Propaganda za uongo: Elimu bure, CHADEMA ikishinda

Propaganda za uongo: Elimu bure, CHADEMA ikishinda

Hapo Msumbiji tu Wamakonde, Wayao na Wamakua wakitaka kutibiwa bure na kupata dawa muhimu bure, huwa wanavuka mto kwenda Msumbiji.
 
Mi nadhani alisema hayo kwa sababu alikuwa kwenye kampeni za siasa, maana kwenye kampeni unaweza kuongea chochote ili u-win kura za raia.Kuna mwanasiasa mmoja 2010 alikuwa kwenye kampeni mikoa ya kanda ya kati aliwa promise wananchi wakimchagua ataleta bahari.
 
Mtumisi wetu, umeongea kitu inayouma!
Ndani ya ccm hakuna mwenye nia njema na nchi yetu!...wanachofanya ni kuhakikisha kuwa wanabaki kwenye hatamu, basi!
Lakini shida kubwa ni ya Wananchi...kukosa uelewa wa mambo haya!
Wangeng'amua wangeshalishinda JITU baya hili ccm!...
Ni mkakati endelevu wa ccm kuwafanya wananchi wawe masikini ili waridhike na Tshirt wakati wa uchaguzi!
 
Mimi siyo mwananchama wa CHADEMA mpaka sasa, ila nimekuwa nikiwafuatilia na ninaweza kusema nimeanza kuvutiwa na sera zao, ila kabla sijaamua kujiunga nao moja kwa moja ningependa kufahamu kitu komoja ambacho kwangu ni muhimu kuliko vyote kwa mustakabali wa nchi yetu!

Je ni nini msimamo wa CHADEMA kuhusu elimu yetu? Je, iwapo tutawapa ridhaa ya kuongoza nchi wanatarajia kuendeleza mfumo wetu wa elimu wa sasa kama ulivyo nikimaanisha mfumo wa lugha ya kufundishia kwamba shule ya msingi kiswahili na kiingereza kama somo au wanatarajia kubadilisha na kama wanatarajia kubadilisha ni kwenda mfumo gani?

Naomba wana CHADEMA wanifahamishe hilo, kwani ni muhumi sana kwangu ktk kujua, nchi itachukuwa muelekeo gani pindi tutakapobadilisha uongozi na chama kwa ujumla!
 
Nashangazwa sana na sera za kiini macho za chama cha demokrasia na maendeleo za kuwa kitakaposhika madaraka kitatoa elimu bure, afya bure na maendeleo makubwa huku tukishuhudia wakiwachangisha wananchi pesa nyingi bila kufafanua matumizi yake angali wakipewa ruzuku na misaada toka vyama rafiki, mfano john mnyika anawachangisha wananchi wa ubungo eti kujenga barabara tena kwa mtindo wa kupitia kwenye simu huu ni wizi, raising funds zisizo na pua wala mdomo,kwenye mikutano ya m4c. Nawahakikishia watanzania genge hili la walanguzi tukiteleza kuwapa nchi watatukomba kila kitu.
 
mwalimu nyerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. Chadema (mh slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni propaganda za uongo.

wiki iliyopita nilipoandika thread "chadema ni chama cha propaganda" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha elimu bure kwa watanzania wote.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa kilimanjaro ambako ndio ngome ya chadema ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa chadema aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia tanzania nzima.

mkoa wa kilimanjaro unaongoza tanzania nzima kwa kuwa na shule za sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya tanzania. Una sekondari 288 wakati hata dar es salaam ina sekondari 252 tu (chanzo: www.moe.go.tz/nectaresuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (chanzo: tanzania: Regions, major cities & urban localities - statistics & maps on city population). Pato la kodi la mkoa wa kilimanjaro (rombo, hai, mwanga, same, mosho mjini na moshi vijijini) ni 14,236.4 milioni (tzsh) wakati lile la dar es salaam ni 441,000.5 milioni (tzsh) (chanzo: tanzania revenue authority - kigoma).

kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa chadema akisaidiana na wapambe wake hapa jf wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake elimu bure kwa watanzania wote ni propaganda ya uongo. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.
kama sasa hivi tu cdm inawachangisha wananchi pesa za kufanyia uhuni na kuongeza wake je wakishika nchi naamini hata bahari itagawiwa wiwanja
 
kwenye hizo hesabu zako tafadhali weka zile trilioni 13 zilizoko kwenye mabenki ya ulaya alafu endelea kutiririka.
 
