PS wangu ananitega

PS wangu ananitega

Wapendwa wana JF mwenzenu nimekwepa majaribu mara kadhaa kutoka kwa secretary wangu hua ananitega mara kwa mara, majuzi nilikuwa Iringa safari ya kikazi akanipigia simu saa tano za usiku baada ya kunisalimia akaniuliza vipi habari za Iringa?

Nilimjibu huku salama ila baridi ni kali sana ndipo alipo niambia kwanini hukuniambia tusafiri wote? nilibaki kimya huku nikisubiri aniambie tatizo la kunipigia simu usiku ule , akaishia kusema haya nilitaka kukusalimia tu ila usikose kuniletea zawadi.

Nilipo rudi akawa ananiangalia kwa macho ya kulembua kila anapo ingia ofisini. Kuna siku nimempa kazi ya kuchapa barua alipo maliza akaniletea laptop ili nii proof read ile barua akasimama nyuma ya kiti changu na kunigusisha nyonyo zake kwenye bega la kulia ,nilijikausha kama sioni kitu pamoja na kuwa mwili wangu ulipatwa na mfadhaiko.

Ilipo fika muda wa chai nilipo maliza kunywa chai nikanawa mikono akanifuta mikono kwa kutumia kitaulo kidogo wakati sio utaratibu ulio zoeleka.

Jana wakati ninatoka ofisini akasimama mlangoni kama vile anataka kunizuia nisitoke ,mimi nikasimama kusubiri anipishe akaniangalia usoni kwa sekunde kadhaa na baadaye akatoa bonge la tabasamu, nikaendelea kumuangalia akakimbia huku anacheka. jamani hii kama si mitego ni nini?
Dawa yake ni nini?
According Code of Ethics and Conduct for the Public Service in Tanzania;
6. A Public Servant shall refrain from having sexual relationships at the workplace. Likewise he/she will avoid all types of conduct which may constitute sexual harassment which include:-
i) Pressure for sexual activity or sexual favors with a fellow employee;
ii) Rape, sexual battery and molestation or any sexual assault;
iii) Intentional physical conduct which is sexual in nature such as unwelcome touching, pinching, patting, grabbing and or brushing against another employee's body, hair or clothes;
iv) Sexual innuendoes, gestures, noises, jokes, comments or remarks to another person about one's sexuality or body;
v) Offering or receiving preferential treatment, promises or rewards and offering or submitting to sexual favours
 
THE ME ME ME GENERATION!
Tatizo la kupewa madaraka mkiwa bado makinda. Ikiwa issue trivial kama hii inakusumbua, je utaweza ku-handle changamoto za kazi weye!NONSENSE KABISA.

Age has nothing to do with ability to manage love affairs. Wapo wazee kibao wameshindwa kumudu love affairs. Hata baadhi ya viongozi wako wanaoonekana wana busara hili limewashinda. Fanya tafakuri utabaini.
 
Ndoa haina formular Bro. kama wote mko single basi na wewe mtege katika kumnasa kwenye pingu za maisha.
 
unamchekea, atakuwekea dawa utasahau hadi watoto wako, utafukuza familia yako yote nyumbani na yeye atajenga kwao kwa kupitia wewe. kama hauamini maneno yangu suburi utaona.
 
big bosss umekwama... just tell her kwamba mapenzi na kazi amna hapa.... na hapa kazi tuu mapenzi kwake.....
 
Wapendwa wana JF mwenzenu nimekwepa majaribu mara kadhaa kutoka kwa secretary wangu hua ananitega mara kwa mara, majuzi nilikuwa Iringa safari ya kikazi akanipigia simu saa tano za usiku baada ya kunisalimia akaniuliza vipi habari za Iringa?

Nilimjibu huku salama ila baridi ni kali sana ndipo alipo niambia kwanini hukuniambia tusafiri wote? nilibaki kimya huku nikisubiri aniambie tatizo la kunipigia simu usiku ule , akaishia kusema haya nilitaka kukusalimia tu ila usikose kuniletea zawadi.

Nilipo rudi akawa ananiangalia kwa macho ya kulembua kila anapo ingia ofisini. Kuna siku nimempa kazi ya kuchapa barua alipo maliza akaniletea laptop ili nii proof read ile barua akasimama nyuma ya kiti changu na kunigusisha nyonyo zake kwenye bega la kulia ,nilijikausha kama sioni kitu pamoja na kuwa mwili wangu ulipatwa na mfadhaiko.

Ilipo fika muda wa chai nilipo maliza kunywa chai nikanawa mikono akanifuta mikono kwa kutumia kitaulo kidogo wakati sio utaratibu ulio zoeleka.

Jana wakati ninatoka ofisini akasimama mlangoni kama vile anataka kunizuia nisitoke ,mimi nikasimama kusubiri anipishe akaniangalia usoni kwa sekunde kadhaa na baadaye akatoa bonge la tabasamu, nikaendelea kumuangalia akakimbia huku anacheka. jamani hii kama si mitego ni nini?

Dawa yake ni nini?
Pole umeshategeka tayari!!!! Kwa kifupi amekusoma weakness yako!!!! Kawaida kama wewe ni mtu uko serious kikazi hawa wadudumu or support wanakaa mbali na wewe tena wanaambiana kabisa kuwa yule boss hana mchezo!!! Sasa amua kubadilika kabla chumba cha ofisi yako hakijajeuka danguro.
 
Dawa ake muombe 0653..naamin atakimbia na ataandika barua ya kuomba likizo
 
Hii ndo dawa ya kutegua TEGO lenyeweeee
j.jpg
 
mpotezee mkuu hakutakii mema na familia yako.ila kama hujaoa mfanye mke tu sio mbaya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom