Proper recording: Nini kilimbadili Mzee Mwanakijiji?

Proper recording: Nini kilimbadili Mzee Mwanakijiji?

Mbona wanaweza kupata wengi tu wana habari ambao wanaweza kuwasaidia? Miye mchango wangu ndio huu huu. Sipendi siasa kihivyo.
MMK, laiti ni ningekuwa mola wako ningekachukua hako kapumzi toka kwako, tazama ulivyo jeuri, ww unajua kwamba mchango wako ni wa lazima kwa sasa, eti unajibu haupendi siasa, hakika umenikera sana brother, acha utaira MM, Hiki ndicho kipindi unatakiwa kuwa hapa makao makuu ya CDM ili umsaidie Tumaini makene, sasa endelea kula hizo bagger,
 
CHADEMA hata wajipange vipi kuiondoa CCM madarakani kwa sanduku la kura sio rahisi kwa sababu chache zifuatazo:
-Mfumo wa sasa wa uchaguzi inaruhusu hujuma za kila aina hasa kwenye uchaguzi wa Rais;
-Katiba ya sasa ya JMT haijaruhusu mfumo wa vyama vingi kikamilifu. Dalili kwamba tutapata KATIBA MPYA kabla ya 2015 ni finyu sana. Suala Muungano litatuchelewesha sana;
-WATANZANIA kwa sehemu kubwa hawajajiandaa kwa badiliko kubwa la aina hii. Mbaya zaidi wameanza kushughulishwa na masuala mengine ya KIDINI, KIKABILA na hili la MUUNGANO. KIla siku sasa tunaamka na UDINI au MUUNGANO!;
CHADEMA inajadiliwa zaidi humu kwenye mitandao kuliko kwa WATANZANIA wa kawaida. Kila wakijaribu kuwafikia WATANZANIA kunatokea vurugu, mauaji na kadhia za kila aina. Nafasi ya kujipanga kuanzia huko chini wataipataje?
 
Hapa unazungumzia kujipanga hasa. Sidhani kama unamaanisha kuwa hili lifanyike baada ya wao kuingia madarakani. Vizuri sana kuweza kufika hapo.



Kuna baadhi ya vitu ambavyo vinahitaji kujulikana; na hatusemi kila "kitu" kiwekwe wazi. Lakini kuna mambo ya msingi ambayo wapiga kura wanahitaji kujua. Kwa mfano suala la kodi ni suala la msingi sana; je kodi chini ya CDM itakuwaje? nani atalipa zaidi au kidogo, italipwa vipi, n.k; suala la elimu ni muhimu sana: je elimu itakuwaje, itakuwa ni mfumo huu huu bali kuuboresha tu? vipi kuhusu walimu, n.k? suala la usalama siyo linalohitaji baadaye. Je jeshi la polisi chini ya CDM litakuwa hivi hivi? usalama wa taifa je?

Je kuna vitu ambavyo tayari tunajua havifanyi kazi (broken system)? NI vitu gani hivi na tutavibadilisha na kitu gani? Umetumia mfano mzuri sana wa George Bush; lakini Bush alilazimika kufanya hivyo baada ya tukio; je na sisi tunasubiri tukio au matukio gani? Kwa mfano, tayari tunajua ufisadi ulivyo je tutakabiliana nao vipi? Tutaenddlea na TAKUKURU hiihii?

Suala uliloliema hapo juu kwangu ni la msingi sana na natamani ulirudie tena na tena. CDM inahitaji kuanza mapemza zaidi kukusanya wadau mbalimbali kuweza kubadilishana mawazo na kufanya brain storming. Kwa mfano -utanisahihisha kama siko sahihi - CDM imewahi kukaa na wadau wa sekta ya elimu na kuweza kubadilishana mawazo ili kuupdate sera ya CDM ya elimu? Vipi kwenye sekta ya afya? Hata kwenye suala la nishati; ukiondoa kauli za individual leaders hadi hivi sasa hatujasikia (sisemi kama haijafanyika inaweza kuwa imefanyika) CDM imeandaa warsha au kongamano la wanachama wake na wadau wengine kupitia sekta ya nishati ili hatimaye iweze kujenga sera mpya inayoendana na hali halisi ya sasa.