Tanzania haikutembea magoti kwa sababu Nyerere alitoa elimu bure. Tanzania tulianza kutembea magoti baada ya vita vya Idi Amin. Be factual.

Tanzania ilianza kuanguka chali lilipotangazwa Azimio la Arusha, miaka mingi kabla ya Vita na Uganda.
 
Halafu hizohizo fedha za halamshauri hao madiwani wa huko wanataka kupigia tripu Rwanda kujifunza usafi!

Ukitaka kuvutia watu waambie neno "bure" au "Free". Chadema walimaanisha "Elimu Bure ikiwa utachangia".
 
Katika vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi mkuu 2010,ni Chadema pekee ndio waliokuwa na ahadi lukuki zisizotekelezeka,kiinimacho. Kutoa ahadi zinazotekelezeka na kisha ukashindwa kutekeleza ni kitu kinawezekana. Lakini kutoa ahadi hewa zisizotekelezeka ndio inaposhangaza,na inapolazimu kuhoji uwezo wa chama hicho kuongoza dola. Na hili lilikuja kudhihirika kuwa hawa watu walikuwa waongo pale walipowasilisha maoni ya kambi ya upinzani VS bajeti ya serikali mwaka wa fedha 2011/2012. Kwa kawaida bajeti ya serikali huwa ina-reflect ilani ya uchaguzi ya chama husika na hata ahadi wakati wa kampeni. Lakini kwa Chadema ilikuwa contrary na ilani yao,ahadi zao. Hatukusikia elimu bure,wala mfuko wa cement kwa sh.5000/=. Na hicho ndicho wanachokiendeleza mpaka sasa,kutoa ahadi za kuwafurahisha vijana wa vijiweni na wananchi maskini ambao hawana elimu. They dont have an "economic plan". Waulize hata leo hii,economic plan ya Chadema,hawana..hawana.


 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti.
CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.



Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.

Naanza kwa kukuambia hiyo elimu uliyonayo ni sumu haikusaidii kitu.

Wewe nadhani ni mchumi zumbukuku usiyejua taratibu za pato la mahali kama DSM, Kili linavyogawanywa mara linapokusanywa. Kwa sababu hali siyo hivyo kwa taratibu za makusanyo ya mapato.

1. Wakusanyaji ni halmashauri na TRA. TRA hupeleka makusanyo hazina kwenye kapu moja ambalo baadae mgao unafanywa na watawala wa CCM kwa vipaumbele vyao. Kwa upande mwingine halmashauri hupanga matumizi yake kwa uwezo wake wa makusanyo pamoja na kuingiliwa na seikali kuu. (Serikali kuu iliua serikali za mitaa na bado inazishikilia kama luba)

2. "Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti". Kauli hii ni dhahiri inaonyesha ulivyo mvivu wa kufikiri. Kwa taarifa yako ilipovunjika jumuiya 1977 Tanzania tulikuwa tunaongoza kielimu na kiuchumi. Hayo kwa taarifa yako na wapuuzi wenzio yalikuwa sababu mojawapo ya uvunja jumuiya. Njoo kwenye Azimio lenu la Zanzibar lililofuta vipaumbele vya kitaifa na kuweka vipaumbele vya kuvunja maadili. Ulitegemea elimu na uchumi kwenye mfumo holela vizingatie dhana ndogo ya msingi ya kutumia rasilimali kwa kipaumbele cha kitaifa? Mwalimu Nyerere uliye na usongo naye kwa kutoa elimu bure kabla hajafariki aliasa kuwa kweli kuna aliyoyakosea, lakini mazuri yalikuwepo wenzie, wewe na wapuuzi wenzio watawala wachumia tumbo hata yale mazuri mmeyafilimba.

