Nionyeshe fundi tajiri nikupe ten.
Unamjua Thomas Lyimbo aliyekuwa anagawa maziwa shule za msingi maeneo ya Kimara na Ubungo mojawapo Ubungo Msewe?
Kiwanda chake Cha welding and metal fabrication kipo Kimara Korogwe pale?
Yule ambae alijikuta kwenye anga za FBI sababu ya kuwauzia gesi Al Qaida waliolipua ubalozi wa Marekani Dar Tanzania?
Huyo mmoja tu Ila wapo wengi.
Kaka yangu tumbo moja fundi magari alifanikiwa kujipata akamiliki gari na viwanja kadhaa, gari ya watalii cruiser extended body maarufu War bus.
Ghorofa, dula jumla kubwa la vinjwaji, duka la spare za gari, Car Wash, Bar, n.k.
Mwinge fundi maarufu wa kufunga sound system kwenye magari kule Arusha? Naye kajipata.
Nenda Gerezani Kariakoo kakutane na mafundi tajiri.
Kutoboa na utajiri inategemea juhudi zako na bahati yako.
Kuna matajiri mafundi body za gari na rangi waswahili, wachina, waarabu, na wahindi matajiri sana Dar na Arusha. Bado hujaenda Nairobi.
Kuna fundi electronics , computer n.k. ambao Ni matajiri Tena baadhi Ni authorized dealers wa brand kubwa Kama Dell, HP, Sony, Samsung n.k.
Mtazamo wako dhidi ya mafundi ni wa mafundi wale wa chini ya mwembe ambao wanajitafuta.