Badala ya kufanya tulivyofanya 2010 ambapo kikundi cha watu wachache sana ndicho kilichoandaa ilani itakuwa vizuri kama safari ijayo mchakato uanze mapema sana. Ikumbukwe kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa ni 2014;huu ni 2012 mwishoni, mwaka 2013 kuna uchaguzi mkuu wa CDM na miezi mitatu mingine ya Bunge na mambo mengine. Je kutakuwepo na muda wa kujipanga kihivyo? Tayari tumeona distractions za kugombea urais; itakuwaje kwenye kugombea nafasi za uongozi wa chama?

Mzee MM niko pamoja na wewe katika msimamo ulionao wa CDM kujipanga kabla ya kuingia madarakani na kuonesha nini watawafanyia watanzania baada ya CCM kuondoka madarakani.Isiwe tu kupiga kelele za kuiondoa CCM madarakani bila kujua nini hatma ya watanzania baada yake.

Hapo kwenye RED ndipo tatizo langu na wewe linaanza. Suala la USIRI wa mikakati waliyonayo CDM. Na swali langu kwako ni rahisi tu,kwa mfumo wa Siasa zetu za kurukiarukia mambo bila kuwa na sera maalum zinazoeleweka za vyama, CDM wakitangaza mambo yote hayo hadharani na CCM wakayabeba kama yalivyo na kuyatekeleza kutakuwa na sababu gani sasa ya kuiondoa? Maana wanayoyataka watanzania CDM wameyawasilisha na CCM imeyafanyia kazi.Kwa maneno mengine unataka CDM iwe Think Tank ya CCM?

Hoja ambazo zimekuwa zinatolewa na wanaotaka kuiondoa CCM madarakani ni kuwa imechoka, haina jipya la kuwafanyia wananchi kutokana na kuchoka kifikra. Sasa kikipatikana Chama (Na kwa maana hiyo CDM) ambacho kitakuwa kinafanya kazi ya kuumiza kichwa namna ya kuongoza dola kwa niaba ya CCM na kukimwagia mikakati hiyo maana yake ni kutaka CCM iendelee kutawala milele.

Jambo jema ni lipi sasa, kuruhusu CDM iendelee kuumiza kichwa na kuimwagia CCM mikakati hiyo ili iendelee kutawala au CDM iwe na 'general promise' kwa wananchi huku ikijipanga kwa siri namna ya kumaliza makovu yaliyosababishwa na CCM?
 
Na swali langu kwako ni rahisi tu,kwa mfumo wa Siasa zetu za kurukiarukia mambo bila kuwa na sera maalum zinazoeleweka za vyama, CDM wakitangaza mambo yote hayo hadharani na CCM wakayabeba kama yalivyo na kuyatekeleza kutakuwa na sababu gani sasa ya kuiondoa? Maana wanayoyataka watanzania CDM wameyawasilisha na CCM imeyafanyia kazi. Kwa maneno mengine unataka CDM iwe Think Tank ya CCM?

He!!! Yaani unataka kutuambia CDM wapo kwa ajili ya madaraka binafsi na sio maendeleo ya Tanzania? Kama CCM wakibadilika wakatenda kile kinacholeta maendeleo, hilo si bora pia kwa CDM kwa kuwa wanachopigania ni maendeleo ya Tanzania? Na kama ikitokea hivyo, basi acha CDM wawaambie wananchi mnaona, sera zetu ndio zinazofanya kazi, na mkituchagua tuitawaletea sera nyingine nzuri zaidi.

Siamini kwamba ni busara kumuona mtu dereva wa basi la abiria akifanya makosa hatari na kuhatarisha uhai wa abiria wake, na wewe kukaa kimya ili tu upate nafasi ya kusema si mnaona, niliwaambia yule dereva hafai!
 
