika (kisahani) mbele ya pua na kukihemea. Baada ya hapo, weka hiyo paste kwenye glasi ya maji, ikoroge na kunywa. Unaponusa kitunguu, harufu yake inaingia kwenye mapafu na damu mara moja.
Kitunguu saumu kina kemikali nyingi sana ikiwemo allicin ambayo inasifa ya kutanua mishipa ya damu (vasodilator). Pia ina sifa nyingine ya kuzuia damu kuganda (anticoagulant). Pamoja na kuyeyusha mafuta (cholesterol) kwenye mishipa ya damu na kusaidia glucose homeostasis. Fanya hivi kila siku kwa wiki mbili halafu nenda tena kafanye vipimo kwa daktari wako.
Kwa kuongezea tuu sifa hizi za kitunguu saumu pamoja na sifa nyingine nyingi ambazo sijazitaja, zinasaidia kuzuia virusi vya Corona visienee mwilini. Virusi vya Corona huwa vinaua mtu kwa kugandisha damu (microemboli).
Kwa wale waliowahi kuugua Corona (nikiwa mmoja wapo) watakuambia jinsi maumivu waliyoyapata kwenye mapafu na kwenye misuli ya mabegani kunakosababishwa na vipande vidogo vidogo vya damu vilivyoganda (microemboli). Kama vipade hivi vitakuwa vingi vitafanya mwili uhamaki na kutengeneza kitu kinachoitwa cytokine storm (mwili unajimaliza wenyewe).
Naona its cheap na ina faida nyingi