3. Kwa upeo wako mfupi na mahali ulipo unaona ya CDM hayawezekani; kwa bahati mbaya sana huzungumzii mafanikio mbadala kwenye yaliyotajwa kama elimu bure, nafuu ya gharama za ujenzi na utawala wa sheria ambavyo kwa sasa ni bidhaa adhimu.

Nikupe somo kidogo

1. Rasilimali za taifa zinasimamiwa kihuria na kiholela mifano madini, watu, shughuli zote za uchumi na mbaya zaidi ombwe la uongozi la CCM.

2. Ili kuwe na mafanikio katika kufikia elimu na uchumi bora tuache majaribio. CDM hawatafanya majaribio watafanya kweli kama wanavyofanya kweli. Watawala baada ya mwalimu hawakujifunza cho chote toka kwa awamu yake. Walianza majaribio yaliyoshindwa ndiyo maana mtu ama wewe huoni uwezekano wa watu makini ndani ya CDM kutimiza yaliyo kwenye ilani yao. Pia ndiyo maana wewe na wapuuzi wenzio mnahofu ya mabadiriko kwa sababu ndani ya dhamiri zenu mnasutwa na dhulma, ufisadi ambao mnahofu mtapatilizwa

3. Utawala huu na CCM ni batili wenye akili na hekima wanajua. Katika hali hiyo ni sawa na mwamba ngozi anayevutia kwake badala ya wapiga makasia wanaopeleka chombo pamoja. Nina maana baadhi yetu tunaotawaliwa hatuoni chembe ya jitihada ya kitaifa kuendelea pamoja; wewe mwenyewe tafuta pengo la walionacho na wasionacho katika kila kona.

Wimbo wenu wa Maisha Bora kwa kila Mtanzania umeitikiwa na Bora Maisha kwa kila Mtanzania, ule mwingine wa ARI MPYA, NGUVU MPYA NA KASI MPYA YA UFISADI nao umedhihirisha upuuzi unaokinzana na ukweli.

Kwanza una mapungufu ya uelewa wa lugha unapotumia neno propaganda, wenye propaganda ni nyie mlioshindwa kutekeleza majaribio yenu.

Halafu unazungumza sekta zingine ambazo ni za kufikirika kwa sababu hata Rais wako dhaifu hajui maana ya sekta. Mfano mara wachanganye sekta ya elimu na sekta ya elimu ya juu, mara utamaduni nayo ni sekta, mara benki ni sekta. Hiyo yote inatokana na kutafuta umaarufu kwa kwadanganya watu kwa nahau. Huna sekta nyingine labada sekta ya Lumumba

Kwa sasa huu mjadala wewe unatafuta pa kutokea ila tafakari na chukua hatua kwa sababu kwa sasa hata uongo wo wote ukisemwa na CDM watu wataona ni kweli kwa sababu watawala na chama tawala WANANUKA
 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.


NImesoma habari hii yote lakini nashawishika kusema inawezekana mleta mada sio Mtanzania,labda kwa taarifa yake ajue yafuatayo kwa uchache:-
1.Hajui kwamba kuna wanyama wa tz walikuwa wanatoroshwa kupitia KIA kwenda Uarabuni kwa muda mresfu?Je, unajua niasi gani cha fedha kimepotea?
2.Je unjua kuna watu wameficha mabilioni ya fedha huko nje? Unafikiri hizo fedha zimetoka wapi na zinaingiza kiasi gani cha kodi huko ziliko? je, kama zingewekezwa hapa tz tungeingiza kiasi gani?
3.Nikurudishe kwenye bandari yetu ya DSM umesikia ufisad unaofanyika hapo? je, kama ingesimamiwa vizuri tungengiza kiasi ganicha fedha?
4.Tuna madini mengi kuliko Nchi yeyote A. Mashariki na kati je hapo napo kama pangesimamiwa vizuri tungekuwa wapi?
Hao tu tuliowapa kuvuna madini yetu kifisadi wanatoa misaada mingi sana kwenye shule zetu kwa kejeli wakituonyesha kwamba kama tungekuwa wazalendo tungefanya haya na kuzidi.
5.NIngeweza kukueleza mambo ya Tanesco,Tazara,Tippa,reli ya kati,mbuga za wanyama etc..