He!!! Yaani unataka kutuambia CDM wapo kwa ajili ya madaraka binafsi na sio maendeleo ya Tanzania? Kama CCM wakibadilika wakatenda kile kinacholeta maendeleo, hilo si bora pia kwa CDM kwa kuwa wanachopigania ni maendeleo ya Tanzania? Na kama ikitokea hivyo, basi acha CDM wawaambie wananchi mnaona, sera zetu ndio zinazofanya kazi, na mkituchagua tuitawaletea sera nyingine nzuri zaidi.

Siamini kwamba ni busara kumuona mtu dereva wa basi la abiria akifanya makosa hatari na kuhatarisha uhai wa abiria wake, na wewe kukaa kimya ili tu upate nafasi ya kusema si mnaona, niliwaambia yule dereva hafai!

Mkuu soma post yangu yote. Hoja yangu ni hii, kama Dereva huyo ameshindwa kuendesha, jambo jema ni kumsaidia kila mara aendeshe vema wakati ameshindwa kuendesha au njia sahihi ni wewe unayejua kuendesha kuchukua usukani? Maana hakuna quarantee ya yeye kuyafanya kwa ukamilifu maelekezo anayopewa kama angepewa usukani mtoaji mawazo mwenyewe.Ndiyo hoja, usipotoshe.
 
MMKJ ni mtu wa wakuangalia maslahi ya tumbo lake...Msije kushangaa mkiona anawapigia debe Uamsho.
 
MMK, laiti ni ningekuwa mola wako ningekachukua hako kapumzi toka kwako, tazama ulivyo jeuri, ww unajua kwamba mchango wako ni wa lazima kwa sasa, eti unajibu haupendi siasa, hakika umenikera sana brother, acha utaira MM, Hiki ndicho kipindi unatakiwa kuwa hapa makao makuu ya CDM ili umsaidie Tumaini makene, sasa endelea kula hizo bagger,

hayo unayonitakia mimi na Mungu akujalie na wewe; kwani lazima watu kuisaidia CDM? kumbuka hiari yashinda utumwa.
 
Tofauti ya Tanzania na marekani ni kwamba congressmen/women wana access ya information zote za nchi na hivyo vyama vyao pia kuwao na huo ufahamu.haya yapo ktk sheria na wadau wote wanawajibika kutunza hizo siri kwa kutotoa hadharani au hata kuwapati access watu watakaohatarisha usalama wa taifa na raia wao waliopo nje.

Don't forget: Romney has been receiving briefings from the U.S. intelligence community since September 17, as is customary for a presidential challenger in the final stages of a campaign.

Source: 5 things to watch in tonight's debate - CNN.com

Fikiri chukua hatua!
 
Hebu tupanue mjadala kidogo: Je, ni muhimu kuiondoa CCM madarakani na maovu yake sasa hivi au muhimu kwanza ni kuiondoa CCM madarakani na mengine yatafuata baadaye? Kama lengo ni kuiondoa CCM madarakani na sio lazima kuondoa na maovu yake mara moja, then MMM is right. Otherwise, he is missing the point.

Mimi msimamo wangu siku zote ni wazi kabisa: cha muhimu kwa sasa hivi ni kuiondoa CCM madarakani.

Kitila, MMM bado yupo, labda aliweke wazi mwenyewe. Nilivyomwelewa mimi, ni kwamba anasema kuwaondoa CCM madarakani ndiyo focus ya CDM, na hilo ni kosa.

Nadhani hapo namwelewa na pia nakubaliana naye.

Siku zote napata picha kwamba CDM hawana tatizo na sera za CCM , bali wana tatizo na watawala wa CCM. Kwa kiasi fulani hili wameliweka wazi, japo hawajakili kwa kiwango kinachotakiwa. Kama tatizo ni watawala wa CCM basi CDM watuambie hivyo ili wasije wakaingia madarakani kwa gia ya watawala wabovu wa CCM, na kisha baada ya kuwaondoa watawala wakataka kuondoa sera za CCM ambazo huenda ni nzuri tu.

