Graduate mlioenda VETA mnaendeleaje?
Tarehe 7 Agosti 2025, Waziri Mkuu wa wakati huo, Kassim Majaliwa, aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha vijana wanapelekwa kwenye mafunzo ya ufundi stadi yanayoratibiwa na VETA na Ofisi ya Waziri Mkuu. Alisisitiza kuwa lengo ni kuwapa vijana ujuzi wa kuajiriwa au kujiajiri.
Mimi tokea makuzi yangu yoote sijawahi kuona fundi mwenye financial freedom, sjjawahi kuona nilipokuwa mdogo kuna jamaa alikuwa ni fundi wa gari la pale home imepita miaka 20 sasa hakuna chochote anachokimiliki naona maisha yake ni magumu tu.
The same na mjomba wangu alikua fundi mechanics mzuri miaka mingi iliyopita kamaliza ujana wake wote sasaivi yupo na 63 na hakuna chochote anachokimiliki,
Mimi sijawai kuona fundi aliefanikiwa ni wachache sana ambao waliingia kwenye mfumo wa kubadilisha ufundi kuwa biashara nb wachache sana, shida ya hapa Tanzania kwa kijana ambae anachipukia kwenye ufundi ni mjuano (nepotism) mimi nikiwa na kazi nitamtafuta mtu ninayemfahamu anifanyie kazi , unajifunza labda umeme wa magari au mechanics au umeme wa majumbani, nani atakayekupa kazi? Je uwezo wa kufungua workshop yako unao?
Mkombozi kwa vijana ni kuwekeza upande sahii, kuwaelekeza upande sahii ambao ni productive nimeona kwenye biashara watu wengi wakianzia chini kabisa, mpaka kufikia kiwango kikubwa mno, nimeona watu wakilima mpaka kumiliki tractor zao binafsi. Lakini sijaona fundi pikipiki, bajaj, tiles, mechanics, n.k akifanikiwa.