Raisi Kagame wa Ruanda amewahi kuomba apewe Reli ya kati tu ili kuupaisha uchumi wa tz sasa waweza kuona jinsi sisi tulivyo lala.Hakuishia hapo alienda mbali kwa kuomba hata apewe uwaziri wa bandari tu na Ruanda iko juu kiuchumi.
Nunayo mengi yakueleza lkn nina wasiwasi na upeo wako wakuelewa mambo baomba niishie hapo na wengine waongezee.
 
Ahadi zipi hazijatimizwa, ziseme na kama hazitaisha 2015. Tatizo la viraza wanashani Rais alipotoa ahadi basi ni siku hiyo zinakamilika.Viraza bwana.hata aibu havina kusema, mimi naona mode ukiona kiraza humu ndani toa hakina maana.Ni kupoteza nafasi, nahiyo inahitaji elimu? Mbona asilmia 80% ya ahadi zimekamilka husemi kiraza wewe.
 
Kelele za nini? Mbona hesabu rahisi tu... Nchi tajiri kama hii, itashindikanaje kutoa elimu bure? Kama hamuwezi pisheni, muone majembe yanavyofanya kazi na suala hilo linawezekana! Ninyi mnaona hamuwezi, mnaendelea kung'ang'ana wakati uwezo wenu wa kufikiri umefika mwisho....Mnapiga propaganda humu jf, huku kazi hamfanyi kazi kueneza fitna tu ilhali silaha zote mnazo... Shame on U!
 
Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.
Hii ni akili muflisi kabisa. Hivi slaa alipiga kampeni kuendeleza shule za kilimanjaro?. Suala la ukanda ulililolilete hapa jamvini - Jiulize kwanini CCM unayoitetea wewe tangu uhuru imetoa madaraka makubwa kwa watu wa kanda ya kaskazini zaidi kuuliko mahali pengine? Mawaziri wakuu J.K. Nyerere, J.S. Warioba, E. M. Sokoine, Frederick Sumaye, E. Lowassa na cleopa Msuya (Wote hawa wametoka kaskazini na tena ni wakristo). Wanne tu toka mahali pengine - Salim A. S., (Zanzibar); R. Kawawa (Kusini), S. J. Malecela (Dodoma), M. K. Pinda (Mpanda). HIKI NI CHAMA CHA KIKANDA (CCM).
 
ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.
Mapato ya serikali yakisimamiwa vizuri na ufisadi kudhibitiwa katika maeneo yoyote hakuna kikwazo ktk mpango wa kutoa elimu Bure!.. Kama hili lingekuwa haliwezekani hata mabosi wako wasingezungumzia huduma za bure na pension kwa wazee. Wanaosomesha hivi sasa wanapata wapi fedha za kusomesha watoto wao kama nchi yetu ni maskini kihivyo?.. Serikali itashindwaje?. Wanaosomesha nani anawalipa?..
 
maana kiuchumi haiwezekani
Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe
na shule kupita Dar es salaam yenye
wakazi 2,809,000.

hapo tu nimekuona hufai kabiiiiiiisa, kilimanjaro wazazi wanajua nini maana ya elimu........si dar es salaam wazazi wanawapeleka madrasa watoto...... Badilikeni, si mpaka msubiri serikali iwajengee
 
Back
Top Bottom