Au je, CDM wanataka kuwaondoa CCM kwa sababu wanaona sera za serikali ya CCM ni mbaya? Kama ndivyo watuambie pia, ni zipi kati ya hizi sera wanaziona mbaya, na wanataka kuzibadili na kuweka sera za namna gani mbadala? Kwa mfano, japo muungano si suala la sera bali ni la kikatiba, CDM hata siku moja haijawa wazi kabisa kuhusu suala la muungano. Wanamung'unya maneno kuhusu msimamo wao thabiti juu ya muungano. Sera ya madini, CDM wamekazania ufisadi wa mikataba, na hawajasema lolote juu ya sera iliyopo. Hivyo hivyo na suala la nishati, na hata mfumo wa utawala wa nchi. Kwa nini CDM wanaogopa kusema kwa mfano, wakichukua nchi wataondoa nafasi za ukuu wa mkoa na wilaya au kuziacha hizo nafasi na kutoa sababu zao za msingi? Je ni kwa kiasi gani wanatumia mjadala wa Katiba wa sasa kuwaonyesha wananchi wanasimamia mambo gani?

Pamoja na yote, nakiri kwamba CDM wanaelewa sana kwamba Tanzania ina wapiga kura (king makers) wa aina gani. Ni kweli wengi wa wapiga kura wa Tanzania wako katika ushabiki zaidi ya uelewevu wa sera na mwonekano wa mtu - na hii ndio sababu JK alishinda kwa kishindo 2005.

Unfortunately, namwona pia MMM kuwa guilty wa ushabiki huu, kwani tupo tulioona tangu mwanzoni kwamba JK alikuwa kiongozi dhaifu kutokana na utendaji wake wa nyuma, na tulisikitika kuona ushabiki uliokuwa nyuma ya jina lake, na kujua kwamba watu watakuja kuujutia uamuzi wao wa kumuweka JK madarakani kwa sababu tu ya ushabiki waliokuwa nao juu yake (kuna posti niliweka kule Wanajamii juu ya hili). Nimeshangaa sana kuona ilimchukua MMM muda mrefu vile kugundua udhaifu wa JK kama kiongozi wa nchi. Sasa ikiwa mtu msomi kama MMM alikuwa kipofu wa hili, vipi yule mpiga kura wa mtaani!

Hivyo basi, kabla ya kuwasema sana CDM kwamba hawanadi sera katika mihadhara yao, ni lazima tujiulize swali la msingi kama tuna wapiga kura nchini ambao wanaelewa umuhimu wa sera katika mfumo wa vyama vingi vya siasa. Leo hii CDM wakianza kuhubiri sera, wapiga kura watawaelewa? Sikatai kwamba wapo Watanzania wapiga kura wachache wanaoelewa maana ya sera, na hili ni jambo ambalo CDM inapaswa kukumbuka na kutumia forum zinazokubalika kuliongelea. Ukweli ni kwamba kwa namna moja au nyingine CDM wamekuwa wakikwepa kukutana na kujadili issues na wasomi, watu wenye mpanuko wa kimawazo zaidi ya kuongea juu ya ufisadi na kuvua gamba!
 
Mkuu soma post yangu yote. Hoja yangu ni hii, kama Dereva huyo ameshindwa kuendesha, jambo jema ni kumsaidia kila mara aendeshe vema wakati ameshindwa kuendesha au njia sahihi ni wewe unayejua kuendesha kuchukua usukani? Maana hakuna quarantee ya yeye kuyafanya kwa ukamilifu maelekezo anayopewa kama angepewa usukani mtoaji mawazo mwenyewe.Ndiyo hoja, usipotoshe.

Sasa watazamaji na abiria watajuaje wewe unaetaka kuchukua usukani ni dereva bora zaidi ya huyo anayeendesha, ikiwa unaogopa kusema ni nini dereva aliyopo anakosea kwa kuhofia atatumia pointi zako kurekebisha makosa yake?

Yaani wewe unataka uchukue usukani kwa kuwa tu umekuwa hodari wa kusema dereva aliyopo ni mbaya, wakati hata siku moja hujawahi kuendesha basi na tukakuona? Tuambie wazi ubaya wake ni nini na wewe ungefanyaje kama ungekuwa dereva.

Ukiwa uwanjani unaangalia mpira badala ya kucheza, kuna makosa Messi wa Barcelona anafanya uwanjani ambayo unaweza kudhani ungekuwa wewe unacheza namba yake usingefanya!
 
Sasa watazamaji watajuaje wewe unaetaka kuchukua usukani ni dereva bora zaidi ya huyo anayeendesha, ikiwa unaogopa kusema ni nini dereva aliyopo anakosea kwa kuhofia atatumia pointi zako kurekebisha makosa yake?

Yaani wewe unataka uchukue usukani kwa kuwa tu umekuwa hodari wa kusema dereva aliyopo ni mbaya, wakati hata siku moja hujawahi kuendesha basi na tukakuona? Tuambie wazi ubaya wake ni nini na wewe ungefanyaje kama ungekuwa dereva.

Ukiwa uwanjani unaangalia mpira badala ya kucheza, kuna makosa Messi wa Barcelona anafanya uwanjani ambayo unaweza kudhani ungekuwa wewe unacheza namba yake usingefanya!

Reflection ya mpira au uendeshaji wa gari ni single grounded and outlooked. Tanua mjadala nje ya gari na uwanja wa mpira. Tunazungumzia uongozi wa dola na mfumo wa siasa wenye mawanda mapana zaidi ya kuonesha utendaji na uwajibikaji.
 
Siku zote napata picha kwamba CDM hawana tatizo na sera za CCM , bali wana tatizo na watawala wa CCM. Kwa kiasi fulani hili wameliweka wazi, japo hawajakili kwa kiwango kinachotakiwa. Kama tatizo ni watawala wa CCM basi CDM watuambie hivyo ili wasije wakaingia madarakani kwa gia ya watawala wabovu wa CCM, na kisha baada ya kuwaondoa watawala wakataka kuondoa sera za CCM ambazo huenda ni nzuri tu.

Umesema vizuri sana hili.. I hope wengi wataelewa.
 
Reflection ya mpira au uendeshaji wa gari ni single grounded and outlooked. Tanua mjadala nje ya gari na uwanja wa mpira. Tunazungumzia uongozi wa dola na mfumo wa siasa wenye mawanda mapana zaidi ya kuonesha utendaji na uwajibikaji.

Lakini hatupaswi kusahau reflection ya mpira na uendeshaji wa gari imetokana na point yako kwamba CDM hawawezi kuweka wazi sera zao kwa kuwa CCM watazitumia na hivyo wananchi wasione haja ya kufanya mabadiliko nchini! Ni kwa kiasi gani hili wazo liko grounded?
 
Unfortunately, namwona pia MMM kuwa guilty wa ushabiki huu, kwani tupo tulioona tangu mwanzoni kwamba JK alikuwa kiongozi dhaifu kutokana na utendaji wake wa nyuma, na tulisikitika kuona ushabiki uliokuwa nyuma ya jina lake, na kujua kwamba watu watakuja kuujutia uamuzi wao wa kumuweka JK madarakani kwa sababu tu ya ushabiki waliokuwa nao juu yake (kuna posti niliweka kule Wanajamii juu ya hili). Nimeshangaa sana kuona ilimchukua MMM muda mrefu vile kugundua udhaifu wa JK kama kiongozi wa nchi. Sasa ikiwa mtu msomi kama MMM alikuwa kipofu wa hili, vipi yule mpiga kura wa mtaani!

Just to reiterate juu ya nilichosema huko nyuma miaka kadhaa iliyopita;


RE: JK bado ang'ara; hivyo basi?‏


Basi katika mazingira haya, kwa nini hatutashangaa kwamba JK bado anan'gara?

Jibu ni rahisi, japo laweza kuwa tusi kwa wengi wa wapiga kura nchini. Ni kwamba uanachama wa vyama vya siasa Tanzania bado uko sawa na uanachama wa klabu za mpira kama Simba na Yanga. Je, Yanga ilipoteza mashabiki pale ilipofungwa 6-0 na Simba? Labda kidogo sana. Basi hiyo ndio hali halisi ya siasa za Tanzania; ni ushabiki zaidi ya sera. Chadema hata wangeuza sera kiasi gani, ni vigumu sana kuwatoa watu toka kushabikia CCM, kama ambavyo Simba hata wacheze vizuri kiasi gani hawataweza kuchukua mashabiki wa Yanga.

Basi huo ndio ujinga wa Watanzania wengi. Ni ujinga kwa sababu wanapaswa kutokana nao kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu. Mmarekani m-Republican anaweza kirahisi kabisa kumuunga mkono na kumpigia kura candidate wa Democrats. Tanzania hilo bado sana.

Njia pekee inayotumika na vyama kuondoa jumuiya ya watu toka ushabiki wa chama fulani na kwenda kingine, japokuwa ina hatari zake, ni kutumia "incidents" zilizosababisha chuki kuelekea chama fulani katika kipindi fulani, sio sera. Kwa mfano, Chedema itatumia suala na sumu ya migodi kule Mara; na wakienda Mbeya labda watasema mnajua nyie watu wa Mbeya hampendwi na Raisi JK ndio maana mkakatiwa umeme; wakienda Kigoma weseme hiki nk.

Lakini ukweli ni kwamba kutangaza sera nchini hakugusi kwa namna yeyote "wajinga" wengi ambao ndio wapiga kura. Watu hawaipigii kura CCM kwa kuwa ina sera nzuri zaidi ya Chadema. Msimamishe mkereketwa wa mtaani wa CCM wakati wowote ule muulize ni sera ipi ya CCM inakufanya upigie kura viongozi wako wa CCM uone atakujibu nini. Huenda hata akakutajia sera iliyogusiwa na Chadema!

In fact, Nyerere aligusa ukweli sana aliposema "suala la msingi sio sura ya mtu, kama unamwona mzuri peleka posa", na kama angefafanua kauli hiyo ungeshangaa ni jinsi gani alituponda watanzania na mtazamo wetu wa kijinga katika kuchagua viongozi wetu. Lakini alitustahi akatuonea huruma katika ujinga wetu.

Vyama vya siasa vinapaswa kujua jinsi ya kujenga development strategies, na jambo moja wakumbuke ni kwamba kushinda uchaguzi katika Tanzania, sera ni kitu kidogo sana.
 
hayo unayonitakia mimi na Mungu akujalie na wewe; kwani lazima watu kuisaidia CDM? kumbuka hiari yashinda utumwa.
MMK, punguza jazba mkuu, Jiulize elimu na ujuzi ulio nao utaisaidiaje TZ 2015? MMK kwa sasa tz imakuhitaji kuliko kipindi chochote, ndg zako tunakuhitaji, njoo tuunganishe nguvu, mimi nimeanza, angalia nimejenga ofisi za CDM matawi 3, kata 1, eti leo mmk unanijibu kizembe kiasi hiki kaka? majibu kama kinder g..., pale makao CDM panakuhitaji,
 
Just to reiterate juu ya nilichosema huko nyuma miaka kadhaa iliyopita;


RE: JK bado ang'ara; hivyo basi?‏


Basi katika mazingira haya, kwa nini hatutashangaa kwamba JK bado anan'gara?

Jibu ni rahisi, japo laweza kuwa tusi kwa wengi wa wapiga kura nchini. Ni kwamba uanachama wa vyama vya siasa Tanzania bado uko sawa na uanachama wa klabu za mpira kama Simba na Yanga. Je, Yanga ilipoteza mashabiki pale ilipofungwa 6-0 na Simba? Labda kidogo sana. Basi hiyo ndio hali halisi ya siasa za Tanzania; ni ushabiki zaidi ya sera. Chadema hata wangeuza sera kiasi gani, ni vigumu sana kuwatoa watu toka kushabikia CCM, kama ambavyo Simba hata wacheze vizuri kiasi gani hawataweza kuchukua mashabiki wa Yanga.

Basi huo ndio ujinga wa Watanzania wengi. Ni ujinga kwa sababu wanapaswa kutokana nao kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu. Mmarekani m-Republican anaweza kirahisi kabisa kumuunga mkono na kumpigia kura candidate wa Democrats. Tanzania hilo bado sana.

Njia pekee inayotumika na vyama kuondoa jumuiya ya watu toka ushabiki wa chama fulani na kwenda kingine, japokuwa ina hatari zake, ni kutumia "incidents" zilizosababisha chuki kuelekea chama fulani katika kipindi fulani, sio sera. Kwa mfano, Chedema itatumia suala na sumu ya migodi kule Mara; na wakienda Mbeya labda watasema mnajua nyie watu wa Mbeya hampendwi na Raisi JK ndio maana mkakatiwa umeme; wakienda Kigoma weseme hiki nk.

Lakini ukweli ni kwamba kutangaza sera nchini hakugusi kwa namna yeyote "wajinga" wengi ambao ndio wapiga kura. Watu hawaipigii kura CCM kwa kuwa ina sera nzuri zaidi ya Chadema. Msimamishe mkereketwa wa mtaani wa CCM wakati wowote ule muulize ni sera ipi ya CCM inakufanya upigie kura viongozi wako wa CCM uone atakujibu nini. Huenda hata akakutajia sera iliyogusiwa na Chadema!

In fact, Nyerere aligusa ukweli sana aliposema "suala la msingi sio sura ya mtu, kama unamwona mzuri peleka posa", na kama angefafanua kauli hiyo ungeshangaa ni jinsi gani alituponda watanzania na mtazamo wetu wa kijinga katika kuchagua viongozi wetu. Lakini alitustahi akatuonea huruma katika ujinga wetu.

Vyama vya siasa vinapaswa kujua jinsi ya kujenga development strategies, na jambo moja wakumbuke ni kwamba kushinda uchaguzi katika Tanzania, sera ni kitu kidogo sana.

Hakuna anayesema vyama visiwe na Development strategies sasa kama vitakuwa havina vitakuwa vinajiendeshaje? Vitakuwa vipo kwa ajili gani sasa? Na ni chama kipi kitakuwa kipo na kinaimba kutaka kuchukua dola kikiwa kimekaa tu bila kuwa na mikakati ya kiutendaji ya nini kitawafanyia wananchi? Ndiyo maana nimesisitiza hapo juu kuwa, ni lazima hao CDM waoneshe beyond doubt uwezo wa kuongoza dola baada ya CCM ingawa hili lazima lifanywe in covert ways huku wakiendelea kuonesha kwa umma kushindwa kwa chama tawala.

Naisisitiza in Covert kwa sababu kuna madai kuwa Chama tawala kimechoka, kimeishiwa ubunifu na hakiwezi kuwapeleka mbali watanzania. Sasa katika mazingira kama hayo yakichanganywa na aina ya siasa zinazoendeshwa na vyama vyetu ya kurukiarukia kila jambo kutokana na kukosa sera madhubuti huwezi ukaruhusu chama cha upinzani kumwaga mikakati yake ya kiutawala. Tatizo lake ni moja tu, itakuwa ni kukisaidia chama tawala kilichoshindwa na kuendelea kukipa uhalali wa kutawala na kuvifanya vyama vya upinzani kuwa vya kudumu.

Sasa hapo kwenye RED unarudia kitu kilekile kulinganisha siasa na mpira wa miguu. Swali moja tu rahisi, tumekuwa tukishuhudia mamia kwa mamia ya wanachama wa chama fulani wakirudisha kadi na kuchukua kadi za chama kingine je hiyo imekuwa ikijitokeza kwenye vilabu vya mpira? Ni lini uliona mamia ya wanachama wa Yanga wakirudisha kadi zao na kujiunga na Simba kisa klabu yao imeshindwa? Jibu unalo.

Ukweli katika siasa ni kuwa huwezi ukaepuka INCIDENTS katika ku win popularity maana zinatokea katika utendaji na utekelezaji wa majukumu ya kisiasa. Na INCIDENTS zinaweza kabisa kuwa chanzo kikubwa cha chama kudondoka madarakani. Kumbuka kazi kubwa ya upinzani si kukisaidia chama tawala kutenda mema na la hasha! Ni kukosoa na kuonesha mabaya kwa umma zikiwemo incidents mbaya zinazojitokeza. Sasa kama wewe unategemea chama cha upinzani kujikite katika kubuni mipango ya maendeleo ya taifa na kukimwagia chama tawala nadhani sasa ni kuugeuza upinzani Think Tank ya kuendesha dola.

Hata hiyo Marekani unayoitaja hapa kampeni zake zinazoendelea sasa zimetawalia na incidence hizohizo. Mfano ni huu, Chama cha Republican kinatumia tukio la kushambuliwa kwa ubalozi wa Marekani nchini Libya na kuuawa kwa Balozi wake kama kete ya kisiasa. Kinadai kuwa chama cha Democratic na utawala wake kimeshindwa kidiplomasia na kiintelijensia. Hiyo ndiyo siasa huwezi kuitofautisha na incidents.
 
Watu wengi sana wamebadilika baada ya kuifahamu "kweli" na "kweli" imewaweka huru. MMM ni mmoja wapo!

Mkuu jibu hili ni sahihi kabisa, wengi tumeijua CCM na kutambua ilivyopoteza mwelekeo baada ya 2005 na mambo yote ya ufisadi kuwekwa wazi.

Hata wenye matumaini kwa CDM walio wengi wamejenga hayo matumaini baada ya 2005!
 
MMK, punguza jazba mkuu, Jiulize elimu na ujuzi ulio nao utaisaidiaje TZ 2015? MMK kwa sasa tz imakuhitaji kuliko kipindi chochote, ndg zako tunakuhitaji, njoo tuunganishe nguvu, mimi nimeanza, angalia nimejenga ofisi za CDM matawi 3, kata 1, eti leo mmk unanijibu kizembe kiasi hiki kaka? majibu kama kinder g..., pale makao CDM panakuhitaji,

Unaweza vipi kufanya kazi na watu wenye hasira za kitoto? Wakikataliwa wafikiria kuua wengine na wanadai wako makao makuu? Si utakuwa utawala wa ajabu huo?
 
Nicholas, unafikiri ni muda gani muafaka ambapo CDM inatakiwa iwe imejiandaa kushinda uchaguzi ujao? Yaani, kuupdate sera zake ili baadaye waandae Ilani ya uchaguzi? Unafikiri muda mzuri ni ule wa mwaka wa uchaguzi mkuu wa 2015, au mwaka wa uchaguzi wa serikali za mitaa 2014? au mwaka wa uchaguzi mkuu wa chama 2013?

Mi mbona naona walichokiweka mwaka 2010 bado ni superior kwa CCM.Ingawa najua mud aukifika utakuwa very suprised kwa watakacho launch.Pia CDM kujibadilishia tuu vitu kwa vile wewe na mimi tumeota tuu kuwa wanahitaji change na change zenyewe ni kama unavyojieleza (hakuna kitu practical kwa jinsi ulivyojieleza) ni kujipinga wenyewe.Unless iwe CCM wameshazimplement CDM wanahitaji prove kuwa hazikuwa porojo.Pengine wanahitaji ongezea vitu vichache vilivyoibuka upya.

Nikuulize tuu, what if CDM wanashinda bila badilisha kitu?Can you prove kuwa watashindwa ongoza nchi?Sometimes ni watengeneza bidhaa ndio hu create demands kwa clients ili kupanua soko.Hembu tuthibitishie kuwa unachopigia kelele hapa si huko kuwalazimisha wananchi wawe na demands for unnecessary things?Kuna theory nyingi sana zimeletwa na wabongo wenye kujiona wanajua sana kujenga hypes za bure sana.Kwa wana technologia huwa wanapenda propose "The next big thing" ila nyingi pia huishia kuwa "the next big failure".So hata wewe hunyimwi kuleta "your next big idea" ila kwa wenye uzoefu wa vitu vinavyopigiwa sana debe halafu vinakuwa disappointment.Wewe unadhani kwanini watu hawaoni kitu kikubwa hivyo katika kelele zako nyingi na hofu ya time kuwa inakimbia?
 
Back
Top Bottom